Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akikaribishwa na Mama Elizabeth Chatham, 
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Caniberra nchini Australia inayotoa 
huduma ya Afya ya Mama, vijana  na watoto mara baada ya kufika eneo la 
hospitali kwa madhumuni ya kujionea namna bora yautoaji huduma.  Mama 
Salma yupo nchini Australia akifuatana na mumewe Rais Jakaya Kikwete 
kwenye ziara rasmi ya kiserikali nchni humo.
Mke wa
 Rais na Mama Salma Kikwete na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa 
Hospitali ya CaniberraMama Elizabeth Chatham wakibadilishana mawazo 
wakati walipokuwa wakitembelea maeneo mbalimbali ya kutolea huduma ya 
mama, vijana na watoto.
Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akiwaangalia baadhi ya watoto wanapatiwa huduma
 ya matibabu katika hospitali ya Caniberra wakijishughulisha na michezo 
mbalimbali wakiwa na wazazi wao.
Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akimpa pole na kumtakia apone haraka binti 
Addison Stephen,6, aliyevunjika mguu na kufungwa PoP na hatimaye kulazwa
 hospitalini hapo huku akihudumiwa na baba yake Mzazi Bwana Stephen 
Miles (aliyesimama kulia) na aliyechuchumaa ni Mkurugenzi Mtendaji wa 
Hospitali hiyo Mama Elizabeth Chatham.
Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akimbeba mtoto mchanga Isabella mwenye umri wa 
siku moja aliyezaliwa na uzito wa kilo 3 na gramu 8 katika hospitali ya 
Caniberra nchini Australia huku wazazi wake Bwana Steven Fanner,34, na 
Bibi Tania Mras,32, wakishuhudia tarehe 28.7.2015.
Mke wa
 Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake,WAMA, Mama Salma Kikwete 
akimkabidhi jarida linalochapishwa na Taasisi yake kwa Mama Elizabeth 
Chatham, Mkurugenzi Matendaji wa Hospitali ya wanawake, vijana na watoto
 ya Caniberra nchini Australia mara baada ya kutembelea sehemu 
mbalimbaali za kutolea huduma hospitalini hapo yarehe 28.7.2015.
Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akibadilishana mawazo na Mke wa Gavana Jenerali
 wa Australia Mama  Cosgrove mara baada ya Rais Kikwete kukutana na 
Gavana Generali wa nchi hiyo  Mheshimiwa Peter Cosgrove kwenye Ikulu ya 
nchi hiyo tarehe 28.7.2015.
Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akitia saini kitabu cha wageni kwenye Ikulu ya 
Australia  huku Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mwenyeji wake Gavana 
Jenerali Peter Cosgrove na Mkewe wakishuhudia.
 
PICHA NA JOHN LUKUWI.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni