Mtoa 
mada Awadh Ali Said, akitoa mada kuhusu muungano na umuhimu wa 
kuzingatia misingi ya amani katika mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi 
ya Mwalimu Nyerere ambao ulifanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius
 Nyerere Dar es Salaam leo.
 Mtoa 
mada Dk. Humphrey Polepole akitoa mada kuhusu kuzingatia misingi ya 
amani na umoja wa taifa letu kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 2015.
 Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku akitoa majumuisho
 ya jumla juu ya dhima ya mdahalo huo, ambapo aliwataka watanzania 
kuendelea kupiga vita rushwa na kusisitiza kutowachagua watoa rushwa 
katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
  Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku (kushoto), 
akiteta jambo na watoa mada katika kongamano hilo, Jaji mstaafu Joseph 
Warioba na Dk.Humphrey Polepole (katikati)
 Jaji mstaafu Joseph Warioba, akimuonesha Dk. Humphrey Polepole ujumbe mfupi aliotumiwa kwenye simu yake .
| Jaji mstaafu Joseph Warioba akisalimiana na washiriki wa mdahalo huo baada ya kumalizika. Mdahalo huo uliorushwa moja kwa moja na Kituo cha Televisheni cha ITV. | 
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye mdahalo huo.
 Jaji mstaafu Joseph Warioba (kulia), akiwaaga washiriki wa mdahalo huo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni