Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Biashara. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Biashara. Onyesha machapisho yote

ZANTEL YAJA NA NGUVU KUBWA BAADA YA UBORESHAJI MTANDAO WAKE


Mtendaji Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa, akiongea wakati wa uzinduzi huo
Mtendaji Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa,akiongea na vyombo vya habari wakati wa hafla ya uzinduzi huo
8.Baadhi ya wafanyakazi wa Zantel wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo

*Yazindua kampeni ya “Tunaliamsha Kivingine”.

Kutokana na kuimarisha miundombinu ya mtandao wake wa data kwa teknolojia za kisasa zaidi,Zantel inawahakikishia wateja wake kuwa hivi sasa imekuja na nguvu mpya itakayowezesha kupata huduma bora,na huduma za interneti yenye kasi kubwa, gharama nafuu na leo inazindua kampeni mpya kwa wateja inayojulikana kama “Tunaliamsha Kivingine”.

Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita,Wataalamu wahandisi wa mtandao wa kampuni ya Zantel wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana, wa kuboresha miundombinu ya mawasiliano ya data,kuhakikisha wateja wanafurahia huduma hiyo kwa kiwango cha juu. Katika kufanikisha kazi hiyo kampuni imewekeza kiasi cha Dola za Kimarekani zipatazo milioni 4.3.

Katika kusherekea ufanikishaji uwepo mtandao bora,Zantel imewaletea watumiaji wa huduma zake waliopo, Zanzibar, Pemba, Unguja na Tanzania Bara kifurushi maalumu cha data cha kuwawezesha kufurahia mashindano ya kombe la Dunia,kupitia promosheni ya “Tunaliamsha Kivingine”.

Akiongea mjini Zanzibar wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo itakayodumu kwa kipindi cha miezi mitatu,Mtendaji Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa alisema “Kumekuwa kukitokea mabadiliko ya kila aina katika sekta ya mawasiliano siku hadi siku, ambayo yanatulazimu kwenda nayo sambamba ili kuhakikisha wateja wetu wanaendelea kupata huduma bora.Kazi tuliyofanya ya kuboresha miundombinu ya mtandao wetu, nawahakikishia wateja wetu wote kuwa huduma za data za Zantel ni bora zaidi kwa sasa na zinawezesha internet yenye kasi kubwa ambayo haijawahi kutokea huko nyuma”.

Aliongeza kusema kuwa kampeni hii imelenga zaidi upande wa Tanzania Visiwani na mikoa ya mwamboa ya Tanzania Bara “Napenda kuwahakikishia wateja wetu wote nchini Tanzania kwamba Zantel tumejipanga kuwekeza zaidi katika kuimarisha miundombinu ya mtandao wetu ili kuhakikisha unakuwa bora zaidi na kuwezesha wateja wetu kufurahia huduma za maongezi ,data na internetI”alisema, Khamis Mussa.

Kampeni ya “Tunaliamsha Kivingine” inakwenda sambamba na kuanzishwa kwa kifurushi kipya cha data kutoka Zantel,kinachowezesha wateja wake kujiunga nacho na kufurahia kuangalia michezo kupitia simu zao na vifaa vyao vingine vya mawasiliano kwa gharama nafuu.

Kifurushi cha Zantel cha Kombe la Dunia kinaanzia shilingi 1,000/-kwa siku,kifurushi cha shilingi 9,000/-kwa wiki na kifurushi cha shilingi 20,000/-kwa mwezi.Vifurushi hivyo vyote 3 vinawezesha kupata data ya 1GB,6GB na 16GB.Vifurushi vya Kombe la Dunia vya data vinapatikana kuanzia vya matumizi ya siku,wiki na mwezi,vinawezesha kuona michezo ya kombe la Dunia kwa programu ya StarTimes tu na kujiunga navyo ni kupitia huduma ya Ezypesa, pekee.

STARTIMES YASHEHEREKEA VALENTINE NA WATEJA

Meneja Masoko wa StarTimes Tanzania ,Felix Awino akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi hao
Bwana na Bibi Alex wakifurahi mara baada ya kukabidhiwa zawadi kampuni ya Star Times Tanzania
Meneja uhusiano wa kampuni ya Sar Times Tanzania Juma Suluhu akikabidhi zawadi kwa Bwana na Bibi Nuezy Fredrick 
Wafanyakazi wa Star Times Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa wameshika maua
Meneja uhusiano wa kampuni ya Sar Times Tanzania Juma Suluhu na Meneja Masoko wa StarTimes Tanzania ,Felix Awinowakikabidhi zawadi kwa washindi wa Ni Valentine's na Star Times
                                                       Na Mwandishi Wetu Dsm

KAMPUNI ya Star Times imesheherekea siku ya wapendanao na wateja wake kwa kutoa zawadi kadhaa katika promosheni yake ya "Ni Valentine na Startimes".

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi zawadi hizo, Meneja Masoko wa kampuni hiyo Tanzania, Felix Awino amesema Star Times inasheherekea siku hii kwa kuwazawadia wapenzi kupata chakula cha jioni na malazi ya Hotel ya kisasa.
“tunafurahi kusheherekea siku ya wapendanao na wateja kwa kuwa karibu nao kama sehemu ya upendo wetu kwao, kwa kuwapa promosheni na maudhui yanayoendana na wakati ,hivyo kwa wateja wetu wa Dar es Salaam watapata malazi SeaScape, Mwanza watalala katika hoteli ya Malaika , Meya wataenda Usungilo , Arusha Palece Hotel na kwa mkoa wa Dodoma watapata kupumzika katika Hotel ya Morena”amesema Awino.

Kwa upande wake mmoja wa washindi wa promotion hiyo ya ni Valentine na Startimes, Nuezy Fredrick amesema kuwa ni furaha kubwa kwao kama wateja wa Star Times kupata nafasi hiyo ya kupelekwa sehemu ya kifahari kama hiyo hili waweze kufurahi na wapenzi wao kutokana na kutumia king’amuzi cha Star Times.
Amesema kuwa star Times imemuheshimu na yeye ataendelea kutumia bidhaa za kampuni hiyo na kufurahia vipindi bomba vya kila siku.

BODI YA UTALII NA SHIRIKA LA NDEGE LA ATCL WASAINI MKATABA WA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII NCHINI NA HUDUMA ZA NDEGE ZA ATCL

a1
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii TTB Bi. Devotha Mdachi na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania ATCL Mhandisi  Ladislaus Matindi wakisaini mkataba wa ushirikiano katika kutangaza utalii wa Tanzania na Huduma za shirika la Ndege la ATCL katika hafla iliyofanyika kwenye makao makuu ya TTB Kinondoni jijini Dar es salaam huku Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso na Mwenyekiti wa Bodi ya TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo  pamoja na wanasheria wa mashirika hayo wakishuhudia tukio hilo.
a3
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii (TTB) Bi. Devotha Mdachi na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) Mhandisi  Ladislaus Matindi wakibadilishana hati za  mkataba wa ushirikiano katika kutangaza utalii wa Tanzania na Huduma za shirika la Ndege la (ATCL) katika hafla iliyofanyika kwenye makao makuu ya (TTB) Kinondoni jijini Dar es salaam huku Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso na Mwenyekiti wa Bodi ya (TTB) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo wakishuhudia tukio hilo.
a4
Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso kushoto  na Mwenyekiti wa Bodi ya (TTB) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo wakikata utepe kuzindua jarida lenye maelezo  kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu utalii wa Tanzania na vivutio vyake pamoja na maelezo kuhusu huduma za usafiri wa Anga za Shirika la Ndege la Tanzania ATCL litakalopatikana pia kwenye ndege za ATCL.
a5
Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso kushoto  na Mwenyekiti wa Bodi ya (TTB) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo wakionyesha jarida hilo mara baada ya kulizindua rasmi.
a6
Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso kushoto akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kusainiwa kwa mkataba huo.
a7
Mwenyekiti wa Bodi ya (TTB) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo kulia akizungumza na waandishi katika hafla hiyo.
a8
Baadhi ya maofisa wa ATCL na TTB kutoka kulia ni Mussa Kopwe Meneja Utawala na Rasilimali Watu  kutoka  TTB , Lilian Fungamtama Ofisa Masoko wa  ATCL na Geofrey Meena Meneja Masoko TTB.
a9
Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso kushoto  na Mwenyekiti wa Bodi ya (TTB) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo wakiwa katika picha ya pamoja kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii TTB Bi. Devotha Mdachi na Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la ATCL Mhandisi Ladslaus Matindi.
a10
Mwenyeviti wa Bodi ya Wakurugenzi ya  (ATCL), Emmanuel Korosso kushoto  na Mwenyekiti wa Bodi ya (TTB) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo wakiwa katika picha ya pamoja kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii TTB Bi. Devotha Mdachi na  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la ATCL Mhandisi Ladslaus Matindi pamoja na maofisa wengine wa TTB.
a11
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Utalii TTB pamoja na maofiza wa Wizara ya Maliasili na Utalii na TTB wakiwa katika hafla hiyo.