Rais
 Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akijiandikisha katika daftari la kudumu la 
wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa kielektoniki(Biometric Voters 
Register( BVR) katika kijiji cha Msoga,kata ya Msoga wilayani Bagamoyo 
leo.Kulia akiangalia kwa makini ni mwandikishaji msaidizi Bi.Happyness 
Thomas Misana na katikati ni Afisa TEHAMA kutoka ofisi Tume ya Taifa 
Uchaguzi Bi.Mariam Rajabu.Kushoto aliyesimama akishuhudia ni Mbunge wa 
Chalinze Ridhwani Kikwete.
 Afisa
 TEHAMA kutoka ofisi ya Tume ya Uchaguzi Taifa ya Uchaguzi Bwana Sanif 
Khalfan akichukua lama za vidole vya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete 
wakati Rais alipokwenda kujiandikisha kijijini kwake Msoga wilaya ya 
Bagamoyo leo .
 Bwana
 SANIF Khalfan ambaye ni Afisa TEHAMA kutoka ofisi ya Tume ya Taifa ya 
Uchaguzi akimpiga picha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati Rais 
alipokwenda kujiandikisha kupiga kura kwa kutkumia teknolojia mpya ya 
BVR kijijini Kwake Msoga leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitambulisho chake wakati wa zoezi la kujiandikisha kijijni kwake Msoga leo.
 Mwenyekiti
 wa tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva akimkabidhi Rais 
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kitambulisho chake cha kupiga kura baada ya 
Rais Kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia 
teknolojia ya BVR huko kijijini Msoga wilayani Bagamoyo leo.
Rais
 Kikwete akimshukuru Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian
 Lubuva baada ya kukabidhiwa  kitambulisho chake cha kupiga kura baada 
ya  kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia 
teknolojia ya BVR huko kijijini Msoga wilayani Bagamoyo leo. Picha na 
Freddy Maro.

Rais akuonyesha kitambulisho chake alichopewa mara baada ya kujiandikisha katika daftari  daftari la kudumu la 
wapiga kura kwa kutumia teknolojia ya BVR huko kijijini Msoga wilayani 
Bagamoyo leo.
---
JUMLA ya watu milioni 11,248,194 wameandikishwa kwenye daftari la 
kudumu la wapiga kura zoezi ambalo linaendelea kwa sasa hapa nchini 
likiwa limeingia mkoani Pwani. 
Hayo yalisemwa leo 
kwenye Kijiji cha Msoga kata ya Msoga wilayani Bagamoyo na mwenyekiti wa
 Tume ya Uchaguzi ya Taifa Damian Lubuva alipokuwa anampa taarifa Rais 
Dk Jakaya Kikwete mara baada ya kujiandikisha. 
Bw. 
Lubuva alisema kuwa malengo ni kuandikisha watu milioni 21 hadi 23 kote 
nchini mara zoezi hilo litakapokamilika kati ya Julai mwishoni au Agosti
 mwanzoni kama hakutatokea matatizo. 
“Hadi sasa ni 
mikoa 11 inaendelea na zoezi ambayo ni Mwanza Shinyanga, Geita, Simiyu, 
Mara, Manyara, Arusha, Kilimanjaro Morogoro na jana ulianza mkoa wa 
Pwani,” alisema Lubuva. 
Aidha alisema kuwa changamoto 
zilizojitokeza ni za kawaida hasa kutokana na mfumo huu kuwa ni mpya 
kwani kila jambo jipya lina changamoto zake.  
“Mfumo 
huu ni mpya hivyo lazima kuwe na changamoto za hapa na pale lakini zoezi
 linakwenda vizuri na tunaamini kuwa tutafanikiwa kama tulivyopanga,” 
alisema Lubuva. 
Mkoa wa Pwani una jumla ya vituo 1,752
 na mashine za BVR 932 ambapo kata ya Msoga kuna jumla ya vituo 17 zoezi
 hilo kwa mkoa wa Pwani lilianza jana na litamalizika Julai 20. 






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni