Kaimu Mganga Mkuu wa 
Serikali, Dk. Mohamed Ally Mohamed (kushoto), akizungumza na waandishi 
wa habari wakati akifungua semina hiyo Dar es Salaam. Kulia ni 
Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Maafa na Dharura, Dk.Elias Kwesi.
Mkurugenzi Msaidizi Kitengo
 cha Maafa na Dharura, Dk.Elias Kwesi (kulia), akizungumza katika semina
 hiyo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali, 
Dk. Mohamed Ally Mohamed kufungua semina hiyo.
Ofisa Mradi wa Usalama 
Barabarani wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Marry Kessy (kushoto), 
akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa mada kwenye semina 
hiyo.
Mkaguzi wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Makao Makuu, Mossi Ndozero (kulia), akitoa mada kwenye semina hiyo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Safe Speed Foundation, Henry  Bantu akizungumza kwenye semina hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Dharura
 na Maafa wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Mary Kitambi akitoa 
mada kuhusu sekta ya Afya inavyokabiliana na changamoto za utoaji huduma
 kwa wagonjwa wanaopata ajali.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa kwenye  semina hiyo.
Wanahabari wakiwa kwenye semina hiyo. 
Na Magreth Kinabo
Imeelezwa kwamba ajali za barabarani yanasababisha  vifo vya watu milioni 1.24 kila mwaka duniani.
Aidha watu kati ya 20 milioni na 50 milioni huumia kutokana na ajali za barabarani.
Hayo
 yalisemwa jana na Mkurugenzi wa Idara ya  Uhakiki  wa Huduma Bora za 
Afya Dk. Mohamed Ali Mohamed  kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii 
kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO)ya mwaka 2013 
,wakati wa semina ya waandishi wa  habari kuhusu usalama barabarani 
iliyofanyika jijini Dares Salaam.
Semina
 ambayo inaambatana na wiki ya Umoja wa Mataifa ya Usalama Barabarani 
ambayo imeanza Julai 9 na kilele chake Julai 15 katika Shule ya Msingi 
ya Uhuru Mchanganyiko iliyopo jijii humo, ambapo mwaka huu imelenga 
kupunguza ajali za barabarani kwa watoto.
Aliongeza
 kwamba  asilimia kubwa (90%) ya vifo vya ajali za barabarani yanatokea 
katika nchi ambazo zina uchumi wa kati na wa chini.
Hali
 ya vifo vinavyotokana na ajali za barabarani kwa nchi ambazo ziko chini
 ya Jangwa la Sahara ni  (24.1 kwa kila vifo 100,000) ukilinganisha na 
idadi ya vifo  kwa dunia nzima (18 kwa kila vifo 100,000). Hii 
inachangiwa kwa kiasi kikubwa na hali mbaya ya barabara zetu.
Alisema
 taarifa ya polisi inaonyesha kuwa katika kipindi cha 2008 mpaka 2013 
nchini Tanzania kumekuwa na magari yaliyosajiliwa ni 500,000 ongezeko 
hili linaenda sambamba na ongezeko la vifo vinavyotokana na ajali 
nchini, kutoka vifo 309 mwaka 2008 mpaka vifo 930 mwaka 2012.
Aidha
 Dk .Mohamed alisema ripoti ya Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini
 (SUMATRA) inaonyesha asilimia 95% ya ajali za barabarani zinasababishwa
 na matumizi mabaya ya barabara.
“Sekta
 ya Afya ina mchango mkubwa katika kukabiliana na majeruhi wa ajali, 
aidha wingi wa ajali na kupelekea majeruhi wengi ni changamoto katika 
sekta ya afya. Madhara yanayotokana na hizi ajali hupunguza maendeleo ya
 nchi.
“Hivyo ni muhimu sote kwa pamoja tuweke juhudi za dhati kupunguza ajali za barabarani,” alisema.
Kwa
 mujibu wa Dk. Mary Kitambi kutoka Wizara hiyo alisema ajali za 
barabarani huigharimu Serikali sh. bilioni 3.4 kila mwaka kwa ajili ya 
matibabu ya watu waliojeruhiwa.
Mwakilishi
 kutoka WHO, ambaye ni Afisa Miradi, Mary Kessi  alisema  kwa mujibu wa 
ripoti ya shirika hilo ya mwaka 2010 watoto 186,300 hufariki kila mwaka 
 kwa ajali za barabarani.
Aliwataka waandishi wa habari  kuripoti kwa kufanya utafiti juu ya vyanzo vya ajli za barabarani badala ya madhara pekee.
Kwa
 upande wake Mkaguzi wa Polis Mossi Ndozero aliwataka jamii kujenga 
tabia ya kutii sheria bila shuruti ili kuweza kupunguza ajali ya 
barabarani na kutoa taarifa  za madereva wanaokiuka sheria za barabara  
kwa kutumia namba za simu 0800 757575 na 0682 88
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni