Meneja Uhusiano wa Kampuni ya 
Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi, akizungumza na waandishi wa 
habari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa msimu mpya wa kandanda 
kwa wateja wa DStv jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Masoko wa
 Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Mwendeshaji wa 
Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.(Picha zote na Zainul 
Mzige wa modewjiblog).
Meneja Uendeshaji wa Multichoice 
Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo, akijibu maswali ya waandishi wa 
habari (hawapo pichani) kuhusiana na huduma za DStv. Kushoto ni Meneja 
Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi.
 Afisa Masoko wa Multichoice 
Tanzania, Furaha Samalu, akielezea huduma za kuunganishwa kwa wateja 
wapya wa DStv, ambapo ving'amuzi pamoja na dishi vinapatikana kwa 
gharama nafuu kabisa ya Sh.99,000/- kwa mawakala wote wa DStv nchini. 
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya 
Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi (wa pili kushoto) akikabidhi 
zawadi  ya begi kwa mwandishi wa habari, Joseph Michael baada ya 
kuchezesha droo kwa waandishi waliohudhuria mkutano huo. Wanaoshuhudia 
kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia 
ni Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
Furaha Samalu na Barbara Kambogi 
wakikabidhi zawadi ya begi Super Sport kwa mpiga picha wa ITV, Abdallah 
Kaniki aliyeibuka mshindi katika droo iliyochezeshwa na Multichoice 
Tanzania wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kulia Meneja 
Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya 
Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi akikabidhi zawadi ya T-shirts kwa 
mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Imani Makongoro.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Na Andrew Chale, modewjiblog
Msimu  mpya wa Soka 2015/16,  
unatarajia kuanza rasmi Jumapili ijayo kwa kushuhudia ligi mbalimbali 
Duniani zikichezwa na kurushwa  moja kwa moja kupitia SuperSport   
ambayo imejipanga kukuletea  burudani kabambe kwa mashabiki wa soka 
barani Afrika.
Meneja  uendeshaji wa Multichoice 
Tanzania , Ronald Baraka Shelukindo mapema jana akizungumza na vyombo 
vya habari amebainisha kuwa, Wateja wa DStv wakae tayari msimu huu 
kwenye Ulimwengu wa Mabingwa ambapo  timu mbalimbali zimejiimalisha 
katika kuakikisha zinatwaa ubingwa.
“Ligi ya mwaka zitakuwa za kasi na 
kuvutia kwa kila timu. Barcelona wanajiandaa kutawala dunia kwa mara 
nyingine, huku Manchester United wanahitaji kurudisha  kiti chao cha 
Ubingwa Uingereza. Jose Mourinho  analenga kuhakikisha Chelsea inabaki  
juu,  wakati huo huo , Hispania inajiandaa kuhakikisha wanashinda kwa 
mara ya tatu kombe la Euro 2016.” Ameeleza Baraka Shelukindo.
 Ameogeza kuwa, Watazamaji wa 
SuperSport  watakuwa na  nafasi ya kipekee kushuhudia mechi  kwenye 
ubora wa  HD, ikiwa ni pamoja na michuano ya  Ligi Kuu ya Uingereza 
(EPL) , Ligi ya Hispania (La Liga) , Ligi ya Mabingwa wa Ulaya(UEFA) na 
Ligi ndogo ya Ulaya ( Europa) ,mechi  za FIFA za kirafiki za kimataifa 
na Klabu Bingwa ya Dunia , Kombe la Ujerumani ,  Kombe la Mfalme  
Hispania (Copa Del Rey) , Kombe la  FA na zaidi.
Kwa upande wake, Meneja  Uhusiano wa
 Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi anaeleza kuwa, Katika msimu huu ,
 Ulimwengu wa Mabingwa itakuwa ikionyesha mechi zaidi ya 900 za 
kimataifa. Wateja wa DStv Compact Plus wataweza kufurahia baadhi ya 
mechi zaidi ya 450 ‘live’, huku Wateja wa  DStv Premium watazawadiwa  
mechi zote ‘Live’ zitakazorushwa katika chaneli zote za SuperSport .
 “Kuanzia msimu huu na kuendelea,  
vituko vyote vya Ligi Kuu ya Uingereza  vitakuwa  vikiletwa kwenu 
kupitia SuperSport 5 ( SS5 ) inayopatikana kwenye kifurushi cha Premium.
  SS5 sasa itakuwa ni nyumba ya soka la Afrika kwa ligi kuu ya Uingereza
  huku ikijumuisha  mechi  3 ‘Live’ kila Jumamosi na Jumapili.  
Kuambatana na mechi  kutakuwa na vipindi maalum vya soka  kama  PLTV 
Kick Off, Match Day Live, Fan Zone, Saturday/Sunday Review, Football 
Today, Classic Matches, Netbusters na  Mech za Wiki” Amebainisha Barbara
 Kambogi.
Moto wa  La Liga utawashwa  ndani ya
 SuperSport 3 ( SS3 ). Chaneli hii itakuwa inakuletea  mechi hadi tatu 
za ligi ya Hispania ‘ Live’ kwa siku ya Jumamosi na Jumapili .  Wateja 
wa DStv Premium na Compact Plus  watapata nafasi ya kuangalia  mechi za 
michuano ya Kombe la mashindano Uingereza ndani ya SS3 sambamba na  
mechi za Jumamosi mchana za Ligi kuu ya Uingereza ,  mbadala wa mechi 
inayorushwa ndani ya SS5,  pamoja na Ratiba zote za  Jumatatu usiku na 
vipindi vya mahojiano vya studio.
Pamoja na Mechi za ‘Live’ ndani ya  
SS3 , itakuwa inakuonyesha vipindi  muhimu  vya shoo za magazeti  , 
yanayojiri ndani ya  La Liga, pamoja na vipindi maalum  vya ligi za soka
 . Makombe yote ya mpira wa miguu, Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Europa, 
 Kombe la FA ,  Kombe la Mfalme  Hispania (Copa Del Rey),  Kombe la 
Ujerumani , Euro 2016 na mechi za kirafiki za kimataifa zitaendelea  
kutapatikana kwenye SS3 .
Kwa habari zaidi za michezo na ratiba za mechi kwenye SS5 na SS3, tafadhali tembelea www.supersport.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni