Maafisa
 Vijana Nchini wametakiwa kutumia elimu wanayopata katika kuwaendeleza 
vijana kiuchumi ili kuwawezesha kushiriki katika shughuli za uzalishaji 
mali. 
Hayo 
yamesemwa leo Jijini Arusha na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya 
Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James 
Kajugusi wakati wa Ufunguzi wa awamu ya kwanza ya mafunzo ya 
Ujasiriamali na ubunifu.
Bw. 
Kajugusi alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa kuwaendeleza vijana nchini
 Wizara kwa Kushirikiana na Chuo cha Uongozi cha Mashariki na Kusini mwa
 Afrika (ESAMI) wameanzisha mradi unaolenga kuwawezesha vijana 
kijasiriamali nakiubunifu kwa kupitia mafunzo wanayowapa Maafisa Vijana.
“tunawaomba
 kushiriki kikamilifu katika mafunzo haya ya ujasiriamali na ubunifu kwa
 kuwasikiliza wawezeshaji kwa makini kwa dhumuni la kutumia elimu hiyo 
kuwainua vijana nchini kiuchumi na kuwawezesha kushiriki kikamilifu 
katika ujasiriamali”. Alisema Kajugusi.
Naye 
Mkurugenzi wa Ujasiriamali na Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi cha 
Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI) Bw. Leon Malisa alisema kuwa 
dhumuni la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo Maafisa Vijana katika eneo 
la  ujasiriamali na ubunifu ili kuwawezesha kuitumia Elimu hiyo kwa 
vijana vijana nchini kwa kuwawezesha kujiajiri wenyewe.
Aidha 
Bw. Malisa ametaka vijana nchini kuunda vikundi na kubuni miradi 
itakayowaendeleza ili Wizara kwa kushirikiana na ESAMI waweze kuwasaidia
 kujiendeleza ikiwa ni njia moja wapo ya kukabiliana na tatizo la Ajira 
Nchini.
Akizungumzia
 kuhusu mafunzo hayo Afisa Vijana toka Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo Bw. Eliackim Mtawa alisema kuwa watatumia mafunzo 
haya kuwatayarisha vijana kuwa wajasiriamali wazuri na kuwasimamia 
katika utekelezaji wa Miradi hiyo ili kuwawezesha kushiriki katika 
uzalishaji mali na kukuza uchumi kupitia ujasiriamali.
Mafuzno
 hayo ya Ujasiriamali na Ubunifu yameandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara 
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Chuo cha Uongozi cha 
Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI)
Mkurugenzi
 wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi akiongea na Maafisa Vijana 
waliohudhuria Mfunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu kutumia elimu na uzoefu 
watakaoupata katika mafunzo hayo kuwainua vijana kiuchumi kwa kutoa 
elimu itakayowajenga na kuwafanya vijana kujitegemea na kuwa 
wajasiriamali, wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo leo Jijini Arusha. 
Kulia ni Mkurugenzi wa Ujasiriamali na Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi 
cha ESAMI (Eastern and Southern Africa Management Institute) Bw. Leon 
Malisa.
Baadhi
 ya Maafisa Vijana wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya 
Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James 
Kajugusi wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo hayo.
Mkurugenzi
 wa Ujasiriamali na Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi cha ESAMI (Eastern 
and Southern Africa Management Institute) Bw. Leon Malisa akiongea na 
Maafisa Vijana na kuwataka kushiriki kikamilifu katika mafunzo ya 
Ujasiriamali na Ubunifu yanayotolewa kwa ushirikiano wa Chuo hicho na 
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ili kuweza kuendeleza na 
kukuza ujasiriamali hasa kwa Vijana, wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo 
leo Jijini Arusha.
Mkurugenzi
 Msaidizi kutoka Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa 
akiwaeleza jambo Maafisa Vijana, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya 
Ujasiriamali na Ubunifu yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya 
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Chuo cha Uongozi cha ESAMI 
(Eastern and Southern Africa Management Institute)leo Jijini Arusha.
Muwezeshaji Prof Bandali Batchu akiwasilisha Mada wakati wa Mafunzo hayo leo Jijini Arusha.
Prof 
Bandali Batchu Akiwaeleza jambo Maafisa Vijana wakati wakiwasilisha mada
 katika mafunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu yaliyoandaliwa kwa 
ushirikiano wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Chuo 
cha Uongozi cha ESAMI (Eastern and Southern Africa Management Institute)
 leo Jijini Arusha.
Baadhi
 ya Maafisa Vijana  wakiwa katika mijadala wakati wa mafunzo ya 
Ujasiriamali na Ubunifu yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya 
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Chuo cha Uongozi cha ESAMI 
(Eastern and Southern Africa Management Institute)leo Jijini Arusha.









Hakuna maoni:
Chapisha Maoni