Usili
 wa kwanza wa Dance 100% (2015) umefanyika kwa mafanikio makubwa Temeke 
jijini Dar es Salaam, ambapo makundi ya Team ya Shamba, The WT Group, 
WD, The Best Boys Kaka Zao na Team Makorokocho wameweza kushinda nafasi 
ya kuingia katika michuano kutoka wilaya ya Temeke.
Makundi
 haya yamechuana vikali na mengine 6 yanayokamilisha idadi ya makundi 
11, UNI 6 Crew, GMF Crew, TWC, Dar Crew, Noma Sana Crew, na Viga Stars 
yaliyojitokeza kuwania nafasi hiyo katika usajili huo wa kwanza.
Mratibu
 wa mashindano hayo kutoka East Africa Television na East Africa Radio, 
Bi Happy Shame, amesema kuwa amefurahishwa na utulivu na amani ambayo 
wapenda burudani Temeke wameonyesha leo, huku pia kukiwa na vipaji 
mbalimbali kutoka makundi yaliyojitokeza katika usaili huo wa kwanza.
Akizungumza
 baada ya kumalizika michuano ya usaili huo, mratibu wa Dance 100% 
kutoka BASATA, Kwerugira Maregesi, mbali na kufurahishwa na vipaji 
vilivyojitokeza, amekumbushia umuhimu wa makundi hususan yale 
yanayotarajiwa kushiriki usajili unaofuata, kuzingatia vigezo na 
masharti yaliyowekwa kujiwezesha kushinda, ikiwepo ubunifu katika 
mitindo ya kudansi, kuburudisha na muonekano, huku akishauri kupunguzwa 
kwa mitindo ya sarakasi na kuongezwa ladha katika upande wa dansi zaidi.
Majaji
 Super Nyamwela, Queen Darleen na Shetta wametumia umakini nkubwa 
kuhakikisha wanatoa alama zinazostahili kwa mujibu wa vigezo kwa 
washiriki wote, huku burudani mbalimbali zikijiri zikishereheshwa 
kikamilifu na watangazaji rasmi wa Dance 100 kwa mwaka huu, T-Bway 360 
na mrembo Maggie Vampire.
Majaji
 pia kila mmoja kwa nafasi yake wametaka washiriki watakaoendelea 
kujitokeza kujipanga zaidi wakizingatia vigezo vilivyowekwa, ambavyo 
ndivyo wanavyovitumia kutoa maksi (alama) zitakazowawezesha kufikia 
ushindi.
Usajili
 wa pili wa mashindano haya makubwa kabisa ya kudansi utafanyika katika 
viwanja vya Don Bosco Upanga siku ya Jumamosi Tarehe 01 Agosti 2015, 
ambapo makundi mengine matano yatasakwa kushiriki katika michuano hiyo 
kwa mwaka huu.
Usikose
 kujionea kwa urefu yote yaliyojiri  pale TCC Chang'ombe katika 
mashindano ya usajili huo, kwa kutazama ting'a namba moja kwa vijana 
EATV, siku ya Jumamosi, kuanzia saa 12 na nusu jioni.
East
 Africa Television na East Africa Radio inaleta Dance 100% kwa kupewa 
nguvu na mtandao wa Vodacom Tanzania na Coca Cola ambao ndio kinywaji 
rasmi cha dance 100% (2015).
PICHANI
 JUU: Kati ya makundi matano yaliyopita kwenye usaili wa kwanza wa Dance
 100% (2015) - Temeke. Kundi linaitwa 'The Best Boys Kaka Zao'
 Kutoka
 kushoto -Majaji wa mwaka huu kwenye Dance 100%  ni Super Nyamwela, 
Shetta na Queen Darleen wakiwa wanajumulisha matokeo ya washiriki kutoka
 Temeke.
 Shabiki
 wa kundi la 'Noma Sana' akiwa anajitayarisha kushangilia timu yake 
kwenye usaili wa kwanza Temeke kwenye Dance 100% (2015)
 Washiriki wa kundi la 'Noma Sana' mwaka huu kwenye Dance 100% wakiwa wanafanya yao viwanja vya TCC Changombe.
Watangazaji
 rasmi wa Dance 100%, TBway 360 na Maggie Vampire wakiwa wanasherehesha 
kikamilifu huku burudani mbalimbali zikijiri TCC Changombe.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni