Katibu
 Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi  
Liberata Mulamula akiwa na  Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa 
Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Katibu
 Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi 
Liberata  Mulamula akiwa na Mkuu wa Utawala,  Bi Lilian Munanka, ambaye 
Balozi  amemwelezea kama Afisa Mkuu Mwandamizi,  mweledi, mchakapakazi, 
 anayejituma na mwajibikaji,   mwenyeuzoefu  mkubwa na nguzo ya 
kutegemewa na ambaye  amewapokea   Mabalozi wengi. 
Katibu
 Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi 
Liberata Mulamula akiwa na  baadhi ya maafisa na wafanyakazi wa 
Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa wakiongonzwa na
  Balozi Ramadhani Mwinyi.
Katibu
 Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi 
Liberata Mulamula, amewaaga watanzania waishio nchini  Marekani,  kwa 
kuwataka kujivunia utanzania wao na kutoionea aibu lugha yao ya taifa,  
 Kiswahili.
Mwishoni
 mwa wiki,   Ubalozi wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania nchini 
Marekani,  uliandaa hafla ya aina yake  ya  kumpongeza, kumshukuru na 
kumuaga  Balozi Liberata  Mulamula ambaye sasa ni  Katibu Mkuu, Wizara 
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Hafla 
hiyo iliyowajumuisha  watanzania wa kada mbalimbali wakiwamo maafisa na 
 wafanyakazi wa Uwakilishi wa Kudumu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
 katika Umoja wa Mataifa, wakiongozwa na   Balozi  Ramadhan  Mwinyi, 
 ilipambazwa kwa nasaha mbalimbali na salamu za kumtakia kheri Balozi 
Mulamula katika  jukumu lake jipya.
Pamoja
 na  kusikiliza salamu kutoka kwa wawakilishi  wa makundi ya  kijamii, 
 na  kupokea zawadi,   Katibu Mkuu, Balozi Mulamula naye alipata fursa 
ya  kuzungumza mawili  matatu.
Katika
  salamu zake  kwa watanzania  waliojumuika katika makazi yake.  Moja ya
 mambo muhimu  aliyoyazungumza ni pamoja na kuwaasa  watanzania waishio 
nchini   Marekani, kujivunia utanzania wao,  umoja wao na kubwa zaidi 
kutoona aibu kuizungumza na kuiendeleza lugha ya taifa Kiswahili.
“Niwaombeni
  jambo moja,  msione aibu kuzungumza lugha yetu, lugha yenu ya 
Kiswahili,  miaka kadhaa iliyopita  watanzania waughaibuni walikuwa 
hawazungumzi  Kiswahili , waliogopa kujitambulisha kwa lugha yao, 
 lakini sasa hali imebadirika sana,  unakutana na watanzania kila kona 
wanazungumza Kiswahili   hili ni jambo la kujivunia sana na ninawaomba  
 tuendeleze utamaduni huu wa kuzungumza Kiswahili, kuwa ugenini 
hakumaainishi  uachane na  lugha yako” akasisitiza Balozi Mulamula na 
kushangiliwa na watanzania.
Katika
  kutilia mkazo  wa lugha ya  Kiswahili,   Balozi  Mulamula aliwataka 
wana DMV kuendelea na darasa la kuwafundisha watoto  lugha hiyo ya 
Kiswahili na  maeneo mengine kuiga mfano huo.
Jambo 
 jingine ambalo Balozi  alililowasisitizia watanzania  hao ni kuhusu 
upendo, mshikamano, kuheshimiana, kusaidia na kutobaguana kwa misingi ya
 dini, kabila,  eneo  ambalo mtu  anatoka au kwa misingi ya itikadi za 
kisiasa.
“ 
Ninaondoka  baada ya miaka miwili ya kuwa   Balozi wenu,  na katika 
miaka hii miwili nimejifunza mengi sana kutoka kwenu, mmeshirikiana nami
  na Ubalozi katika mambo mengi yakiwamo ya kuchangia maendeleo yenu 
wenyewe na maendeleo ya watanzania wenzenu endeleeni na moyo huu”.,
Kaongeza
 “nitakuwa nanyi na kama  mjuavyo  tunakitengo kizima kinachoshughulia 
masuala ya diaspora, na kama ningekuwa mwanasiasa basi  nyie 
wanadiaspora mngekuwa  mtaji wangu,  jimbo langu”. akabainisha na 
kuamsha tena   vifijo kutoka kwa wana-diaspora hao.
Katika
 hatua nyingine,   Katibu Mkuu, Balozi Mulamula amewahimiza  watanzania 
walioko nje, kumchangamkia   hasa kwa wale wenyekutaka kujaza fomu za 
maombi ya pasi zao za kusafiria ambazo zimekwisha muda.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni