Mkurugenzi
 wa Taasisi ya Takwimu nchini Dr Albina Chuwa akiongea na vyombo vya 
habari jijini Arusha katika mafunzo ya siku tano  kuhusu suala la 
takwimu zinazohusu hali ya mazingira, ikiwemo uharibifu unaotokana na 
uchafuzi wa maji, hewa chafu na kupotea kwa uoto wa asili ,Mafunzo hayo 
yameudhuriwa  na viongozi kutoka Nchi za Jumuiya ya Afrika 
Mashariki(Habari Picha na Pamela Mollel wa Jamiiblog)
Washiriki wa mafunzo wakiwa katika picha ya pamoja
Mkuu
 wa kitengo cha takwimu katika Umoja wa Mataifa, Reena Shah amesema 
idara yake ina mkakati maalum wa kusaidia nchi hizo katika ukusanyaji wa
 takwimu za mazingira ambazo kwa sasa ni muhimu sana katika kuweka 
ajenda na mipango ya maendeleo endelevu.
Mkurugenzi wa Takwimu Nchini Burundi Mohamed Feruz akizungumza na vyombo vya habari kuhusu takwimu katika nchi yake
Washiriki wakifwatilia mafunzo kwa ukaribu zaidi
Washiriki wa mafunzo ya Takwimu kutoka Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki
Meneja wa idara ya Takwimu Mkoani Arusha Margeret Mutaleba  akizungumza katika mafunzo hayo jijini Arusha
Prof.Innocent Ngalinda akizungumza katika mafunzo hayo
Mkurugenzi
 wa Taasisi ya Takwimu nchini Dr Albina Chuwa amesema kuwa suala la 
takwimu zinazohusu hali ya mazingira, ikiwemo uharibifu unaotokana na 
uchafuzi wa maji, hewa chafu na kupotea kwa uoto wa asili bado ni ngeni 
katika nchi zinazoendelea, hususan za bara la Afrika na kwamba kuna 
umuhimu wa kutoa mafunzo maalum kwa wafanyakazi wa idara za takwimu 
nchini.
Aliyasema hayo jana wakati akifungua mafunzo ya siku tano kwa nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki jijini Arusha uliohudhuriwa na viongozi wa Takwimu wa nchi hizo
Bi.Chuwa alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia hali ya tabia nchi na mazingira huku akisisitiza kuwa Takwimu za mazingira zinahitaji watu wawe na uwezo mkubwa yaani elimu pamoja na rasilimali fedha na vifaa huku akitoa rai kwa Jumuiya ya Afrika mashariki kuangalia tasnia hiyo kwa kupewa kipaumbele kama sekta zingine
Naye mkuu wa kitengo cha takwimu katika Umoja wa Mataifa, Reena Shah amesema idara yake ina mkakati maalum wa kusaidia nchi hizo katika ukusanyaji wa takwimu za mazingira ambazo kwa sasa ni muhimu sana katika kuweka ajenda na mipango ya maendeleo endelevu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Takwimu nchini Burundi Mohamed Feruz alisema kuwa katika nchi yake bado hawajaweza kuwa na vifaa vya kisasa vya kuweka kumbukumbu
“Hatujapata mafunzo ya namna ya kufanya hizi takwimu kwa ufasaha bado ni changamoto kwetu”alisema Feruz








Hakuna maoni:
Chapisha Maoni