Na Mahmoud Ahmad-Arusha
Mahakama za Tanzania bado 
zinakabiliwa na changamoto ya kuzikabili kesi za kimataifa ikiwemo kesi 
za uhalifu wa kimtandao,biashara ya binadamu kwani imeonekana zimekuwa 
zikiisha bila ya kuwatia hatiani wakosaji wa makosa hayo na kuangalia 
kama vyombo husika na mashtaka vinauwezo kiasi gani katika kuzikabili 
kesi hizo.
Kauli hiyo imetolewa kwenye 
Kongamano lililowakutanisha majaji kutoka sehemu mbali mbali za bara 
hili na nje na kaimu jaji mkuu wa Tanzania Ibrahim Juma wakati 
alipotakiwa kuelezea suala la makosa mbali mbali ya kimataifa na 
kuandaliwa na Taasisi ya Wayamo na kufanyika jijini hapa.
Jaji Juma alisema kuwa wamekutana
 kuangalia ni namna gani wanaweza kuyakabili makosa ya namna hiyo na 
kupeana njia ya kuweza kuyashughulikia kikamilifu na kutoa haki yenye 
tija kwa makosa hayo pindi yanapofika mahakamani ambapo miongoni mwa 
makosa hayo yanayofika kwenye mahakama ni ujangili wa kimataifa,wizi wa 
njia ya mtandao,na kesi za chaguzi.
“Tumefika mahali sasa kuangalia 
makosa hayo na njia ya kuyatatua ilikuweza kuipeleka mahakama kuweza 
kuyashughulikia makosa kwa weledi na kutoa haki inayostahili kwa makosa 
hayo”alisema kaimu jaji mkuu.
Nae Jaji mkuu wa Zanzibar Othman 
Makungu alisema kuwa Ongezeko la makosa ya Chaguzi limeonekana kukuwa 
kwa kasi kwenye mataifa yetu kila pembe hivyo kongamano hilo litakuja na
 jibu la kuweza kuyatatua kwa ukaribu na kuweza kuyashughulikia kwa 
uweledi.
Ametolea mfano wa makosa ya 
ujangili ambapo mshtakiwa analetwa mahakamani halafu anaachiwa huru au 
kesi inachelewa kuamlizika kwa wakati hapa je ni 
umaskini,kutokujali,rushwa, au uzoefu mdogo ndio maana tunakutana 
kuyajadili ilituweze kuyapatia majibu masuala hayo.
Jaji Makungu amesema kuwa njia 
pekee ya kuweza kufikia malengo ya makosa hayo ya kimataifa ikiwemo 
biashara ya binadamu,Makosa ya uhalifu wa mtandao,inasababisha watu 
kuweza kuendelea kuteseka hapa njia ni kuanza kuyazuia yasitokee.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni