MAHAKAMA YAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA KESI ZA MAKOSA YA KIMATAIFA


juma
Na Mahmoud Ahmad-Arusha
Mahakama za Tanzania bado zinakabiliwa na changamoto ya kuzikabili kesi za kimataifa ikiwemo kesi za uhalifu wa kimtandao,biashara ya binadamu kwani imeonekana zimekuwa zikiisha bila ya kuwatia hatiani wakosaji wa makosa hayo na kuangalia kama vyombo husika na mashtaka vinauwezo kiasi gani katika kuzikabili kesi hizo.
Kauli hiyo imetolewa kwenye Kongamano lililowakutanisha majaji kutoka sehemu mbali mbali za bara hili na nje na kaimu jaji mkuu wa Tanzania Ibrahim Juma wakati alipotakiwa kuelezea suala la makosa mbali mbali ya kimataifa na kuandaliwa na Taasisi ya Wayamo na kufanyika jijini hapa.
Jaji Juma alisema kuwa wamekutana kuangalia ni namna gani wanaweza kuyakabili makosa ya namna hiyo na kupeana njia ya kuweza kuyashughulikia kikamilifu na kutoa haki yenye tija kwa makosa hayo pindi yanapofika mahakamani ambapo miongoni mwa makosa hayo yanayofika kwenye mahakama ni ujangili wa kimataifa,wizi wa njia ya mtandao,na kesi za chaguzi.
“Tumefika mahali sasa kuangalia makosa hayo na njia ya kuyatatua ilikuweza kuipeleka mahakama kuweza kuyashughulikia makosa kwa weledi na kutoa haki inayostahili kwa makosa hayo”alisema kaimu jaji mkuu.
Nae Jaji mkuu wa Zanzibar Othman Makungu alisema kuwa Ongezeko la makosa ya Chaguzi limeonekana kukuwa kwa kasi kwenye mataifa yetu kila pembe hivyo kongamano hilo litakuja na jibu la kuweza kuyatatua kwa ukaribu na kuweza kuyashughulikia kwa uweledi.
Ametolea mfano wa makosa ya ujangili ambapo mshtakiwa analetwa mahakamani halafu anaachiwa huru au kesi inachelewa kuamlizika kwa wakati hapa je ni umaskini,kutokujali,rushwa, au uzoefu mdogo ndio maana tunakutana kuyajadili ilituweze kuyapatia majibu masuala hayo.
Jaji Makungu amesema kuwa njia pekee ya kuweza kufikia malengo ya makosa hayo ya kimataifa ikiwemo biashara ya binadamu,Makosa ya uhalifu wa mtandao,inasababisha watu kuweza kuendelea kuteseka hapa njia ni kuanza kuyazuia yasitokee.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni