Kulia
 ni Ofisa Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Uchumi UN, Laura Paez 
akifafanua sehemu ya Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi Barani 
Afrika ya Mwaka 2015 kwa wanahabari jijini Dar es Salaam nchini 
Tanzania. Kushoto ni Ofisa Habari wa Kituo cha Taarifa cha Umoja wa 
Mataifa Tanzania (UNIC), Stella Vuzo.
Ofisa
 Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Uchumi UN, Laura Paez akifafanua
 sehemu ya Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi Barani Afrika ya 
Mwaka 2015 kwa wanahabari jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.
Ofisa
 Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Uchumi UN, Laura Paez akifafanua
 sehemu ya Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi Barani Afrika ya 
Mwaka 2015 kwa wanahabari jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.
Baadhi
 ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini Tanzania 
wakifuatilia uwasilishwaji wa Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi 
Barani Afrika ya Mwaka 2015.
Kulia
 ni Ofisa Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Uchumi UN, Laura Paez 
pamoja na Ofisa Habari wa Kituo cha Taarifa cha Umoja wa Mataifa 
Tanzania (UNIC), Stella Vuzo wakiwa wameshika nakala ya Ripoti ya UNCTAD
 ya Maendeleo ya Kiuchumi Barani Afrika ya Mwaka 2015 mbele ya 
wanahabari.
Baadhi
 ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini Tanzania 
wakifuatilia uwasilishwaji wa Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi 
Barani Afrika ya Mwaka 2015.
Baadhi
 ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini Tanzania 
wakifuatilia uwasilishwaji wa Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi 
Barani Afrika ya Mwaka 2015.
Baadhi
 ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini Tanzania 
wakifuatilia uwasilishwaji wa Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi 
Barani Afrika ya Mwaka 2015.
Ofisa
 Habari wa Kituo cha Taarifa cha Umoja wa Mataifa Tanzania (UNIC), 
Stella Vuzo akifafanua jambo wakati Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya 
Kiuchumi Barani Afrika ya Mwaka 2015 ilipokuwa akifafanuliwa kwa 
wanahabari jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.
KUTOKANA
 na hali ya huduma ya miundombinu ya usafirishaji kuwa duni na ya aghali
 imeshindwa kukuza biashara na uchumi katika kiwango kinachotegemewa 
katika mataifa mengi ya barani Afrika. Sekta ya huduma ya miundombinu 
ambayo ni kichocheo kikubwa katika kukua kwa uchumi imeshindwa kuleta 
mageuzi ya kutosha.
Taarifa
 hiyo imebainishwa katika Ripoti ya UNCTAD ya Maendeleo ya Kiuchumi 
Barani Afrika ya Mwaka 2015 iliyozinduliwa Jijini Geneva na kusoma 
katika baadhi ya mataifa ya Afrika. Akifafanua ripoti hiyo nchini 
Tanzania, Ofisa Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Uchumi UN, Laura 
Paez alisema huduma za miundombinu ni muhimu katika kufikia malengo ya 
maendeleo endelevu yaliyowekwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya 
2016-2030 na kujenga jukwaa kwa ajili ya ukuaji mpana barani Afrika.
Alisema
 katika ripoti hiyo inayotoa mwangaza wa uchumi wa Afrika imebainisha 
huduma za miundombinu kama vile maji na afya zinahusishwa zinahusishwa 
na malengo muhimu ya maendeleo endelevu katika kufikia matokeo ya 
maendeleo ya kijamii na endelevu. Alisema huduma kama vile umeme, 
mawasiliano ya simu na usafiri huchangia katika tija pia huamuwa 
ushindani wa makampuni ya Afrika.
“Afrika
 inawakilisha asilimia 15 ya idadi ya watu duniani lakini inatoa 
asilimia 2.2 tu ya huduma za mauzo ya nje kimataifa, hali hii inaonesha 
kutotumika kikamilifu kwa sekta hiyo,” anafafanua Katibu Mkuu wa UNCTAD 
Mukhisa Kituyi akizungumzia ripoti hiyo ya Maendeleo ya Kiuchumi Barani 
Afrika ya Mwaka 2015.
Aliongeza
 kuwa ripoti ya Maendeleo ya Kiuchumi Barani Afrika ya Mwaka 2015 
inasisitiza umuhimu wa mataifa ya Afrika kukabiliana na changamoto za 
mapungufu mbalimbali katika udhibiti wa sera, ambayo yamechangia 
kukosekana kwa ufanisi wa kuweza kutumia kikamilifu sekta ya huduma 
kuchochea maendeleo ya kiuchumi.
Ripoti
 hiyo pia inabainisha kuwa katika kipindi cha mwaka 2009-2012 sekta ya 
huduma barani Afrika ilikuwa kwa kiwango cha asilimia 4.6 ikilinganishwa
 na asilimia 5.4 katika nchi zinazoendelea. Sekta ndogo za kihuduma 
zilizokuwa kwa kasi zaidi zilikuwa usafiri, uhifadhi na mawasiliano.
Hata
 hivyo sekta ya huduma katika Afrika iliongoza ukuwaji wa pato la taifa 
katika chi 30 kati ya nchi 54 katika kipindi cha 2009-2012, huku kati ya
 nchi 45 ambapo pato la sehemu ya huduma lilipanda, 30 zilipata tatizo 
la kupungua kwa uzalishaji viwandani kuanzia kipindi cha 2001-2004 hadi 
kipindi cha 2009-2012.
Aidha
 alisema baadhi ya nchi za Afrika zimeendeleza huduma za viwanda vyao 
kwa mafanikio na hata zinapeleka huduma zake katika masoko ya Afrika 
huku akizitaja nchi hizo kuwa ni pamoja na Mauritius na Nigeria ambapo 
zinafanya vizuri sekta ya huduma za kifedha na kibenki. Alisema 
kibiashara katika sekta ya usafiri wa anga nchi za Ethiopia, Kenya na 
Afrika ya Kusini zinafanya vizuri huku huduma za elimu ni Uganda, huduma
 za mawasiliano ya simu Misri na huduma za Bandari ni nchi ya Djibouti 
na Kenya.
Baada
 ya ufafanuzi huo ripoti imeshauri masuala kadhaa ikiwemo kuwa na kanuni
 ya ufanisi wa huduma ya miundombinu. Alisema pamoja na hayo mataifa 
mengi yapo chini katika uhuru udhibiti sekta zote na mifano ya viwango 
vya kimataifa vya udhibiti wa miundombinu havitumiki barani Afrika 
ilhali vyombo vingi vya udhibiti vipo katika hatua za awali za maendeleo
 na bajeti ya kawaida na mara nyingi hata hukosa wafanyakazi wenye sifa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni