Ofisa 
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Zantel, Pratap Ghose (katikati), 
akimkaribisha  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda wakati 
akiwasili kwenye hafla ya kuzindua kisima cha maji safi katika Kituo cha
 Watoto Yatima cha Watoto Wetu Tanzania kilichopo Mbezi Suka Dar es 
Salaam jana.
DC Makonda akisaini katika kitabu cha wageni katika kituo hicho.
Mmoja wa vijana wa kituo hicho akiigiza igizo kuonesha changamoto zinazowakabili watoto waishio katika mazingira hatarishi.
Mkuu 
wa Kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Evans Tegete (kulia), akizungumza 
katika hafla ya kuzindua kisima hicho. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa
 Kampuni ya Simu ya Zantel, Pratap Ghose na  Mkuu wa Wilaya ya 
Kinondoni, Paul Makonda.
Naibu 
Mkurugenzi wa Kituo hicho, Theobard Bubelwa (kulia), akiteta jambo na 
Chief Commerial Officer wa Zantel, Sukwinder Bajwa wakati wa hafla hiyo.
 
Ofisa
 Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Zantel, Pratap Ghose (kushoto), 
akizungumza katika hafla hiyo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, 
Paul Makonda.
Watoto wa kituo hicho na wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Watoto wa kituo hicho wakitoa burudani.
DC Makonda akipokea risasi ya watoto wa kituo hicho.
Vijana wa kituo hicho wakitoa burudani.
DC Makonda akizungumza katika uzinduzi huo ambapo alitoa ahadi ya kuwasomesha baadhi ya wanafunzi wa kituo hicho.
Mkuu 
wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, akifungua pazia wakati akizindua 
kisima cha maji katika Kituo cha Yatima cha Watoto Wetu Tanzania 
kilichopo Mbezi Suka Dar es Salaam jana. Kisima hicho kimejengwa kwa 
ufadhili wa Kampuni ya Simu ya Zantel.
DC Makonda akifungua bomba kuashiria uzinduzi wa kisima hicho.
Hapa DC Makonda akimtwisha maji mmoja wa wanafunzi wa kituo hicho baada ya kukizindua.
DC Makonda akimkabidhi kitabu, mtoto Yusla Omari kwenye uzinduzi huo.
DC Makonda akiwa katika picha ya pamoja na timu nzima ya kituo hicho.
Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI
 ya Simu ya Zantel jana ilitoa msaada wa kisima cha maji kwa watoto 
yatima wa kituo cha Watoto Wetu Tanzania,ikiwa na lengo la kumaliza 
tatizo la maji na kuhakikisha  upatikanaji wa maji safi na salama kwa 
takribani watoto 70 wa kituo hicho.
Tatizo
 la maji ni moja ya matatizo sugu katika mkoa wa Dar es salaam pamoja na
 Tanzania kwa ujumla hivyo msaada huu ni wa muhimu kwa watoto wa kituo 
hicho.
Kisima
 hicho kilichokabidhiwa jana kitatoa maji safi na salama na yaliyotayari
 kwa matumizi ambayo yatawasaidia watoto kuepukana na maradhi 
yanayosababishwa na maambukizi ya maji yasiyo salama na machafu.
Akizungumza
 wakati wa makabidhiano hayo , Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Zantel,
 Pratap Ghose alisema kampuni ya Zantel imekuwa siyo tu ikitoa huduma 
bora na zenye unafuu kwa wateja wake bali pia imekuwa ikifanya jitihada 
za kusaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwenye jamii inayoizunguka
‘Kampuni
 yetu inalenga kugusa maisha ya wananchi wanaotuzunguka, na ndio maana 
tumeamua kutoa msaada huu wa kisima ili kiweze kukisaidia kituo hiki 
kumaliza moja ya matatizo yaliyokuwa yanawakabili kwa muda mrefu’ 
alisema Pratap.
Mkuu
 wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika
 shughuli ya makabidhiano hayo, aliipongeza kampuni ya Zantel kwa msaada
 huo akisema ni ishara inayofaa kupongezwa.
‘Ustawi
 wa watoto na vijana ni jambo muhimu katika jamii, hivyo nakipongeza 
kituo hiki kwa kazi kubwa wanayofanya, na pia kampuni ya Zantel kwa 
kulikumbuka kundi hili muhimu katika jamii, na ninatoa wito kwa 
makampuni mengine kushiriki na kusaidia kituo hiki’ alisema Makonda.
Kituo cha Watoto Wetu Tanzania kilichopo Mbezi Suka jijini Dar es Salaam kilianzishwa mwaka 2001, kwa lengo la kuhakikisha watoto wasio na wazazi au walezi wanapata matunzo na elimu bora.
Akitoa
 neno la shukurani Mkuu wa Kituo cha Watoto Wetu Tanzania,Evance Tegete 
alisema awali kituo kilikuwa na tatizo kubwa la maji, lakini sasa 
shukrani kwa Zantel tatizo hilo limemalizika.
‘Awali
 tulikuwa tunategemea maji kutoka DAWASCO ambayo upatikanaji wake si wa 
uhakika,tunawashukuru Zantel wameweza kutusaidia kutatua tatizo hili’ 
alisema Tegete. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni