Mtia
 nia ya ubunge kwa CCM Philemon Mollel akizungumza katika mkutano wa 
kujinadi mbele ya wana CCM wa kata ya Sinoni jijini Arusha ili kuomba 
ridhaa yakuteuliwa na chama chake kuwania ubunge wa jimbo la Arusha 
katika uchaguzi wa mwezi Oktoba Mwaka huu.(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
Mkurugenzi
 wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ya ubunge wa jimbo
 la Arusha kwa tiketi ya CCM akinadi sera zake mbele ya wanachama wa 
chama hicho katika kata ya Sakina jijini Arusha ili kuomba ridhaa ya 
kuteuliwa kuwamgombea wa ubunge jimbo la Arusha kupitia CCM. 
Mtia
 nia ya ubunge kupitia CCM mwanasheria Victor Njau akimwaga sera zake 
mbele ya wana CCM wa kata ya Sinoni jijini Arusha ili kuomba ridhaa 
kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa mwezi Oktoba mwaka huu.
Wanachama
 na waasisi wa CCM wa kata ya Sakina jijini Arusha wakisikiliza kwa 
umakini sera zinazotolewana watia nia ya ubunge wa jimbo la Arusha 
walipokua wakijinadi kwao ili kuomba ridhaa ya kuteuliwa na chaa chao 
kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani 
utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Kada
 wa CCM Mosses Mwizarubi anayeomba ridhaa yakuteuliwa na chama chake 
kuwania ubunge wa jimbo la Arusha akisisitiza jambo katika mkutano wa 
kujinadi uliofanyika katika kata ya Ngarenaro jijini Arusha.
Mtia
 nia ya ubunge wa jimbo la Arusha kupitia CCM Hamis Migire akijieleza 
mbele ya wanachama wa CCM wa kata ya Sokon One jijini Arusha ili kuomba 
ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea wa kiti hicho kupitia CCM.
Mmoja
 wa wanachama wa CCM wa kata ya Sakija jijini Arusha ambaye hakujulikana
 jina lake mara moja akipitia kwa umakini kipeperushi chenye maelezo 
binafsi na mikakati ya kazi za ubunge cha mtia nia ya ubunge wa chama 
hicho Mustafa Panju wakati wa mkutano wa kujinadi wa watia nia hao 
uliofanyika katika kata hiyo.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni