Mkurugenzi
 wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ubunge wa jimbo la
 Arusha kwa tiketi ya CCM akinadi sera zake mbele yawananchi na 
wanachama wa chama hicho katika kata ya Moivaro ofisi za kata hiyo 
jijini Arusha ili kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea wa ubunge 
jimbo la Arusha kupitia CCM,aliwataka watanzania kuiga nyendo za Baba wa
 Taifa Mwalimu Julias Nyerere kwa kuwa na upendo,ushirikiano na kukataa 
rushwa(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog) 
Mkurugenzi wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ubunge wa jimbo la Arusha kwa tiketi ya CCM akicheza wimbo wa chama cha mapinduzi ,...CCM MBELE KWA MBELEEEEEEEEE ......kushoto kwake ni Mtia nia mwenzake wakili msomi Edimond Ngemela na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Monaban yajijini Arusha,Philemon Mollel ambaye pia ni Mgombea Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM
 Mosses
 Mwizarubi ambaye pia ni mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama cha 
mapinduzi CCM akiomba ridhaa kwa wananchi pamoja na wananchama wa chama 
hicho kuwatumikia katika nafasi ya Ubunge
Mkurugenzi wa Bushback Safaris Mustafa Panju akimwaga 
sera zake mbele yawananchi na wanachama wa chama hicho katika kata 
Olorieni katika uwanja wa ccm,alisisitiza watu kujitolea kwa upendo kama
 alivyofanya Baba wa Taifa hili Mwalimu Jualias Nyerere kwa kusimamia na kuweza kukomboa Nchi na hakukuwepo na swala la rushwa
 Wakili msomi Edimond Ngemela anayeomba
 ridhaa ya ccm katika nafasi ya ubunge akisalimiana na mmoja wa wananchi
 waliojitokeza kuwasikiliza watia nia kupitia chama cha mapinduzi CCM 
katika kata ya Olorieni jijini Arusha
Mohamed
 Omary ambaye pia ni mgomea Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM 
akimwaga sera zake ambapo alisema kuwa akipata ridhaa ya kuwatumikia 
atahakikisha anawachukulia hatua kali wale wote wanaotelekeza watoto 
hali inayosababisha watoto wa mtaani kuongezeka 
Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano ambaye pia ni msimamizi wa uchaguzi akiongea katika mkutano huo
Katibu
 wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano ambaye pia ni msimamizi wa 
uchaguzi kulia akiwa na mmoja wa wagombea mapindizi Mosses Mwizarubi 
Mtia
 nia ya Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM Thomas Munisi akimwaga 
sera zake katika kata ya Moivaro akiomba ridhaa ya kwa wananchi ya 
kuwatumikia katika nafasi ya ubunge jimbo la Arusha mjini
Taswira katika kata ya Moivaro jijini Arusha

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni