Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Matukio biashara. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Matukio biashara. Onyesha machapisho yote

NBC NA SANLAM WASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO


 Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati) akisaini mkataba wa ushirikiano katika ya NBC na Kampuni ya Bima ya Sanlam, jijini Dar es Salaam wiki iliyopita. Kulia kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Tanzania, Manasseh Kawoloka na kushoto kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Tanzania, Khamis Suleman.  Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake ndani ya matawi ya NBC nchini kote Waliosisima kutoka kushoto ni, Meneja Uenezaji Biashara na Masoko wa Sanlam General, Jabir, Kigoda, Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Benjamin Nkaka na Meneja Mkuu Bima Binafsi wa Sanlam Life, Wilson Mnzava. 

 Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati) Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Tanzania, Manasseh Kawoloka (kushoto) na  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Tanzania, Khamis Suleman (kulia), wakifurahi baada ya utiaji saini makubaliano ya ushirikiano. Wa pili kutoka kushoto ni Meneja Uenezaji Biashara na Masoko wa Sanlam General, Jabir, Kigoda, Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Benjamin Nkaka na Meneja Mkuu Bima Binafsi wa Sanlam Life, Wilson Mnzava. Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake katika matawi ya NBC nchini kote
 Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati), akizungumza katika hafla ya utiaji saini makubaliano ya ushirikiano katika ya benki hiyo na Kampuni ya Bima ya Sanlam. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General, Manasseh Kawoloka na kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam Life, Khamis Suleiman. Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake katika matawi ya NBC nchini kote.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam General, Manasseh Kawoloka (kushoto), akisaini mkataba wa ushirikiano katika ya NBC na Sanlam. Katikati ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Filbert Mponzi na kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam Sanlam Life Insurance, Khamis Suleiman.  Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake katika matawi ya NBC nchini kote
 Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati) Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Tanzania, Manasseh Kawoloka (kushoto) na  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Tanzania, Khamis Suleman (kulia), wakifurahi baada ya utiaji saini makubaliano ya ushirikiano. Wa pili kutoka kushoto ni Meneja Uenezaji Biashara na Masoko wa Sanlam General, Jabir, Kigoda, Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Benjamin Nkaka na Meneja Mkuu Bima Binafsi wa Sanlam Life, Wilson Mnzava. Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake katika matawi ya NBC nchini kote

 Ni furaha tu baada ya Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati) Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Tanzania, Manasseh Kawoloka (kushoto) na  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Tanzania, Khamis Suleman (kulia), kusaini  mkataba wa ushirikiano. Wa pili kutoka kushoto ni Meneja Uenezaji Biashara na Masoko wa Sanlam General, Jabir, Kigoda, Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Benjamin Nkaka na Meneja Mkuu Bima Binafsi wa Sanlam Life, Wilson Mnzava. Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake katika matawi ya NBC nchini kote.
 Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati) akisaini mkataba wa ushirikiano katika ya benki hiyo na Kampuni ya Bima ya Sanlam, jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Tanzania, Manasseh Kawokol na kushoto kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Tanzania, Khamis Suleman.  Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake ndani ya matawi ya NBC nchini kote Waliosisima kutoka kushoto ni, Meneja Uenezaji Biashara na Masoko wa Sanlam General, Jabir, Kigoda, Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Benjamin Nkaka na Meneja Mkuu Bima Binafsi wa Sanlam Life, Wilson Mnzava. 
Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Filbert Mponzi (katikati) Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam General Tanzania, Manasseh Kawoloka (kushoto) na  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Tanzania, Khamis Suleman (kulia), wakipiga picha baada ya kutia saini mkataba wa ushirikiano. Wa pili kushoto ni Meneja Uenezaji Biashara na Masoko wa Sanlam General, Jabir, Kigoda, Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Benjamin Nkaka na Meneja Mkuu Bima Binafsi wa Sanlam Life, Wilson Mnzava. Ushirikiano kati ya NBC na Sanlam utawawezesha wateja kupata huduma za kibenki pamoja na huduma za bima za bidhaa zake katika matawi ya NBC nchini kote.

Pata Kifaa Chenye Uwezo Asilimia 99% wa Kuongeza Ukubwa wa Uume....

Handsome up ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa uhakika na bila madhara. Inapatikana kwa @200,000/=tu. PIA kuna Gely ya kupaka @ 120,000/= na Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa kwa wanaume @120,000/=.
Na spray ya kuchelewesha kufika kileleni kwa mwanaume @120,000/=

NB.Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON $ CO. Wasiliana nasi kwa no (+255) 0767447444 au
0714335378.
Follow us
@Markson_beauty_pr

MRADI WA GREEN VOICES WAFANIKISHA UTENGENEZAJI WA JIKO LA UMEME-JUA MOSHI

Mgeni rasmi katika uzinduzi wa jiko la umeme-jua, Robert George, ambaye ni Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Moshi, akisikiliza maelezo ya namna jiko hilo linavyofanya kazi kutoka kwa Mkurugenzi wa Uhawilishaji Teknolojia wa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini – CAMARTEC, Mhandisi Noela Byabachwezi. Kushoto kwa Noela ni mshiriki kiongozi wa mradi wa Green Voices Moshi, Farida Makame. Wengine pichani ni washiriki wa kikundi hicho. Uzinduzi wa jiko hilo lililotengenezwa na CAMARTEC kwa ufadhili wa Green Voices ulifanyika hivi karibuni mjini Moshi.
Jiko la umeme-jua ambalo limetengenezwa na CAMARTEC kwa ufadhili wa mradi wa Green Voices Tanzania kwa ajili ya kikundi cha akinamama wa TAWOCA Moshi. Jiko hilo linafaa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na uharibifu wa mazingira.
Wanakikundi wa TAWOCA Green Voices Moshi wakihakikisha jinsi joto la jua linavyosaidia kupika kwa kutumia jiko la umeme-jua. Kushoto ni mgeni rasmi katika uzinduzi wa jiko hilo, Robert George, ambaye ni Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Moshi.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa jiko la umeme-jua, Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Moshi, Robert George, pamoja na akinamama wakisikiliza maelezo ya namna jiko hilo linavyofanya kazi kutoka kwa Mkurugenzi wa Uhawilishaji Teknolojia wa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini – CAMARTEC, Mhandisi Noela Byabachwezi.
Mhandisi Noela Byabachwezi, mwenye kofia kulia, akionyesha kwa vitendo jinsi jiko la umeme-jua linavyofanya kazi.
Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Moshi, Robert George – kulia – akisikiliza maelezo mbalimbali ya akinamama wa TAWOCA Green Voices Moshi kabla ya kuzindua jiko la umeme-jua.
                                                                                                                  Picha ya pamoja.

VIUNGA vya ukumbi wa Aroma mjini Moshi vimesheheni akinamama wengi katika siku hii ya Jumamosi, kama ilivyo kawaida kwa siku kama hiyo, ambapo wote wanaonekana kuwa na nyuso za furaha kutokana na mijadala inayoendelea.

Lakini tofauti na Jumamosi nyingine ambapo akinamama wa kikundi cha Wamama wa Kahawa ambao ni wanachama wa Tanzania Women Coffee Association - TAWOCA mjini humo kujadili masuala mbalimbali ya ujasiriamali, siku hii inaonekana kuwa ya tofauti kwa sababu licha ya idadi ya akinamama kuongezeka, lakini kuna tukio kubwa na muhimu ambalo limewakutanisha.

"Leo tunazindua rasmi jiko la umeme-jua, yaani parabolic solar cooker, ambalo kupitia udhamini wa mradi wa akinamama wa Green Voices, hatimaye limeweza kupatikana baada ya jithada za miezi kadhaa," ndivyo anavyoanza kuelezea Farida Makame, mshiriki kiongozi wa mradi wa Green Voices wa kikundi hicho, huku akionyesha kifaa kinachofanana na dish kama la satellite ambacho katikati yake kumewekwa sufuria inayong’aa kama taa kubwa ya umeme.

Anasema kwamba, jiko hilo linaweza kupika kila aina ya chakula kwa kutumia mionzi ya jua ya moja kwa moja bila kuathiri mazingira.

"Kwa kutumia jiko hili maana yake huhitaji kutafuta mkaa wala kuni, hivyo kuokoa misitu ambayo inateketea kila siku kutokana na ukataji wa miti kwa ajili ya kutafuta nishati ya kupikia," anaongeza.

Farida, ambaye pamoja na akinamama wengine 14 – wakiwemo wanahabari watano wanawake – walipatiwa mafunzo ya takriban miezi miwili jijini Madrid, Hispania mapema mwaka huu wa 2016, anasema kwamba lengo la kubuni na kutengeneza jiko hilo la umeme-jua ni kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kupambana na uharibifu wa mazingira.

Anaeleza kwamba, haikuwa kazi rahisi kwake kukamilisha ubunifu wake, wazo ambalo aliliwasilisha akiwa mafunzoni, na kwamba ndiyo maana mradi wake umechelewa kutokana na kuhitaji teknolojia zaidi.

"Tumeanzisha huu mradi baada ya kukaa na akinamama wa TAWOCA na kuwauliza changamoto mbalimbali zinazowakabili katika maisha yao, moja ya changamoto ni upatikanaji wa kuni na mkaa, gesi na umeme.

"Kwahiyo tukaangalia kama kuna njia mbadala ambayo akinamama wanaweza kuitumia na ikawa nafuu na pia kiafya, kwa sababu njia ya kutumia umeme-jua ina manufaa sana kiafya, kwa hiyo tukaungana na wenzetu wa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini, CAMARTEC, kwa sababu ndio watafiti wa mashine na zana za kilimo, ili kutengeneza jiko hili linalotumia nishati ya jua," anasema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uhawilishaji Teknolojia wa CAMARTEC, Mhandisi Noela Byabachwezi anasema imekuwa ni fursa kubwa kwao kufanya kazi na mradi wa Green Voices, kwani wameweza kutengeneza kwa mara ya kwanza jiko hilo ambalo limewapa hamasa wahandisi wa kituo hicho kuliboresha zaidi kwani linaonekana kuwa na manufaa makubwa.

Anakiri kwamba, ingawa wanabuni teknolojia mbalimbali ikiwemo kutengeneza majiko na makaushio yanayotumia umeme-jua, lakini hiyo ndiyo mara ya kwanza kwa kituo hicho kutengeneza jiko linalotumia nguvu ya jua moja kwa moja.

"Hivi sasa tunafanya utafiti kama tunaweza kulitengeneza dogo lakini lenye nguvu au kutengeneza jiko linaloweza kukunjwa na kuhifadhiwa kirahisi kwa sababu hili ni kubwa na inakuwa shida ikiwa mtu hana nafasi kubwa ya kuhifadhia," anasema Mhandisi Noela.

Akizungumzia kuhusu ufanisi wake, Noela anasema kwamba, jiko hilo ni rafiki mkubwa wa mazingira na lina uwezo mkubwa wa kupika na hata kuoka vyakula vya aina zote ikiwa tu kutakuwepo na jua la kutosha.

Kwa maeneo kame na yenye jua kali kama mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na hata Dar es Salaam, jiko hilo linafaa sana kutumiwa bila shida, anaongeza mhandisi huyo.

Aidha, anafafanua kwamba, jiko hilo linaweza kupika chakula kwa ajili ya watu wengi na kwamba ni jukumu la jamii kugeukia matumizi ya jiko hilo lisilotumia mafuta wala nishati nyingine kwa sababu siyo tu linapunguza gharama, lakini pia linaokoa misitu kwa vile miti haitakatwa ikiwa watakuwa wanalitumia.

"Jambo jingine la muhimu ni kwamba, upikaji kwa kutumia jiko la umeme-jua mara nyingi hufanyika nje na katika mazingira ambayo yanahitaji matumizi madogo ya mafuta na kuni, au hatari ya ajali za moto na inaokoa afya za wanajamii, hususan akinamama pamoja na kuyalinda mazingira yetu," anaongeza Mhandisi Noela.

"Kama unavyoliona, jiko hili limetengenezwa kwa vifaa maalum vikiwemo vioo, ambavyo vinang’aa na kuakisi mwanga wa jua, vimepangwa kitaalam na mwanga huu unapoakisiwa unakwenda moja kwa moja kwenye sufuria ambayo kutokana na joto lake, chakula chochote kinachopikwa kinaiva bila wasiwasi wowote. Kama jua litakuwepo la kutosha, joto linalozalishwa na jiko hili linaweza kufikia hadi nyuzijoto 400 °C."

Kwa mujibu wa mhandisi huyo, vyakula vinavyopikwa kwa kutumia jiko la aina hiyo ni vyema vikawa katika maumbile madogo ili kusaidia kuiva haraka na kwamba muda wa chakula kuiva unategemea na vifaa unavyotumia, kiwango cha jua, na kiasi cha chakula kinachopikwa.

Faida kubwa za utumiaji wa jiko la umeme-jua zinatajwa kwamba, mbali ya kuokoa mazingira, ni uwezo wa kupika vyakula vigumu, kukaanga nyama, kupika supu, kuoka mikate na kuchemsha maji kwa muda mfupi.

Hata hivyo, jiko hilo linahitaji zaidi uwepo wa jua, kwani ndiyo chanzo cha joto linalofaa kupikia.

Mmoja wa wanakikundi hicho, Esther Moshi, amesema kupatikana kwa jiko hilo kutawakomboa wanawake wengi ambao mara nyingi ndio wanaokabiliwa na changamoto ya utafutaji wa nishati za kupikia kama kuni na mkaa.

"Tunashukuru mradi wa Green Voices kwa sababu unalenga kumkomboa mwanamke kutokana na adha ya upatikanaji wa nishati ya kupikia, kama majiko haya yatatengenezwa kwa wingi na kila familia kulipata, hakika yatakuwa mkombozi na yatasaidia kuokoa mazingira, " anasema.

Fatima Aziz Faraji ni mwenyekiti wa Chama cha TAWOCA, amesema ni muhimu kwa wanawake kuzidisha umoja wa vikundi ili waweze kusonga mbele na akaupongeza mradi huo kwamba utakuwa mkombozi si kwa wanawake pekee, bali jamii nzima.

Mgeni rasmi katika uzinduzi wa jiko hilo, Robert George, ambaye ni Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Moshi, ameupongeza mradi wa Green Voices pamoja na akinamama hao na akahimiza kuwa, ni vyema kutumia teknolojia ambazo ni rafiki wa mazingira.

Amesema akinamama ndio waathirika wakubwa wa matumizi ya nishati za kupikia, na kwamba ndio wanaoongoza kupata madhara kiafya, hasa wanapotumia mkaa na kuni.

"Jitihada hizi za wenzetu wa Green Voices zinapaswa kuongezwa, kwa sababu zinalengo siyo tu kumkomboa mwanamke, bali kulinda mazingira yetu ambayo yanazidi kuteketea kila uchao kutokana na ukataji wa misitu kwa madhumuni ya kutafuta kuni na mkaa.

"Akinamama wanaathirika sana, wengine utakuta macho mekundu kutokana na moshi wa kuni, na wanapokuwa wazee ndio wanaoshambuliwa na watu wengine wasio na utu kwamba eti ni wachawi kwa sababu macho yao ni mekundu, lazima kutumia teknolojia mbadala kuwanusuru mama zetu, " alisema.

Hata hivyo, aliwataka akinamama hao kushikamana pamoja katika shughuli zao ili waweze kujiletea maendeleo, kwani umoja ni nguvu.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Green Voices Tanzania, Bi. Secelela Balisidya, amesema, mradi wa jiko la umeme-jua ni sehemu ya miradi 10 inayotekelezwa chini ya Green Voices ambapo Tanzania ndiyo pekee iliyopendekezwa kutekeleza mradi huo unaofadhiliwa na Taasisi ya Mfuko wa Wanawake wa Afrika, , ambayo inaongozwa na makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandez de la Vega Sanz.

Hata hivyo, taasisi hiyo inafadhili miradi 15 ya wanawake katika nchi 12 barani Afrika ambayo imeonyesha mafanikio, huku mradi wa Green Voices ukitajwa kuwa na mafanikio makubwa katika kipindi kifupi.

Kwa mujibu wa Bi. Secelela, Mradi wa Green Voices unatekelezwa katika mikoa sita ya Tanzania Bara ambayo ni Dar es Salaam, Pwani, Mwanza, Kigoma, Morogoro na Kilimanjaro.

“Miradi hiyo ni kilimo cha miti ya matunda mkoani Kigoma, kilimo cha viazi lishe visiwani Ukerewe mkoani Mwanza, Ufugaji Nyuki mkoani Morogoro na Pwani, ukaushaji wa mbogamboga kwa kutumia nishati ya jua mkoani Morogoro, usindikaji wa vyakula mbalimbali kutokana na muhogo mkoani Pwani, kilimo hai cha mbogamboga, na kilimo cha uyoga mkoani Dar es Salaam, mradi wa majiko banifu mkoani Pwani na mradi huu wa utafiti wa jiko linalotumia nishati ya jua mkoani Kilimanjaro,” anafafanua Secelela.

Anasema, lengo kubwa la mradi wa Green Voices ni kupaza sauti za akinamama kueneza ujuzi wao wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi ili jamii nzima ya kitanzania iweze kujifunza zaidi na kuzitumia mbinu hizo katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Serikali kupitia taasisi na idara zake zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii imekuwa ikiendesha program mbalimbali za mafunzo ya ufundi ikiwemo utengenezaji wa majiko banifu na sanifu kama inayoendelea katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Malampaka wilayani Maswa.

Hata hivyo, bajeti ndogo imekuwa changamoto kubwa kukwamisha kuwafikia wananchi wengi na kuwapatia elimu ya aina hiyo.

KATIBU MKUU (SEKTA YA UJENZI) ATEMBELEA UJENZI WA JENGO LA TATU LA ABIRIA (TERMINAL III), JIJINI DAR ES SALAAM

uje1
Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (kushoto), alipokagua maendeleo ya mradi huo.
uje2
Meneja Mradi wa BAM International ya Uholanzi, Erick Van Zuthem, akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (kulia), alipokagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), jijini Dar es Salaam.
uje3
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga, akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, alipokuwa akikagua mradi huo, jijini Dar es Salaam.
uje4
Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo upande wa kushukia abiria kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (kushoto), alipokagua maendeleo ya mradi huo.
uje5
Mafundi wa umeme wakiendelea na kazi ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), jijini Dar es Salaam. Jengo hilo likikamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua ndege 21 kwa wakati mmoja na abiria milioni 6.
uje6
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga, akifurahi jambo na Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), jijini Dar es Salaam.

KATIBU MKUU (SEKTA YA UJENZI) ATEMBELEA UJENZI WA JENGO LA TATU LA ABIRIA (TERMINAL III), JIJINI DAR ES SALAAM

uje1
Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (kushoto), alipokagua maendeleo ya mradi huo.
uje2
Meneja Mradi wa BAM International ya Uholanzi, Erick Van Zuthem, akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (kulia), alipokagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), jijini Dar es Salaam.
uje3
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga, akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, alipokuwa akikagua mradi huo, jijini Dar es Salaam.
uje4
Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo upande wa kushukia abiria kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (kushoto), alipokagua maendeleo ya mradi huo.
uje5
Mafundi wa umeme wakiendelea na kazi ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), jijini Dar es Salaam. Jengo hilo likikamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua ndege 21 kwa wakati mmoja na abiria milioni 6.
uje6
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga, akifurahi jambo na Mkurugenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Eng. Mohammed Milanga, alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), jijini Dar es Salaam.

MKUTANO WA MWAKA WA WATAALAMU WA MANUNUZI NA UGAVI WAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi nchini(PSPTB)Dk Hellen Bandiho akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Wataalamu unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa AICC jijini Arusha na kusisitiza miiko ya uadilifu katika manunuzi ya umma na sekta binafsi.
Mjumbe wa Bodi ya Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi nchini(PSPTB)Ahmed Kilima akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Wataalamu unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa AICC jijini Arusha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Manunuzi nchini(PSPTB)Dk Clemence  Tesha  akizungumza jambo na wajumbe wa mkutano wa mwaka wa Wataalamu wa taaluma ya Manunuzi na Ugavi unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa AICC jijini Arusha na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka mikoa mbalimbali nchini na wageni kutoka nchi jirani.
Wajumbe wakiwa kwenye ukumbi wa Simba 
Wajumbe wa mkutano ambao ni wana taaluma ya Manunuzi  na Ugavi wakifatilia mada kwenye mkutano huo leo.
Baadhi ya wajumbe wa mkutano wa Manunuzi  na Ugavi wakifatilia mada kwenye mkutano huo leo.
Wajumbe wa mkutano wa mwaka wa PSPTB
Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB,Dk Charles Kimei(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa fani Manunuzi na Ugavi nchini baada ya kufungua mkutano wa mwaka ambao amesisitiza umuhimu wa kufanya manunuzi sahihi yenye lengo la kuokoa fedha za umma.

Route launch today: Harare to Victoria Falls


ae41d820-ce28-4670-9307-fdac36f49253



Harare to Victoria Falls flights start today! 

 
At 2pm CAT today we’ll take off from Harare and fly to the stunning Victoria Falls for the first time!
Tickets are on sale now for this new route, and until 30th November prices start from just Tsh 83,600 one way, including tax (Tsh 44,000 fare, plus Tsh 33,000 taxes and Tsh 6,600 VAT).
Why not combine your trip to Harare with a visit to the beautiful Victoria Falls?

TFDA NA TAASISI YA TRADEMARK EAST AFRICA (TMEA) WAZINDUA MFUMO WA UTOAJI VIBALI KWA MFUMO WA KIELEKITRONIKI

Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi (kulia), akibonyeza kituvye Dar es Salaam leo asubuhi, kuashiria uzinduzi wa mfumo wa utoaji vibali kwa njia ya kielekitroniki (e-portal) ambao utawezesha Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), kuhudumia wateja wake kwa kutumia mtandao wa intaneti. Mpango huo unaendeshwa kwa ushirikiano wa TFDA na Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA)
                                                  Viongozi wakiwa meza kuu wakifuatilia uzinduzi huo.
                                       Wadau mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo ya uzinduzi.
                                                                       Wadau wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Viongozi wakiwa tayari kuzungumza na wanahabari. Kutoka kulia ni Meneja wa Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA), Josephat Kweka, Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi na Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo.
Maofisa Habari kutoka Kampuni ya PR ya PPR, wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo (kushoto), akizungumza na wanahabari.

                                                                                                    Na Dotto Mwaibale

MAMLAKA ya Chakula na dawa nchini (TFDA), imezindua mfumo mpya wa utoaji vibali kwa mfumo wa kielektroniki ujulikanao kama 'e-portal'.

Mfumo huo uliogharimu kiasi cha sh. milioni 300 kwa ushirikiano wa taasisi ya Trademark East Afrika(TMEA) kwa kutoa dola za marekani 250,000 lengo ikiwa ni kuboresha mfumo wa utoaji huduma kwa njia ya mtandao.

Akizungumza Dar es Salaam leo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Donan Mmbando, Dk.Mkuu wa Serikali Muhammad Kambi alisema mfumo huo uliozinduliwa umekuja wakati muafaka kwani utasaiduia kuboresha huduma katika sekta ya afya kwa kuongeza uwazi, ukweli na kwa uharaka zaidi.

"Mfumo huu uliozinduliwa leo utarahisisha katika kufanya maamuzi ya kudhibiti katika utoaji wa vibali vya kuingiza bidhaa nchini na kutoa bidhaa nje ya nchi kwa kuwa wa kuandaa vibali utafupishwa na utaongeza faida katika mamlaka hiyo,"alisema.

Alisema mfumo huo utasaidia kuhudumia wateja na katika kusajili na kufuatilia ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa za chakula,dawa, vipodozi na vifaa tiba sokoni sanjari na kuongeza kiwango cha wateja katika kuzingatia matakwa ya kisheria.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo alisema mfumo huo mpya unatumiwa na watu takribani 300 ambao wamethibitisha kuwa hauna matatizo yeyote kwani lengo la mamlaka hiyo ni kuhakikisha wanapunguza muda wa wateja wao katika kuomba vibali ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za huduma hiyo.

"TFDA inatambua mchango wa TMEA katika kuendeleza mfumo wa e-portal ambao utarahisha ukusanyaji wa takwimu, uchambuzi na uhifadhi wa taarifa za usajili, uratibu na ufuatiliaji wa taarifa za ubora na usalama wa vyakula dawa, vipodozi, vifaa tiba nchini,"alisema.

Mkurugenzi wa TradeMark East Afrika Tawi la Tanzania, Dk. Josephat Kweka alisema mfumo huo utasaidia kuweka mazingira mazuri ya kibiashara hasa katika kuingiza na kutoa bidhaa katika soko la ushindani.

"Portal inatarajia kuongeza kasi ya usajili, kupunguza kwa kiasi kikubwa muda wa kuingiza bidhaa kutoka nje ya nchi na muda wa kusafirisha bidhaa nje ya nchi. Tumewawezesha portal hiyo ili kukuza biashara ya kikanda na ushirikiano wa kiuchumi kwa nchi za jumuia za Afrika Mashariki,"alisema.

Aidha uzinduzi huo ni hitimisho la maboresho ya mfumo huo ulioanza mwaka 2011 ambapo utawawezesha wafanya biashara kuomba na kupata vibali vyote muhimu kwa njia ya mtandao bila kulazimika kufika ofisi za mamlaka hiyo.

KAMPUNI MPYA YA SIMU YAZINDULIWA JIJINI DAR

 Ofisa Biashara wa Manispaa ya Kinondoni, Ananias Kamundu (wa tatu kushoto), akipata maelezo kuhusu bidhaa za kampuni mpya ya simu za mkononi ya Halotel katika hafla ya uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania wamiliki wa Halotel,  Nguyen Thanh Quang na wageni wengine waalikwa.
 Ofisa Biashara wa Manispaa ya Kinondoni, Ananias Kamundu (kushoto), na Mkurugenzi  wa kampuni mpya ya simu za mkononi wa Halotel  Mkoa wa Kinondoni, Alex Thiem (kulia), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo nchini jijini Dar es Salaam leo. Katikati Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania wamiliki wa Halotel,  Nguyen Thanh Quang .
 Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania wamiliki wa Halotel,  Nguyen Thanh Quang akizungumza katika hafla hiyo.
 Biashara wa Manispaa ya Kinondoni, Ananias Kamundu akizungumza akimwakilisha mkuu wa wilaya hiyo aliyetarajiwa kuwa mgebni rasmi.
 Ofisa Biashara wa Manispaa ya Kinondoni, Ananias Kamundu (kushoto), akiagana na  Mkurugenzi  wa kampuni mpya ya simu za mkononi wa Halotel  Mkoa wa Kinondoni, Alex Thiem mara baada ya kumalizika kwa shughulia za uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo. 
 Wasanii wa kikundi cha Mama Afrika wakitoa burudani katika uzinduzi huo.