Waziri
 wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Philip Mpango akisoma hotuba kwa niaba ya
 Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) wakati 
akifungua mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na 
uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi 
Kida akitoa neno la ukaribisho kwa washiriki wa mkutano wa 6 wa mwaka wa
 ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam. 
 Mwenyekiti
 wa bodi ya ESRF, Philemon Luhanjo akizungumza machache kabla ya 
kumkaribisha mgeni rasmi kufungua mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF 
unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi
 wa Ubalozi wa China nchini Tanzania anayeshughulikia wa Masuala ya 
Uchumi na Biashara, Lin Zhiyong akizungumza kwa niaba ya balozi wa China
 wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia 
biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar 
es Salaam.
 Katibu
 Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Adolf Mkenda 
akiwasilisha mada inayohusu namna watanzania wanavyoweza kunufaika na 
fursa za kibiashara na uwekezaji China wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka 
wa ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Pichani
 juu na chini ni sehemu ya washiriki kutoka China na Tanzania 
waliohudhuria mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na 
uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti ya Taasisi ya Utafiti wa Maendeleo China (CIDRN), Prof. Dr. 
Li Xiaoyun akitoa neno la ukaribisho kwa washiriki wa mkutano wa 6 wa 
mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na 
China uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Balozi
 wa Tanzania nchini China, Mh. Mbelwa Kairuki akizungumzia namna ambavyo
 watanzania wanaweza wakafaidika na fursa za biashara na uwekezaji 
nchini China wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia 
biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar 
es Salaam.
 Mkuu
 wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akiwasilisha mada inayohusu mahusiano 
ya kibiashara ya uwekezaji kati ya Tanzania na China kwa mtazamo wa 
Serikali za Mitaa wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia 
biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar 
es Salaam.
 Kutoka
 kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii
 (ESRF), Dk. Tausi Kida, Balozi wa Tanzania nchini China, Mh. Mbelwa 
Kairuki, Waziri Mkuu mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim, Mwenyekiti wa bodi
 ya ESRF, Philemon Luhanjo, Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni
 za Infotech Investment, Ali Mfuruki wakifuatilia mada mbalimbali 
zilizokuwa zikiwasilisha wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF 
unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkutano ukiendelea.
 Balozi
 wa Tanzania nchini China, Mh. Mbelwa Kairuki pamoja na Waziri Mkuu 
mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim wakifuatilia mada mbalimbali zilizokua 
zikiwasilishwa katika mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia 
biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar 
es Salaam.
 Profesa
 Humphrey Moshi kutoka idara ya Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es 
Salaam akiwasilisha mada inayohusu uhusiano wa China na Tanzania katika 
masuala ya uwekezaji na biashara wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF
 unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Mamlaka Maalum ya Uwekezaji (EPZA), Kanali Mstaafu Joseph 
Simbakalia akichangia maoni wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF 
unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mwanachama
 wa Chama cha Wanafunzi walisomea China (CAAT), Linas Kahisha akielezea 
uzoefu wake katika fursa za kibiashara nchini humo katika mkutano wa 6 
wa mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na
 China uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Pichani
 juu na chini ni washiriki kutoka Tanzania na Chini waliohudhuria 
mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati 
ya Tanzania na China uliofanyika jijini Dar es Salaam

 Mgeni
 rasmi Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Philip Mpango, Mkurugenzi 
Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida
 na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka wakiwa katika picha ya pamoja 
na wanafunzi watafiiti kutoka nchini China.
 Mkuu
 wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa ESRF, Prof. Fortunata Makene 
(kushoto) katika picha ya kumbukumbu na Mkuu wa Idara ya Maarifa na 
Ubunifu wa ESRF, Bi. Margareth Nzuki (kulia) mara baada ya ufunguzi 
rasmi wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na 
uwekezaji
  
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi 
Kida (katikati), Mkuu wa Idara ya Maarifa na Ubunifu wa ESRF, Bi. 
Margareth Nzuki na Mwenyekiti ya Taasisi ya Utafiti wa Maendeleo China 
(CIDRN), Prof. Dr. Li Xiaoyun katika picha ya kumbukumbu.
 Mkuu
 wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (katikati) katika picha ya pamoja na 
washiriki kutoka TPSF na ESRF na Mshereshaji wa mkutano huo Eng. George 
Mulamula (kushoto).
 Baadhi
 ya washiriki kutoka China wakichukua baadhi ya makabrasha yenye taarifa
 mbalimbali zilizoandaliwa na ESRF wakati wa mkutano wa 6 wa mwaka wa 
ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Waziri
 wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Mkurugenzi 
Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida
 alipowasili katika ufunguzi wa mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF 
unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China 
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mgeni
 rasmi Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Philip Mpango (katikati) 
akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na 
Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida (kushoto) na Mwenyekiti wa bodi ya ESRF, 
Philemon Luhanjo baada ya kuwasili katika mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF 
unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China.
  
Mgeni
 rasmi Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Philip Mpango katika picha 
ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na 
Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida mara baada ya kufungua mkutano wa 6 wa 
mwaka wa ESRF unaozungumzia biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na 
China uliofanyika jijini Dar es Salaam. 
WAZIRI
 wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Philip Mpango ametaka kuwapo na uratibu 
wenye maslahi mapana katika biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na 
China.  
 
Alisema
 hayo wakati akifungua mkutano wa 6 wa mwaka wa ESRF unaozungumzia 
biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China. Alisema mahusiano 
yaliyopo kati ya Tanzania na China ambayo ni ya kihistoria yasitumike 
vibaya bali yanahitaji kuratibiwa kiuangalifu kwa maslahi ya pande zote 
mbili.  
 
Aliwataka
 washiriki wa mkutano huo wa mwaka kujadili kwa makini namna ya kuratibu
 vizuri vitega uchumi na biashara kwa manufaa ya nchi zote mbili.  
 
Alielezea kufurahishwa kuwapo na mada mbalimbali zinaozungumzia biashara
 na uwekezaji kati ya Tanzania na China na kusema mada hizo zitumike 
vyema kuweka misingi mizuri yenye manufaa kwa pande zote mbili. 
Aidha
 aliipongeza ESRF kwa kuona haja ya kuwapo kwa mazungumzo ya aina hiyo 
na kusema kupitia tafiti mbalimbali taifa hili litaenda mbele katika 
kujenga uchumi wa viwanda.  
 
Mkutano
 huo unaohusisha washiriki mbalimbali wa ngazi za juu wa biashara na 
uwekezaji kati ya Tanzania na China umeitwa kama sehemu ya mchango wa 
ESRF katika ujenzi wa uchumi wa viwanda wa Tanzania. “Sisi serikalini 
tunaridhishwa na juhudi zinazofanywa na taasisi za kitafiti kama hii 
zenye lengo la kusaidia juhudi za serikali za kuhudumia watu wake na 
kuongeza ustawi” alisema Mpango. 
 
Mkutano
 huo ambao unazungumzia mahusiano ya kibiashara na uwekezaji umeelezwa 
na Mh. Dk Mpango kuwa moja ya mikutano inayotoa fursa za kuangalia 
uwekezaji wenye tija unaozingatia maslahi mapana ya mataifa husika.  
 
Alisema
 Tanzania na China zina uhusiano mzuri wa kihistoria na hadi sasa na 
kwamba kinachostahili ni kuoanisha uhusiano huo na kuuweka katika hali 
bora zaidi za kunufaisha pande zote mbili.  
 
Baadhi
 ya miradi mikubwa ambayo Tanzania imesaidiwa na China ni pamoja na 
ujenzi wa Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) na kiwanda cha Urafiki; 
kuanzishwa kwa shamba la mpunga la Mbarali; kiwanda cha sukari cha 
Mahonda na mgodi wa mawe wa Kiwira.  
 
Kwa
 sasa China ni moja ya taifa lililo na uwekezaji mkubwa nchini Tanzania 
pia ikifanya shughuli nyingi za ujenzi zenye gharama kubwa kama daraja 
la Kigamboni na barabara.  
 
Naye
 Mwenyekiti wa bodi ya ESRF, Philemon Luhanjo, akimkaribisha Mheshimiwa 
Waziri Mpango alisema kwamba alisema kwamba mkutano huo umeandaliwa kwa 
pamoja kati ya ESRF na Chuo kikuu cha Kilimo cha China. 
Alisema
 mkutano huo umewaleta pamoja wanazuoni wa Kichina na Kitanzania 
kuangalia mahusiano yaliyopo na kutengeneza mustakabli bora wa namna ya 
kushirikiana.  
 
Naye
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF),
 Dk. Tausi Kida amesema kwamba mkutano huo ni sehemu ya juhudi za 
kusaidia serikali kwa njia ya utafiti ambapo majibu yanatumiwa 
kutengeneza sera au majibu ya changamoto mbalimbali. Mkutano huo 
ulifungwa na Waziri Mkuu mstaafu, Mh. Dkt. Salim Ahmed Salim. 
 
 
 
 
  
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni