Mtaalam
 kutoka Kituo cha Jimolojia Tanzania (TGC), Jumanne  Shimba (kulia) 
akielezea shughuli za kituo hicho kwenye banda la Wizara  ya Nishati na 
 Madini.
Mtaalam
 katika   Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Rayson Nkya (kushoto) 
akielezea sera ya madini  kwa wananchi waliotembelea  banda la Wizara  
hiyo kwenye maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika 
viwanja  vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mtaalam
 kutoka  Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), Ayoub Shija  akielezea 
shughuli za mgodi huo  katika banda la Wizara ya Nishati na Madini.
Mtaalam
 kutoka Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) Steven Lowoko akitoa  maelezo 
 juu ya  jinsi mtambo wa kufua umeme  kwa kutumia maji unavyofanya kazi 
kwa kutumia mfano wa mtambo huo kwa baadhi ya wanafunzi waliotembelea 
banda la  TANESCO.
Afisa 
Mawasiliano kutoka Mpango wa Kuongeza Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia
 ya Uziduaji Nchini (TEITI), Godwin Masabala akitoa maelezo  jinsi  
taarifa za mapato  yatokanayo na rasilimali za gesi na madini 
zinavyokusanywa.
Afisa 
Huduma kwa Wateja katika  Shirika la Umeme Nchini(TANESCO), Lucas Kusare
 (katikati) akielezea shughuli za shirika hilo kwa mmoja wa wananchi 
waliotembelea banda la Tanesco.
Afisa 
Uokoaji katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), Evarist Mwanakatwe 
(kulia) akielezea shughuli za uokoaji zinavyofanyika katika mgodi huo 
pindi majanga yanapojitokeza.
Baadhi ya wananchi wakiangalia aina mbalimbali za madini katika banda la Wakala wa Jiolojia  Tanzania (GST).
Mtalaam
 kutoka Wakala wa Jiolojia  Tanzania (GST), Kankila Wakimbili akielezea 
shughuli za wakala huo kwa wananchi waliotembelea banda  hilo.
Mtaalam
 katika   Chuo cha Madini Dodoma(MRI), Mkunde Msaky (kulia) akielezea 
fani zinazotolewa na chuo hicho kwa wananchi waliotembela banda hilo.
Wataalam  katika Wakala wa Jiolojia  Tanzania (GST) wakiwa katika picha ya pamoja.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni