Tizama:MATUKIO MBALIMBALI KAMA YALIYOTOKEA MJINI DODOMA KATIKA MKUTANO MKUU WA CCM.


Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikumbatiana na Dkt. John Pombe Magufuli, mara baada ya kutangazwa kuwa ndiye Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, mchana huu hapa kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Dodoma Convition Centre, Mjini Dodoma. Dkt. Magufuli ameibuka kidedea kwa jumla ya kura 2104, wakati wapinzani wake Amina Salum Ally, akiibuka na kura 253 na Dkt. Asha-Rose Migiro, akipata kura 59. Viongozi wakuu wameenda kwenye kikao hivi sasa cha kujua nani atakuwa Mgombea Mwenza wa Urais. hivyo tutaendelea kuwajuza zaidi, endelea kuwa jirani na Libeneke lako pendwa la Globu ya Jamii.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Dkt. John Pombe Magufuli kuwa ndie Mgombea Urais wa Tanzania.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mgombea Mwenza wake, Mh. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kumtangaza, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Dodoma Convition Centre, Mjini Dodoma mchana huu.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mh. Samia Suluhu Hassan akipombewa na Spika wa Bunge, Mh. Anne Makinda pamoja na viongozi wengine. Kushoto ni Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni