Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili katika Uwanja wa
 Ndege wa kijeshi wa Fairbairn mjini Canberra katika siku ya mwanzo ya 
ziara yake Rasmi ya siku nne ya Kiserikali nchini Australia.
 Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembezwa katika jumba 
la Makumbusho ya Taifa ya vita  - Australian War Memorial - mjini 
Canberra zilikohifadhiwa  kumbukumbu mbalimbali ambayo zinazoonesha 
jinsi Australia ilishiriki kwenye vita mbalimbali  katika siku ya mwanzo
 ya ziara yake ya Kiserikali nchini Australi. 
 Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete akiweka shada la maua na kutoa heshima katika 
kaburi la askari wa Australia wakati alipotembelea jumba la Makumbusho 
ya Taifa ya vita - Australian War Memorial - mjini Canberra 
zilikohifadhiwa kumbukumbu mbalimbali ambayo zinazoonesha jinsi 
Australia ilishiriki kwenye vita mbalimbali  katika siku ya mwanzo ya 
ziara yake ya Kiserikali nchini Australia.
Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Watanzania waishio Australia 
alipkutana nao na kuongea nao katika siku ya mwanzo ya ziara yake ya 
Kiserikali nchini Australia. 
RAIS
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete 
ambaye aliondoka nchini usiku wa Jumamosi, Julai 25, 2015, amewasili 
nchini Australia na kuanza  ziara rasmi ya Kiserikali ya siku nne kesho,
 Jumatatu, Julai 27, 2015.
Rais
 Kikwete anafanya ziara hiyo rasmi ya Kiserikali katika Jumuia ya Madola
 ya Australia (The Commonwealth of Australia) kwa mwaliko wa Mheshimiwa 
Jenerali Sir Peter Cosgrove AK MC (Mstaafu), Gavana Jenerali wa Jumuia 
ya Madola ya Australia.
Wakati
 wa ziara yake, Rais Kikwete ambaye mara ya mwisho alitembelea Australia
 kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Serikali wa Nchi za Jumuia ya Madola 
mjini Perth mwaka 2011, atatembelea mji mkuu wa Australia wa Canberra na
 miji ya Newcastle na Sydney.
Mara
 baada ya kuwasili mjini Canberra kesho, Rais Kikwete atapanda Mti wa 
Kumbukumbu katika Bustani ya Taifa ya Miti ya Australia na kutembelea 
Makumbusho ya Taifa ya Vita ya nchi hiyo kabla ya kukutana na Watanzania
 wanaoishi katika Australia. 
Kesho
 kutwa, Jumanne, Julai 28, 2015, Rais Kikwete atafanya mazungumzo rasmi 
ya Kiserikali na Waziri Mkuu wa Australia, Mheshimiwa Tony Abbot (MB) na
 pia kukutana kwa mazungumzo na mwenyeji wake Gavana Jenerali Sir Peter 
Cosgrove ambaye alipata pia kuwa Mkuu wa Majeshi ya Australia. 
Aidha, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa GaiBrodtmann (MB), Waziri Kivuli wa Ulinzi wa Australia. 
Maeneo
 makuu ambako mazungumzo kati ya Rais Kikwete na viongozi hao wa 
Australia yanatarajiwa kujikita ni katika eneo la madini na uchimbaji 
wake, fursa za elimu ya juu na mafunzo ya ufundi, masuala yanayohusu 
Bahari ya Hindi (The Indian Ocean Rim) na usalama wa Bahari hiyo, ugaidi
 na masuala ya usalama wa nchi za Afrika Mashariki. 
Rais
 Kikwete pia atatumia nafasi hiyo kuwashukuru na kuagana na viongozi wa 
Australia, nchi ambayo kwa miongoni mitano iliyopita imekuwa na uhusiano
 wa karibu na Tanzania katika maeneo ya uchumi, ulinzi, siasa, jamii na 
masuala ya usalama.
Jioni
 ya siku hiyo, Rais Kikwete atahudhuria dhifa ya kitaifa ambayo 
itaandaliwa kwa heshima yake na mwenyeji wake, Gavana Jenerali Sir Peter
 Cosgrove na baada ya dhifa hiyo, Rais Kikwete na ujumbe wake wataondoka
 mjini Canberra kwenda Sydney, mji mkuu wa kibiashara wa Australia.
Jumatano,
 Julai 29, 2015, Rais Kikwete atakwenda mjini Newcastle ambako 
atatunukiwa Digriii ya Uzamivu ya Heshima ya Sheria (Degree of Doctors 
of Laws Honoriscausa – honorary LLD) na Chuo Kikuu cha Newcastle. Rais 
atatunukiwa digrii hiyo ya heshima kwa kutambua uongozi wake uliotukuka 
na mchango wake katika maendeleo ya Tanzania na Afrika na jitihada zake 
za kuleta amani.
Chuo
 Kikuu cha Newcastle ni moja ya vyuo ambavyo vimekuwa vinatoa nafasi za 
masomo kwa wanafunzi wa Tanzania, chini ya sera ya miaka mingi ya 
Australia kusaidia elimu katika Tanzania. 
Wanafunzi
 26 wa Tanzania tayari wamemaliza masomo katika chuo hicho na kurejea 
nyumbani katika maeneo ya madini, elimu ya juu, vyombo vya habari, 
masuala ya fedha na masuala ya serikali. Wanafunzi 45 bado wanaendelea 
na masomo yao katika chuo hicho.
Rais Kikwete na ujumbe wake wataondoka Australia asubuhi ya Alhamisi, Julai 30, 2015 kurejea nyumbani.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni