Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo
 ya Biashara Tanzania (TanTrade), Jacqueline Mneney Maleko (wa tatu 
kushoto) akiongozana na Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na 
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa 
pili kushoto) mara baada ya kuwasili katika viwanja vya maonyesho ya 39 
ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', barabara ya Kilwa, jijini 
Dar.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo
 ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko (wa pili 
kushoto) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa 
Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro 
Rodriguez wakati wakielekea katika banda la Shirika la Umoja wa Mataifa 
lilipo Karume Hall mara tu baada ya kuwasili.
Na Modewjiblog team, Sabasaba
Mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, 
akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea banda la Umoja wa 
Mataifa leo katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba 
amesema Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika utekelezaji wa miradi na
 mikakati ya Umoja wa Mataifa miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki.
Ameongeza kuwa dunia sasa imekuwa kijiji 
kimoja na Umoja wa Mataifa umekuwepo Tanzania hata kabla ya uhuru, hivyo
 unakusudia kuendelea kuwepo kushirikiana na watanzania katika kutatua 
matatizo kwenye Nyanja mbalimbali.
Bw. Alvaro amewataka watanzania 
kusherehekea pamoja miaka 78 ya Umoja hapa nchini kwa kutoa maoni mbali 
mbali na kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.
Amesema kwa pamoja tunahitaji kuzungumzia 
usawa wa kijinsia, masuala ya kisiasa, mabadiliko ya tabia nchi na mambo
 ya kiuchumi kwa ajili ya ustawi wa taifa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya 
Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko, 
ameushukuru Umoja wa Mataifa kwa kufanya juhudi za kusaidia vijana 
kuanzia ngazi za chini kabisa na kuwawezesha kuwa wajasiriamali.
Amesema kitendo cha Umoja huo kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba sambamba na kijana Amos Mtambala waliyemuwezesha kwa kumpatia mafunzo ya sanaa za uchoraji kumeleta hamasa kubwa miongoni mwa vijana wasio na ajira nchini.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro 
Rodriguez akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye banda
 la Shirika la Umoja wa Mataifa katika viwanja vya maonyesho ya 39 ya 
kimataifa ya biashara 'Sabasaba', barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo
 ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko akisaini 
kitabu cha wageni kwenye banda la Umoja wa Mataifa.
 Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa
 Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu, akitoa maelezo  jinsi 
wanavyoelimisha wananchi kuhusiana shughuli mbalimbali za Umoja wa 
Mataifa nchini sambamba na malengo ya millenia yanayofikia kileleni kwa 
Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
 Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez aliyeambata na mwenyeji wake 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan 
Trade), Jacqueline Mneney Maleko walipotembelea banda hilo kwenye 
maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', katika viwanja vya 
Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa 
Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akielezea maeneo ya Program 
mbalimbali za UNDAP yaliyofanikiwa nchini Tanzania kwa Mratibu Mkazi wa 
Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP)
 nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) aliyeambata na mwenyeji wake 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan 
Trade), Jacqueline Mneney Maleko.
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa 
Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akikabidhi taarifa ya mwaka 
ya UNDAP kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara 
Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko (katikati) aliyefuatana 
na Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika
 la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) walipotembelea 
banda la Shirika la Umoja wa Mataifa lililopo Karume Hall.
Mkurugenzi na Meneja mradi wa TUBEGA 
ART ambaye ni mtaalamu wa sanaa za uchoraji, Amos Mtambala, akitoa 
maelezo jinsi alivyowezeshwa kupitia Shirika la Kazi Duniani (ILO) 
kupata elimu inayomwezesha kuwa mjasiriamali kwa kuuza michoro hiyo 
ndani ya banda la Umoja wa Mataifa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez alipotembelea banda la Shirika la Umoja wa Mataifa  
lililopo Karume Hall ndani ya viwanja vya maonyesho ya 39 ya biashara ya
 kimataifa maarufu kama “Sabasaba”.
Afisa Mawasiliano wa Shirika la Kazi 
Duniani (ILO) nchini, Magnus Minja akifafanua jambo kwa Mratibu Mkazi wa
 Mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez kuhusiana na program ya kazi njenje ya 
mradi wa kufundisha vijana katika shughuli za ujasiriamali inayoratibiwa
 na Shirika la Kazi Duniani (ILO) ambapo kijana Amos iliweze kumuinua na
 kujiajiri kupitia sanaa ya uchoraji.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo
 ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko, akionyesha 
kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya karatasi inayotoa 
maelezo ya jinsi ya Watanzania wanavyoweza kushiriki kutoa maoni 
mbalimbali juu ya utendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini 
Tanzania kwa kutuma SMS ambayo ni bure bila malipo yoyote na moja kwa 
moja kumfikia Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini  Alvaro Rodriguez.
Jinsi ya kutuma ujumbe mfupi wa maandishi 
(SMS), kwa kuandika neno UN au UMOJA WA MATAIFA ambapo kwa  watumiaji wa
 mtandao wa  Airtel watatuma ujumbe wao kwenda namba 15453, kwa 
watumiaji wa mtandao wa Tigo  wanatuma kwenda 15055 au 15453 na kwa 
Vodacom ni namba 15055.
Ambapo pia njia nyingine ya kuwasilisha maoni ya moja kwa moja ni kupitia mtandao wa (Online) kwa kubofya link hii http://gpl.cc/UN2
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo
 ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko akizungumza 
na waaandishi wa habari katika banda la Shirika la Umoja wa Mataifa 
ambao wanashiriki maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', 
katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, vilivyopo barabara ya Kilwa, jijini
 Dar. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro 
Rodriguez akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya 
Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko mfuko wenye 
machapisho na vijarida mbalimbali vya Umoja wa Mataifa.
Afisa Utawala wa Wizara ya Ushirikiano 
wa Afrika Mashariki, Suleiman Magoma (wa pili kushoto) akiuliza swali 
kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa 
Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto) wakati 
alipotembelea banda la Umoja wa Mataifa lililopo Karume Hall katika 
maonyesho ya Sabasaba. Kulia ni Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha 
Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama na Wa pili kulia ni Mchumi 
wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Vainess Molle.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro 
Rodriguez akijibu swali la Bw. Suleiman.
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha 
Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akionyesha namna ya kutoa 
maoni ya utendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa Tanzania kwa njia ya 
SMS ambayo ni bure kwa mitandao yote ya simu za mkononi nchini kwa wadau
 waliotembela banda la UN Tanzania.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro 
Rodriguez ajibu maswali mbalimbali yalitumwa kwa njia ya mtandao na 
wananchi katika banda la Umoja wa Mataifa maonyesho ya Sabasaba.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro 
Rodriguez na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara 
Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko katika picha ya pamoja na
 wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wanaotoa huduma katika banda la Umoja 
wa Mataifa maonyesho ya Sabasaba.
Baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja na Mkuu wa UN Tanzania.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni