Afisa Madini Mkazi, Mkoa wa 
Kilimanjaro, Fatuma Kyando akielezea  sheria na kanuni za uchimbaji wa 
madini  nchini katika mafunzo  yaliyoshirikisha wachimbaji wa madini 
Mirerani kuanzia  tarehe 25 hadi 26 Julai, 2015. Lengo la mafunzo hayo 
lilikuwa ni kuwapa uelewa juu ya  huduma za leseni kwa njia ya mtandao.
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati 
na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe (kulia) akihakiki leseni  ya
 mmoja wa wachimbaji (katikati) Kushoto ni Afisa Madini katika Ofisi ya 
Madini, Mirerani, Denis Mrengo
Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kaskazini Alex Magayane (kulia) akifungua mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wa  semina hiyo wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinawasilishwa kwa  nyakati  tofauti.
Mjiolojia katika Ofisi ya 
Afisa Madini Mkazi -Mirerani, Amir Chande Ramadhani (kushoto) na Mtaalam
 kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe 
(kulia) wakifuatilia tovuti  ya huduma za leseni  kwa njia ya mtandao 
(online mining cadastre transactional portal) kwenye mafunzo hayo.
……………………………………………………………………
Na Greyson Mwase, Arusha
Imeelezwa kuwa  ili kuondokana na
 migongano kwenye usimamizi wa sekta ya madini Kanda  ya Kaskazini, 
Wizara ya Nishati na Madini  imeandaa mafunzo kuhusu sekta ya madini  
yatakayoshirikisha  viongozi mbalimbali katika mikoa ya Manyara, Arusha 
na Kilimanjaro yanayotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.
Akizungumza katika mahojiano 
maalum jijini Arusha jana, Afisa Madini Mkazi, Mkoa wa Kilimanjaro, 
Fatuma Kyando alisema kuwa mafunzo hayo yatashirikisha wakuu wa wilaya, 
 wakurugenzi wa halmashauri,  maafisa tawala wa wilaya, watendaji na 
wenyeviti wa vijiji na kata na wawakilishi kutoka Mamlaka ya Mapato 
Tanzania (TRA)
Alieleza kuwa katika usimamizi wa
 sekta ya madini katika kanda hiyo, kumekuwepo na mgongano wa mamlaka 
ambapo kila upande umekuwa ukiona una nguvu kuliko  mwingine kwenye 
utoaji na usimamizi wa leseni za madini.
Alisema ni vyema kila mamlaka 
ikafahamu  majukumu na mipaka yake katika usimamizi wa  shughuli za 
madini ili kuzuia migogoro  inayoweza kujitokeza.
Alisisitiza kuwa  kati ya mambo 
watakayojifunza ni pamoja na sheria na kanuni za madini, utunzaji wa 
mazingira katika shughuli za madini na  fursa za madini  yaliyopo.
Akielezea changamoto  nyingine 
katika usimamizi wa shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini katika 
kanda hiyo, Kyando alisema kumekuwepo na  migongano kwenye tozo  la kodi
 kwenye mapato yatokanayo na madini.
Alisema mapato  wanayokusanya  
wamekuwa wakiwasilisha  serikali huu  ambapo  fedha hizo  hurudishwa 
tena kwenye  halmashauri  kwa ajili ya kuimarisha  huduma za jamii 
lakini bado watu wamekuwa wakihoji kwanini  fedha hizo zisilipwe  moja 
kwa moja tu kwenye halmashauri na kutumika kwa maendeleo moja kwa moja.
Aliongeza kuwa hali hii inatokana
 na wananchi na   viongozi kutokuwa na uelewa wa sheria na kanuni za 
madini  na ndio maana ofisi  yake imeandaa mafunzo hayo.
Alisema kuwa mafunzo hayo 
yatawawezesha  mamlaka zote kuwa na lugha moja na kufanya kazi kwa 
pamoja na kuzuia migogoro inayoweza kujitokeza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni