Kituo Kikuu cha Mabasi, Dodoma
  | 
| Bw.
 Justin Kisoka, Mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa 
Afrika Mashariki ambaye amebobea katika masuala ya uchumi akitoa somo 
namna vijana wa Kitanzania watakavyoweza kuuza bidhaa zao ndani ya soko 
la Afrika Mashariki lenye nchi sita na idadi ya watu wanaofikia milioni 
165.  | 
  | 
| Mfanyabiashara
 akielezwa namna bidhaa zake ambazo amezibeba kichwani atakavyoweza 
kuziuza katika nchi za Afrika Mashariki na kupata faida kubwa. | 
  | 
| Ujumbe
 wa kutaka vijana na Watanzania kwa ujumla wazinduke ili wanufaike na 
soko la Afrika Mashariki ulifikishwa kwa njia tofauti ikiwemo sanaa ya 
maigizo. | 
  | 
| Baadhi
 ya watu waliojitokeza kupata mbinu za kufanya biashara ndani ya Jumuiya
 ya Afrika Mashariki. Hapa ilikuwa Kituo Kikuu cha Mabasi mjini Dodoma. | 
Gandhi Hall , Mwanza 
  | 
| Bw.
 Justin Kisoka akiwa kwenye bustani ya Gandhi Hall mjini Mwanza akitoa 
somo namna Wanamwanza watakavyoweza kuuza Sato, Sangara na bidhaa 
nyingine katika soko la Afrika Mashariki. | 
  | 
| Wanamwanza
 acheni woga, vukeni mipaka ya Tanzania kuuza bidhaa zenu, ni baadhi ya 
maneno aliyokuwa anayatumia Mchumi huyo katika kuwashajihisha vijana 
wachangamke kuvuka mipaka ya Tanzania kuuza bidhaa zao. | 
  | 
| Dada somo limemkolea anapata maelezo zaidi kutoka kwa wataalamu wa Wizara ili shughuli ya kuvuka mipaka ianze mara moja. | 
Viwanja vya Furahisha, Mwanza
  | 
| Bw.
 Abel Maganya, Mtaalamu wa Masuala ya Afrika Mashariki kutoka Wizara ya 
Mambo ya Nje akitoa somo kwenye viwanja vya  furahisha.  | 
  | 
| Serikali
 za Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zinatimiza majukumu 
yake kwa kuweka mazingira mazuri ikiwemo sheria, kanuni na miundombimu 
ili wanajumuiya mfanye biashara katika nchi unayopenda bila bugdha. 
Msijifungie ndani vukeni mipaka kupeleka bidhaa mbalimbali. | 
  | 
| Baadhi ya Wananchi waliojitokeza katika viwanja vya furahisha. | 
  | 
| Mzee
 anasema somo limengia barabara hivyo na  uzee wangu nawahimiza wajukuu 
zangu kufanya biashara ya kuvuka mipaka. Anafikisha ujumbe wake kwa 
kushiriki kusakata dance linalohimiza biashara za kuvuka boda. | 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni