Ololosokwan yazindua utabibu kwa njia ya tehama

Mradi mkubwa wa kijiji cha digitali cha Ololosokwan, Loliondo umezinduliwa rasmi mwishoni mwa wiki, miaka miwili tangu kutiwa saini kwa uanzishwaji wake kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) na kampuni ya Samsung.

Hiki kitakuwa ni kijiji cha nne cha digitali barani Afrika cha kwanza kikiwa nchini Afrika Kusini huku kingine kikiwa Gabon na Ethiopia.

Kijiji hicho cha digitali ni nadharia ya Samsung katika kurejesha faida kwa umma na kina huduma mbalimbali ambazo zikiunganishwa na haja ya wananchi zitasaidia kubadili maisha ya wamasai na kuondokana na utegemezi wa mifugo pekee.

Uzinduzi rasmi wa kijiji hicho umefanywa na Mkuu wa mkoa Arusha Mrisho Gambo kwa niaba yaWaziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu.

Kijiji hicho cha digitali kina shule yenye tehama ikiwa na maunganisho ya intaneti, kiliniki ya kisasa ikiwa na kituo cha teknolojia ya mawasiliano yenye kuwezesha utabibu (telemedicine) na jenereta linalotumia nguvu za jua.

Mradi huo ambao ulishuhudiwa utiaji saini na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Bi. Leah Kihimbi kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Dkt. N. Iriya kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Dar es Salaam na wafanyakazi wa UNESCO mwaka 2014, kukamilika kwake kunawezesha UNESCO na serikali ya Tanzania kuwapatia wakazi wa eneo hilo huduma bora za afya na vijana wa Kimasai nafasi ya kupata elimu kutokana na ukweli kuwa kwa utamaduni na kazi zao za ufugaji wamekuwa wakipata shida ya kupata elimu.

Utiaji saini wake katika mwaka huo ulifanywa na Mkuu wa ofisi na Mwakilishi Shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania, Bw. Mike Seo .Kupitia kijiji hicho vijana wataendelea na masomo hata kama wanachunga mifugo yao kutokana na kupatiwa tablet ambazo zitawawezesha kujifunza hata wakiwa nje wakichunga mifugo yao.

Aidha miongoni mwa manufaa makubwa yatakayopatikana katika mradi huo wa kijiji cha digitali ni kuweza kupata nishati rahisi na iliyo rafiki kwa mazingira kwa kuwepo na jenereta linalotumia nishati ya jua.Kuwepo kwa kijiji hicho kunataka kudhihirisha ni kwa namna gani teknolojia inaweza kutumika kuleta mabadiliko chanya yanayotakiwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi waliopo vijijini.

Kijiji hicho cha Loliondo ambacho kitakuwa cha nne katika vijiji vya kidigitali barani Afrika kimeelezwa naMkuu wa mkoa wa Arusha Mheshimiwa Mrisho Gambo kama utekelezaji wa Sera ya Tiba Mtandao kutokana na kuzinduliwa kwa Kliniki Mtandao iliyopo katika Kijiji hicho.Katika uzinduzi wa mradi huo kwa ujumla wake, kliniki ndicho kitu ambacho kinaonekana kwenda karibu zaidi na wananchi wa Ololosokwan kwani itakuwa inatoa huduma za afya, bora za kisiasa na za haraka kwa wakazi wa kata za Soitsambu naa Oloipiri, Wilayani Ngorongoro.

Katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa mkoa wa Arusha ,Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Mhe Ummi Mwalimu wakati wa uzinduzi wa kliniki hiyo,alisema kuwa Tiba Mtandao imekua ni miongoni mwa Vipaumbele vya Wizara yake ili wananchi wote Tanzania waweze kupata huduma stahiki za matibabu pasipo kujali changamoto za Kijiografia zinazotukabili,

Pamoja na kufanya uzinduzi huo katika hotuba yake Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo aliwashukuru wote walioshiriki kuleta Mradi huo wa maana kwa mkoa wa Arusha kwani wangeweza kupeleka sehemu nyingine yeyote na kuongeza kuwa ni deni kubwa sana lazima tuhakikishe huduma hiyo imefanikiwa.

Akizungumzia masuala ya afya kama kipaumbele katika mradi huo wenye lengo la kuhifadhi utamaduni wa kimasai huku wakitumia teknolojia ya kisasa kuleta maendeleo katika elimu na kuhifadhi mazingira, Mkuu huyo wa mkoa akizungumza kwa niaba ya Waziri alisema kuwa kutokana na umuhimu wa sekta ya afya kwa kila Mtanzania ,serikali itaelekeza nguvu katika Kliniki hiyo ili kuiwezesha kutoa huduma stahiki na Kwa muda mrefu kwa wananchi wa maeneo haya.

"Kliniki hii ni ya kwanza Tanzania na itaweza kutoa huduma bora na za kisasa kwa njia ya mtandao kwa wananchi zaidi ya elfu kumi kutoka katika maeneo ambayo hapo awali wananchi walikuwa wanatembea umbali mrefu zaidi ya Kilomita 50 kufuata huduma za afya".

" Hii inadhihirisha kwamba mwananchi wa Ololosokwan na maeneo ya jirani anaweza kuhudumiwa na daktari bingwa aliyeko Muhimbili au kokote Duniani kupitia Klinik hii;na mfumo wa Mtandao uliopo unaruhusu upatikanaji wa huduma hizi kwa kipindi chote cha mwaka mzima".

Aidha aliitaka Halmashauri kutenga Bajeti kwa ajili ya kuongeza hadhi ya zahanati hiyo kuwa Kituo cha Afya ambapo itaenda sambamba na kuongeza majengo Pamoja na wataalam watakaoweza kutoa huduma stahiki Kwa wananchi.

Upatikanaji wa kituo cha Afya katika eneo hilo huku kukiwepo na kliniki mtandao kutasaidia kuokoa maisha ya wananchi ambao wengi wao waliamini kupona magonjwa makubwa ni mpaka uende KCMC au Muhimbili tu.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo Mkuu Shirika la Umoja wa mataifa linaloshigulikia Elimu na Sayansi (UNESCO) nchini Tanzania Bi. Zulmira Rodrigues alisema kijiji hicho ni ushuhuda tosha wa ukuaji wa teknolojia unaenda sambamba na maono ya shirika la Unesco la kutoa kipaumbele katika miradi ya sayansi inayosaidia wananchi wenye mahitaji moja kwa moja.

Alisema kwa kutambua adha waliyokuwa wanaipata wananchi wa Ololosokwan walitengeneza mradi ambao sehemu mojawapo ni kliniki Mtandao ili kuleta mabadiliko ya afya za watu kwa njia ya kisayansi.

Naye mkurugenzi wa Tiba Kutoka Wizara ya Afya Dr. Margareth Evelyne Mhando alishukuru Unesco kusaidia kutekeleza malengo ya Wizara kupitia Mradi huu wa kijiji cha digitali na kuongeza kuwa ni hatua nzuri katika sekta ya afya Kwa sababu hivi sasa wananchi waliombali na vituo vya Afya kupitia Mradi huu watapata huduma bora kutoka Kwa matabibu wabobezi.

Uzinduzi wa Mradi huu ulihudhuriwa pia na Balozi wa Switzerland Nchini Tanzania Bi. Florence Mattli, Wawakilishi wa Samsung ambao ndio waliotoa fedha na Teknolojia pamoja na wawakilishi kutoka Umoja wa Ulaya (EU).

Bi. Mattli alisema kwamba wataendelea kusaka wadau wengine kuhakikisha kwamba mradi huo unaendelea kutanuka na kufanikiwa kwa kujazia maeneo ambapo panahitaji nguvu nyingine.
Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Rashid Taka akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (kushoto aliyeketi) kuhutubia wageni waalikwa na wanakijiji wa Ololosokwan wilayani Ngorongoro kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa kijiji cha kidigitali chenye kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao uliofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Arusha.
Pichani juu na chini ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akisoma hotuba katika hafla ya uzinduzi wa kijiji cha kidigitali chenye kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu uliofanyika kwenye kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.

Pichani juu na chini ni baadhi ya wanakijiji wa Ololosokwan na wageni waalikwa wakimsikiliza mgeni rasmi RC Gambo kwenye hafla ya uzinduzi wa kijiji cha kidigitali chenye kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao uliofanyika mwishoni mwa wiki, wilayani Simanjro, mkoani Arusha.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akizungumzia ukuaji wa teknolojia ambayo inaenda sambamba na maono ya shirika lake kwenye hafla uzinduzi wa kijiji cha kidigitali chenye kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao uliofanyika mwishoni mwa wiki, wilayani Simanjro, mkoani Arusha.

Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Samsung Afrika Mashariki, Patricia Kingori akizungumza kwenye hafla uzinduzi wa kijiji cha kidigitali cha Samsung (Samsung Digital Village) kinachotumia umeme wa jua chenye kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao uliofanyika mwishoni mwa wiki, wilayani Simanjro, mkoani Arusha.
Balozi wa Uswisi nchini, Mh. Florence Tinguely Mattli akizungumza kwenye uzinduzi wa kijiji cha kidigitali cha Samsung (Samsung Digital Village) kinachotumia umeme wa jua ambacho kina kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao kilichopo katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Simanjro mkoani Arusha.

Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya, Dr. Margaret Mhando akitoa neno ambapo aliwashukuru Unesco kusaidia kutekeleza malengo ya wizara kupitia mradi huu wa kijiji cha kidigitali cha (Samsung Digital Village) unaoratibiwa na Shirika la UNESCO kwenye kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro, mkoani Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akimsikiliza kwa makini Balozi wa Uswisi nchini, Mh. Florence Tinguely Mattli wakati wa hafla ya uzinduzi wa kijiji cha kidigital cha Samsung chenye kituo cha huduma maalum za afya pamoja na kituo cha elimu kwa njia ya mtandao (Samsung Digital Village) uliofanyika kwenye kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.

1 ya 491 [EAC NEWS] EAC SECRETARY GENERAL, AMB. LIBERAT MFUMUKEKO TAKES OVER COMESA - EAC- SADC TRIPARTIE TASK FORCE CHAIRMANSHIP

PRESS RELEASE

EAC SECRETARY GENERAL, AMB. LIBERAT MFUMUKEKO TAKES OVER COMESA - EAC- SADC TRIPARTIE TASK FORCE CHAIRMANSHIP

Secretary General pledges to work towards the attainment of the Tripartite Free Trade Area by June 2017

East African Community Headquarters, Arusha, Saturday, 31th October 2016: The Secretary General of the East African Community, Amb. Liberat Mfumukeko today took over the Chairmanship of the COMESA-EAC-SADC Tripartite Task Force (TTF) over the next year from Dr. Stergomena Tax, the SADC Executive Secretary, who oversaw the work of the Tripartite from July 2015 to October 2016.

Addressing Hon. Members of the Council, Directors and senior officials from the COMESA, EAC and SADC Member States at the hand-over ceremony held over the weekend at the Hilton Hotel in Nairobi, Kenya, Amb. Liberat Mfumukeko, commended Dr. Stergomena Tax for the exemplary leadership during the period of the Tripartite, especially given the resource constraints which have delayed the launch of Phase II negotiations and the implementation of other important activities.

The Secretary General noted that there were many hurdles to be overcome in meeting the clear priorities the Tripartite Council had set and he prioritized resource mobilization: finalization of studies for phase II negotiations whereby EAC will work closely with COMESA Secretariat on the necessary actions to be taken; Tariff Offer Negotiations to always be on the agenda of the relevant Policy Organs; and lastly Ratification of Tripartite Free Trade Area. He disclosed that EAC has pledged to ratify and deposit instruments of ratification by the end of February 2017 and urged all Member/Partner States to ratify the Agreement before the end of June 2017.

At the hand over ceremony, which was also attended by Dr. Stergomena Tax, the SADC Executive Secretary, Dr. Kipyego Cheluget, the COMESA Deputy Secretary, and Mr. Peter Kiguta, the EAC Director-General, Customs and Trade, the Secretary General pledged to work towards the attainment of the Tripartite Free Trade Area by June 2017.

The main focus during the SADC Chairmanship (July 2015 to October 2016) was to lead the TTF to facilitate Member/Partner States implement the directives of the 3rd Tripartite Summit following the launch of the Tripartite Free Trade Area on 10th June 2015 in Sharm el Sheikh, Egypt, namely: expeditious operationalization of the COMESA-EAC-SADC Tripartite Free Trade Area; finalization of outstanding issues on the COMESA-EAC-SADC Tripartite Free Trade Area Agreement in relation to Annex 1 on Elimination of Import Duties, Annex 2 on Trade Remedies and Annex 4 on Rules of Origin and the legal scrubbing of completed Annexes; and ccommencement of Phase II negotiations covering trade in services, cooperation in trade and development, competition policy, intellectual property rights and cross border investments.

WAZEE WILAYANI ARUSHA WAMUOMBA RAIS KUWAPA NAFASI YA UWAKILISHI BUNGENI KATIKA NAFASI ZAKE KUMI

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Gabriel Daqarro wakitoa Maagizo kwa watendaji wa serikali na taasisi kuwapa kipaumbele cha kwanza wazee wakati akiongea na wazee wa Halmashauri ya jiji la Arusha leo jijini Arusha picha zote na mahmoud ahmad Arusha

Katikati Ni mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro na kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Arusha David Mwaiposa na kushoto ni mwenyekiti wa baraza la wazee wilaya Arusha Mhina Sezua wakati wa mkutano na mkuu huyo wa wilaya kubaini changamto mbali mbali wanazokumbana nazo wazee wilayani hapa

Meza kuu wakifuatilia hoja mbali mbali zilizokuwa zinatolewa na wazee leo jijini Arusha

Sehemu ya wazee waliohudhuria mkutano huo wakiwa wanamsikiliza mkuu wa wilaya Gabriel Daqarro

Katibu wa wazee akiongea katika mkutano huo

WAALIMU WASTAAFU NAO HAWAKUWA NYUMA KWENYE KIKAO HICHO

Katibu Tawala wilaya ya Arusha David Mwaiposa akiwa anamkaribisha mkuu wa wilaya kuongea na wazee ilikujua kero zinazowakabili

Mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro akiongea na wazee wa jiji la Arusha ambao wamemuomba mkuu huyo kuwafikishia salamu zao kwa viongozi wakuu wa serikali akiwemo raisi dkta John Magufuli kuwa wakifika Arusha waweze kuonana na baraza la wazee kama wanavyoonana na wazee wa Dar es salaam

Mwakilishi wa OCD nae akijibu maswali ambali mbali kwa niaba ya mkuu wa polisi wilaya ya Arusha

Mwenyekiti wa baraza la Wazee wilaya ya Arusha mjini Mhina Sezue akiongea katika mkutano huo ambao aliiomba serikali wilayani hapa kuwapa uwakilishi wazee kwenye mabaraza ya serikali kuanzia ngazi ya kijiji kata hadi Taifa huku wakimuomba raisi kuwapa nafasi moja katika zile kumi za uwakilishi wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania

Hata sisi hatupo nyuma kama walivyokutwa na kamera wakiingia ndani ya ukumbi wa Simba kwenye kituo cha mikutano cha AICC Leo Jijini Arusha

WAZEE HAWA NAO WALIKUWEPO KATIKA KUTOA MICHANGO YAO YA MAWAZO KUBORESHA HUDUMA ZAO

wakifuatilia mkutano huo kwa umakini

Bibi akifuatilia mkutano huo wa mkuu wa wilaya ya Arusha na wazee wa jiji la Arusha leo jijini Arusha

Sehemu ya wakifuatilia mkutano huo

Mandari ya muitikio wa wazee kwenye mkutano huo wakiwa katika ukumbi wa simba hall

wazee wakifuatilia mkutano huo kwa umakini na kueleza kero mbali mbali kwa mkuu wa wilaya ya Arusha

WAALIMU WASTAAFU NAO HAWAKUWA NYUMA KAMA HAPA WAKIFUTILIA MKUTANO HUO.Picha zote na mahmoud ahmad arusha
MKUU wa wilaya ya Arusha, Gabriel Fabian Daqarro, amemugiza afisa Usitawi wa jamii wa halmashauri ya jiji la  Arusha kuhakikisha wazee wote wa jiji hilo wanapatiwa vitambulisho kabla ya mwisho wa mwaka huu ili waweze kupata huduma mbalimbali ikiwemo matibabu kwenye  Hospitalini mbalimbali.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo hilo jana kwenye mkutano na wazee wa jiji la Arusha uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya kimataifa ,AICC, ulikuwa una lengo la kusikiliza kero za wazee ili zipatiwe ufumbuzi pia kufahamiana.

Mkuu huyo wa wilaya ameiagiza Idara hiyo kuhakikisha vitambulisho vinapatikana kabla ya mwisho wa mwezi, sanjari na kuwataka watendaji wa serikali, mashirika ya umma na taasisi mbali mbali za serikali katika jiji la Arusha kuhakikisha kuwa zinatoa kipaumbele kwa wazee ambao wamekuwa hawapati huduma zao kwa wakati.

Aidha amewataka wenyeviti wa mitaa,kata na tarafa kushirikiana na jeshi la  na jeshi la polisi kuhakikisha wanaimarisha usalama kwenye maeneo yao ili kuwezesha wazee kuishi kwa usalama bila kubughudhiwa na kuhakikisha wanasiamia maadili.

‘’Mumepewa madaraka ya kuimarisha ulinzi yatumieni ili wazee wasibughudhiwe ,tambueni kuwa wazee ni muhimu ndio waliotufikisha hapa sasa sitaki kusikia kuwa wanasumbuliwa sitaki kusikia malalamiko ya ya kuporomoka kwa maadili ””alisema Daqarrro.Wakichangia  kwenye mkutano huo wazee wamedai kuwa taasisi za fedha pamoja na halmashauri ya jiji haziko tayari kuwakopesha wazee kwa hofu ya kuwa watakufa karibuni na  kutaka dhana hiyo iondoke kwa kuwa kuzeeka sio kufa .

Wamesema nao wana mahitaji mbalimbali ya kuendesha sghuhuli zao za kiuchumi hivyo wanayo haki ya kupewa mikopo kama yalivyo makundi mengine ya jamii.

Wameomba kushirikishwa kuanzia ngazi ya mtaa hadi halmashauri ili wawe na wawakilishi wao ambao watawasilisdha kero zao kwenye vikao vya maamuzi vya serikali na baraza la madiwani pia wapate uwakilishi bungeni kama yalivyo makundi mengine ya walemavu, vijana na wanawake.

Wamelalamikia kukosa Vitambulisho ambavyo vingeliwawezesha kupata huduma za haraka kwenye taasisi mbalimbali za serikali,ikiwemo dawa kwenye hospital za serikali, pia wamelalamikia lugha za kuwadharirisha zinazotolewa na baadhi ya wahudumu wa hospital za serikali na vituo vya afya.Wamelalamikia hatua ya Zahanati kutokutoa huduma siku za mwisho wa wiki hali ambayo inawasababisha kukosa huduma za matibabu.Aidha wamelalamikia TASAF kutoa fedha kwa ajili ya watu wasiokuwa na uwezo kwa upendeleo ambapo walengwa wamekuwa hawanufaiki na mpango huo wa TASAF.

\

GAMBO ASHIRIKI UJENZI WA DARAJA FUPI LONGIDO




Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Mashaka Gambo ameshiriki ujenzi wa daraja fupi(drift) katika kijiji cha Orgirah kata ya Mundarara na tarafa ya Engarenaibow kwa lengo lakuhamasisha wananchi na viongozi wengine.
Akitoa msisitizo kwa viongozi kujitoa sana pale wanapoitajika kushiriki shughuli mbalimbali za  maendeleo kwa wananchi wao hasa zile ambazo zimeanzishwa kwa nguvu za wananchi wenyewe.
“Viongozi mbalimbali wasiwe wazito kujitoa katika shughuli kama hizi za maendeleo ya wananchi na hasa ambazo zimeanzishwa kwa nguvu za wananchi wenyewe nivema basi na serikali nayo kupitia viongozi kwa ngazi tofauti kujitokeza nakuunga mkono”.
Mradi huo wa daraja fupi(drift) ulianza rasmi mnamo Octoba ,2016 kwa lengo lakuunganisha vijiji viwili vya Orgirah na Igulailungwa ambavyo vilitenganishwa kwa ukosefu wa daraja hilo fupi na kupelekea kwa vijiji hivyo kukosa mawasiliano.
Aidha mradi huo mpaka kukamilika utagharimu kiasi cha shilingi milioni 9 ambapo mpaka sasa ni milioni 6 tu ndio zimetumika katika ujenzi huo, ikiwa Halmashauri ya Wilaya ya Longido ilichangia 450,000, Mkurugenzi wa halmashauri alichangia 640,000 na nguvu za wananchi ni milioni 5.
Hata hivyo Gambo aliwapongeza wananchi hao kwa juhudi walizozianza za ujenzi huo na hivyo serikali itawasaidia pale penye mapungufu na wananchi wenyewe wanatakiwa kujitokeza zaidi hususani kwenye shughuli kama hizo za maendeleo.
Mradi huo bado unamapungufu ya shilingi milioni 2 ili kukamilisha milioni 9 kama gharama nzima ya ujenzi na Mkuu wa Mkoa aliaidi kuchangia mifuko 30 ya simenti,pesa taslimu 500,00 na kutoa katapila ikiwa wananchi watakuwa tayari kuchangia mafuta. 
Meneja wa TANROAD Arusha Enginia John Kalupale aliaidi kuchangia mifuko 50 ya simenti.
Pia mwenyekiti wa chama cha CCM Mkoa Lekule Ole Laiza atachangia mifuko 30 ya simenti, mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido bwana Sabore Molleiment atachangia 500, 000, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Longido  Juma Muhina nae atachangia 400,000 na Halmashauri yenyewe itaenda kujadili kwenye vikao vyake namna yakusaidia ujenzi huo.
Gambo bado yupo ziarani Longido huku akishirikiana na wananchi wa Wilaya hio katika shughuli mbalimbali za maendeleo yao.


Wananchi wa kijiji cha Orgirah wakishiriki katika ujenzu wa daraja fupi(drift) kwenye kijiji chao.

Hili ndilo daraja fupi(drift) lililoanzishwa kwa nguvu za wananchi wa kijiji cha Orgirah kata ya Mundarara Wilayani Longido.

Vijana wasomi 53 wafyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni ya wanafunzi na nyumba za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani

 Vijana wasomi 53 wa grupu la Whatsapp la WAZALENDO wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani, umbali wa kilomita 151 kutoka Dar es salaam, na kilomita 53 kutoka makao makuu ya Wilaya. 
Vijana hao, ambao wameungana katika  grupu la Whatsapp la WAZALENDO,  leo wamekutwa wakifanya kazi hiyo nzito huku wakihamasika kwa nyimbo wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga (wa pili kulia pichani juu). 
 Vijana hao, 14 wakiwa wanawake na 39 wanaume, walikubaliana kupiga kambi shuleni hapo toka Septemba 27, 2016  na kufanya kazi hiyo ya kujitolea na bila malipo kwa moyo mmoja na kufanikiwa kufyatua matofali hayo. Kambi hiyo inatarajiwa kufungwa kesho Jumamosi Oktoba 29, 2016 na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako
 Mmoja wa vijana hao wasomi akielekea kazini
  Sehemu ya vijana hao wasomi 53 wakichota maji ili kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Sehemu ya vijana hao wasomi 53 wakichota maji ili kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Sehemu ya vijana hao wasomi 53 wakichota maji ili kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Sehemu ya vijana hao wasomi 53 wakichota maji ili kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga akielekeza vijana sehemu ya kuweka matofali 
 Kazi ikiendelea
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga akiwa katika picha ya pamoja  na vijana hao wasomi 53 baada ya kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga akipungia pamoja  na vijana hao wasomi 53 baada ya kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga akitoa maelekezo kwa vijana hao wasomi 53 baada ya kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakiwa bwenini
 Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakiwa bwenini ambako kuna uhaba wa nafasi kiasi cha kurundikana namna hiyo
 Huko jikoni msosi unaandaliwa
 Wanafunzi wa shule hiyo wakijipanga kupata chakula cha mchana
 Wanafunzi wanapata chakula na matunda kila mlo
 Mojawapo ya nyumba chache za walimu ambamo wanakaa walimu saba
 Walimu sita kati ya saba wanaoishi kwenye nyumba hiyo
 Nishati mbadala ya solar itumiwayo na walimu hao saba
 Wanafunzi wakipata mlo wa mchana
 Vijana wasomi wanawake wanalala hapa 
 Sehemu ya vijana hao 14 wanawake wakipumzika baada ya kazi nzito
 Pamoja na kufyatua matofali baadhi ya vijana hao wasomi ambao ni walimu walikuwa wakiingia darasani kufundisha. Hapa mwalimu akiandaa kipindi baada ya kufyatua matofali
 Mwalimu akiandaa kipindi
 Sehemu ya vijana hao
 Jiwe la msingi
 Nje ya darasa
 Mandhari ya sehemu ya shule hiyo
 Bweni la vijana wasomi wanaume
 Pamoja na kazi nzito ya kufyatua matofali vijana hawa wazalendo wana nyuso za furaha na kuridhika kwa kujitolea kwao
 "....HAPA KAZI TU!" anasema kijana huyu mzalendo
 Furaha ya kumaliza kazi kwa mafanikio
 Kijana mzalendo Petro Mgoti (suruali ya njano) alikuwa katika ziara ya mafunzo ya wiki sita nchini Ujerumani, na aliporejea nyumbani alienda moja kwa moja kujiunga na wenzie huko Mkuranga.
 Furaha ya ushindi
 Utamu wa uzalendo ni kufanya kazi na kufurahi kwa pamoja
 Vijana mapumzikoni
  Jengo la darasa la maabara ambalo sasa hutumika kama bweni la wanafunzi wa ziada
  Darasa la maabara ambalo sasa hutumika kama bweni la wanafunzi wa ziada
  Darasa la maabara ambalo sasa hutumika kama bweni la wanafunzi wa ziada
 Bweni kwa ajili ya wanafunzi ndani ya darasa la maabara
 Kila sehemu ya stoo ya darasa la maabara  hutumika kama bweni la wanafunzi wa ziada
 Stoo ya darasa la maabara  hutumika kama bweni la wanafunzi wa ziada
 Darasa la maabara ambalo sasa hutumika kama bweni la wanafunzi wa ziada
 Hayo matofali ni alama ya kuwa upande huo wa mbele ni wa Msikiti kwa ajili ya walimu na wanafunzi wa Kiislamu. Wakristo na waumini wa madhehebu mengine hutumia madarasa
 Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakielekea bwenini
 Baada ya kazi na msosi sasa ni wakati wa kuimba wimbo wa kambi
 Wimbo wa kambi ukiimbwa na kuchezwa kwa furaha
 Kijana akishukuru kwa kuhitimishwa kwa kazi hiyo
 Mmoja wa vijana hao akishukuru Mungu kwa kumaliza kazi salama
 Sehemu ya vijana hao
 Vijana wakiwa katika kikao kidogo cha kuhitimisha kazi
  Kijana mzalendo Petro Mgoti (suruali ya njano) akisema machache. Yeye alikuwa katika ziara ya mafunzo ya wiki sita nchini Ujerumani, na aliporejea nyumbani alienda moja kwa moja kujiunga na wenzie huko Mkuranga.
 Baada ya kazi nzito Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga akijiunga kupata msosi na  vijana hao wasomi 53 baada ya kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
Vijana hao wasomi 53 wakipata msosi baada ya kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani.