MTOTO WA MIAKA MIWILI ALIYEKUWA AKIVUTA SIGARA 40 KWA SIKU AACHA KUVUTA SIGARA


Mtoto wa kiume wa miaka miwili aliyekuja kuwa maarufu kimataifa baada ya kuwa na tabia ya kuvuta zigara katika kijiji kimoja nchini Indonesia ameacha tabia hiyo na kupungua uzito na sasa amekuwa anafanya vizuri katika shule anayosoma.

Mtoto huyo Aldi Rizal alipata umaarufu mnano mwaka 2010 alipogundulika katika kijiji kimoja masikini huko Sumatra, Indonesia, akivuta sigara 40 kwa siku huku akiendesha kigari cha watoto.

Miaka miwili baadaye mtoto huyo aliacha tabia hiyo ya uvutaji sigara kwa msaada wa serikali ya Indonesian kwa kumpatia tiba maalum ya kuondokana na tabia hiyo, na kufanikiwa kuachana kabisa na uvutaji sigara.
                                    Mtoto Aldi Rizal akivuta sigara yake huku akiendesha kigari cha watoto
                            Mtoto Aldi Rizal anavyoonekana sasa akiwa na umri wa mika tisa 
                  Mtoto Aldi Rizal akicheza shuleni hivi sasa amekuwa ni mwenye tabia nzuri 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni