Na Ahmed Mahmoud Watanzania wametakiwa kuzalisha bidhaa za Kilimo zinazoendana
na masoko ya kimataifa ili kuweza kujingezea kipato na kukamata masoko hayo ya
kimataifa Aidha Waziri wa Kilimo Husein Bashe anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi
katika maonesho ya kimataifa ya kilimo TanzFood Expro 2022 yenye kibwagiz mbiu
Ladha ya Tanzania. Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya EAC
Jijini Arusha Mkurugenzi wa sekta ya uzalishaji ndani ya Jumuiya ya Afrika
masharika Jean Baptiste amesema maonyesho hayo yatafanyika kwa siku tatu kuanzia
tarehe 11 hadi 13. Amesema kwa siku tatu watatumia kujenga mtandao wa kibiashara
katika mazingira ya kitaalamu na kwamba sekta hii ya kilimo sio kwa ajili ya
Tanzania Pekee ndio maana kama Eac na KiliFair Promotion tumeungana ili nchi
wanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki tutoke na bidhaa zilizo bora. "Bidhaa
bora zinahitajika sana ili kuweza kutangaza katika maonyesho haya kutoka kote
katika jumuiya itasaidia kuongeza tija ya kuzalisha bidhaa zenye ubora wa
kimataifa". Awali Mkrugenzi wa Kilifair Dominic Shoo Alisema kuwa maonesho ya
kilimo TanzFood pia yatazinduliwa na Balozi wa Ujerumani nchini Regine Hess na
Waziri wa Kilimo Husein Bashe na kuyaleta pamoja makampuni 120 ya hapa nchini na
nchi za Eac. Alisema kuwa wanayofuraha kuona waonyeshaji wa ndani na nje ya nchi
kutoka masoko mengine kuja kuangalia bidhaa zetu huku akiyataka makampuni ya
mbegu na Mashine za kilimo kuleta bidhaa zao katika maonyesho. Kwa Upande wake
Mkurugenzi Mwenza wa Kilifair Tom Kunkler alisema kuwa maonesho hayo washiriki
watapata fursa ya kupata mafunzo ya kilimo na uzalishaji wa bidhaa ili waweze
kushindana katika soko la kimataifa. Alisema kuwa mafunzo hayo kwa wakulima
yatawasaidia kuongeza ubora na maendeleo katika sekta ya kilimo ambapo kauli
mbiu yake ni Ladha ya Tanzania.
Na Ahmed Mamoud
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Makamishna Wasaidizi wa Ardhi wa mikoa nchini kuwajibika na kutumia wajibu wao katika kutekeleza mikakati ya Wizara kufikia malengo.
Aidha, amewataka Makamishna hao kuwapangia majukumu kwa malengo maafisa walio chini yao na kufuatilia kazi wanazowapa mara kwa mara.
Dkt Mabula amesema, hayo tarehe 25 Februari 2022 wakati akifungua kikao kazi cha Menejiment na Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha.
‘’Yapo malamiko ya lugha zisizofaa kwa wateja, hii haikubaliki fuatilieni hili na kulikemea vikali na kuzingatia misingi na kanuni za utumishi wa umma katika majukumu yenu ya kila siku ’’ alisema Dkt Mabula.
Aidha, aliwataka katika utekelezaji mpango mkakati wa wizara wanazingatia vipaumbele vya serikali hususan maelekezo ya mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi.
Akigeukia suala la makusanyo ya kodi ya pango la ardhi, Waziri wa Ardhi aliwataka Makamishna wa ardhi Wasaidizi wa mikoa kuwa wabunifu katika njia za kukusanya mapato.
‘’Sula la mtandao kutopataikana muda mwingi linaonekana kuwa kikwazo katika ukusanyaji maduhuli, lifanyieni kazi’’ alisema Dkt Mabula.
Waziri Dkt Mabula pia alihimiza kuongezwa kwa kasi ya umilikishaji ardhi na kuwataka Makamishna hao na wakuu wa idara katika wizara kuweka malengo kwa kila ofisa mwenye taaluma ya ardhi kuandaa hati.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi alisema baada ya kuteuliwa alifanya ziara katika baadhi ya mikoa na kukutana na baadhi ya changamoto alizozitaja kuwa ni pamoja na kutofikiwa malengo ya ukusanyaji kodi ya ardhi pamoja na baadhi ya halmashauri kutohudumia idara za ardhi kwa madai ya idara hizo kuhamishiwa wizarani.
‘’Nimeanza kuchukua hatua ili kutatua changamoto hizo ambapo tayari nimetoa maagizo mbalimbali kwenye mikoa na menejimenti ya wizara na ni matarajio kikao kazi kutaibua suluhisho la changamoto hizo’’ alisema Dkt Allan Kijazi.
Kwa mujibu wa Dkt Kijazi, Wizara ya Ardhi imekuwa ikinyooshewa vidole na wananchi kwa masuala ya ukiukwaji wa haki za wananchi na kuchafua taswira ya Wizara na kutaka watendaji wa sekta ya ardhi kujitafakari na kujisahihisha kwa kutimiza wajibu ili kuondoa dhana hiyo.
Aligusia pia mpango wa urasimishaji makazi holela na kueleza kuwa, ni matarajio yake kupitia kikoa hicho washirikia wataibuka na mkakati wa uelekeo wa wizara katika kupanga miji sambamba na usimamamia fedha zilizotolewa kwa ajili ya mpango wa kupanga, kupima na kumilikisha ardhi maarufu kama KKK.
Mashindano ya Sed Miss Valentine's 2022 yatafanyika kesho februari 14 mwaka 2022
Mjini Babati Mkoani Manyara huku warembo 15 wanatarajiwa kuchuana vikali kutwaa
taji hilo. Afisa Masoko wa Kiwanda cha Mati Super Brand Gwandumi Mpoma ambao
ndio wadhamini wakuu wa mashindano hayo wamesema kuwa wamejipanga kuhakikisha
wakazi wa Babati wanafurahia mashindano hiyo amewataka wajitokeze kwa wingi.
Gwandumi amesema kuwa Mashindano hayo yanalenga kuibua vipaji vya vijana na
kuwapa fursa ya kufanya kazi na kiwanda hicho kupitia bidhaa mbali mbali
wanazozalisha ikiwemo Strong Gin,Sed Pinepale na Tanzanite Premium Vodka. Hamisi
Saidi ni Moja kati ya waandaaji wa Mashindano ya Sed Miss Valentine amesema kuwa
warembo wamejiandaa vizuri katika kambi hiyo na wanatarajia ushindani utakua
mkali kutokana na maandalizi waliyoyafanya. wa Upande wao washiriki wa
Mashindano hayo Jenifer Paulo Mmari na Keithwin Pallangyo wamepongeza udhamini
wa kampuni ya Mati Super Brands Limited kwa kuwawezesha kukaa kambini na
kujiandaa vyema hivyo wamewataka wakazi Mkoa wa Manyara na Mikoa jirani
kujitokeza kwa wingi.
Na Ahmed Mahmoud Arusha
SERIKALI imeridhishwa na utekekezaji wa miradi miwili ya maendeleo ya
ujenzi wa Jengo la ghorofa kumi la nyumba za kuishii watumushi wa
serikali lililopo mkabala na jengo la Uhamiaji mkoa pamoja na
uboreshaji wa uwanja wa ndege wa Arusha..
Naibu waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara, ameyasema hayo
ilipohitimisha ziara yake ya siku moja ya kutembelea miradi
hiyo,iliyotanguliwa na Waziri huyo kufanya kikao na watumishi wa
serikali kwenye ukumbi wa benki kuu.
Kwenye mradi wa ujenzi wa Jengo la ghorofa kumi linalomilikiwa na
linalijengwa na wakala wa majengo nchini TBA,Waitara,ameipongeza
wakala huyo na kuagiza kuwa kipaumbele cha watu watakao ishi ndani ya
jengo hilo iwe ni watumishi wa serikali.
Alisema kukamilika kwa ujenzi wa Jengo hilo kutaongeza mapato ya
serikali na uhitaji wa majengo ya kuishi watumushi ni mkubwa mno hivyo
Jengo hilo litaiwezesha TBA,kujiendesha kibiashara .
Alisema wizara imeshaagiza wastaafu ikiwemo wabunge waliomaliza muda
wao kuondoka kwenye nyumbaza serikali zilizopo Dodoma ili kuwezesha
watumishi wengine kupata nyumba za kuishi.
Akiwa kwenye uwanja wa ndege wa Arusha,Waziri Waitara,ameridhishwa na
hatua za uboreshaji wa uwanja huo uliofanywa na mamlaka ya viwanja vya
ndege nchini,na kusema kuwa serikali Imetoa fedha nyingi kwa ajilj ya
miradi hiyo.
Alisema kukamilika kwa ukarabati huo unahusisha kuongeza Urefu wa
uwanja eneo la kurukia ndege kutaongeza ndege nyingi kutua uwanjani
hapo na mapato nayo yataongezeka.kwani uwanja huo ni rafiki kwa
watalii na wananchi wa mkoa wa Arusha
Alisema jumla ya viwanja kumi na moja nchini vitafanyiwa marekebisho
na uboreshaji katika bajeti ya mwaka huu na serikali sasa inafungua
njia za uchumi kwa kuimarisha miundo mbinu ya barabara,reli,ndege na
Mali kwa wizara hiyo ni wezeshi kufikia malengo ya kiuchumi.
Kwa upande wake meneja wa uwanja wa ndege wa Arusha,Mhandisi Eliud
Tesha,alisema mradi wa ukarabati na maboresho ya uwanja huo
yanahusisha eneo la maegesho ya ndege na kuruka ,maegesho ya
magari,eneo la kurukia ndege na miradi hiyo iliyotekelezwa ambayo
imekamilika mwaka jana.
Ameongeza kwamba mamlaka ya viwanja vya ndege nchini ina mpango wa
kujenga jengo lingine la kisasa uwanjani hapo.la kufikia wageni kwa
lengo la kuendelea kuongeza wigo mpana kwa abiria wanaofika kusafiri
ndani ya uwanja huo.
DC DAQARRO ATAKA WADAU WA ELIMU KUHAKIKISHA MPANGO WA LANES UNAENEA ARUSHA NA KULETA MATOKEO CHANYA
posted on
Afisa elimu Vielelezo Godfrey Augustino akitoa hotuba kwenye ufunguzi wa wiki ya usomaji Lanes kabla ya kumkaribusha mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro picha na mahmoud ahmad arusha |
Meza kuu wakiwa wanajadiliana mkuu wa wilaya na mkutubi mkuu wa maktaba bi Rafiki Mvamba ambapo afisa elimu akiendelea kutoa hotuba yake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi |
MAONYESHO YA VITABU MBALI MBALI NAYO YALIKUWEPO KWENYE WIKI YA USOMAJI KATIKA JIJI LA ARUSHA ILIYOADHIMISHWA KWENYE MAKTABA KUU YA MKOA WA ARUSHA |
Mwanafunzi wa shule ya Msingi Uhuru Jaquline Abrogast akisoma kitabu mbele ya mkuu wa wilaya kwenye maadhimisho ya siku ya Usomaji iliyoadhimishwa kimkoa kwenye maktaba ya mkoa jijini Arusha |
Picha juu ni igizo la wanafunzi wa shule ya msingi Naura wakionyesha masuala mbali mbali ya safari ya kusoma kwenye maonyesho ya wiki ya usomaji mbele ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Arusha |
Wanafunzi wa shule ya msingi Arusha School wakiimba wimbo mbele ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Arusha |
Mkutubi mkuu wa maktaba ya mkoa akiwa na majaji wenzake wakifuatilia mashindano ya kusoma kwa wanafunzi wa shule sita za Naura,Sombetini,Meru,Mwangaza,Uhuru na Arusha School |
TCCIA LONGIDO SACCOS WAITAKA SERIKALI KUSIMAMIA SUALA LA ELIMU KWA VYAMA VYA USHIRIKA NCHINI
posted on
Juu na chini ni sehemu ya wanachama wa saccos ya TCCIA wilayani Longido wakiwa katika mkutano wao wa mwaka wakifuatilia vipengele vya Agenda za mkutano huo picha na mahmoud ahamad longido |
Vijana nao walikuwemo kama sehemu ya mkakati wa serikali kuweza kutengeneza uchumi wa kati wa viwanda vijana ndio nguvu kazi ya taifa lolote kufikia malengo kaama walivyokutwa na kamera ya matukio |
Wanachama wakisoma taarifa za kikao hicho hatua kwa hatua katika mkutano huo |
Mwenyekiti wa mkutano huo David Wiliam na makamu wake Adela Magani wakisikiliza taarifa ya mapato na matumizi ikisomwa |
Wanachama hawakuwa nyuma kufuatilia hatua kwa hatua taarifa ya mapato ya chama chao |
Wananchama juu na chini wakifuatilia kikao hicho ambapo waliibua mambo mengi ya kuweza kusaidia kukuza chama chao |
Mwili mmoja wa mtoto umepatikana saa nne asubuhi hii, wakati wazamiaji wakiweka sehemu ya chini Maputo (boya) yanayojazwa upepo ili kukiinua kivuko cha MV Nyerere, eneo la Bwisya kisiwani Ukara, jijini Mwanza.
Kazi ya kukinyanyua kivuko hicho kilichozama Alhamisi iliyopita na kusababisha vifo vya watu 225 ilianza jana Jumamosi Septemba 23.
Kazi hiyo inafanywa na kampuni ya Songoro Marine chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika Kijiji cha Bwisya Kisiwa cha Ukara kilipozama kivuko hicho, mtaalamu kutoka kampuni hiyo, Meja Songoro alisema hatua ya kwanza itakuwa kuingiza hewa ndani ya kivuko ili kuyatawanya maji na kuanza kukivuta.
“Kivuko kinaendelea kuelea kwa sababu kuna hewa ndani yake. Wakati kinageuka (kupinduka) kilichota maji, tutaanza kuingiza hewa kutoa maji na kuanza kukivuta. Tutakapoanza kuyatawanya maji hayo, pia tutapeleka boya na hii itafanya chombo kizidi kuja juu. Baada ya hapo tutakisogeza taratibu hadi kwenye maji mafupi.”
Usisahau Kuinstall Andoid Applicatuion yetu ili kupata habari zetu kwa haraka zaidi. Ingia Playstore, search Manyara leo blog
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)