Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Matukio. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Matukio. Onyesha machapisho yote

Arusha kulindwa kwa CCTV- Camera


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (katikati) akizungumza na
Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnite akizungumza
aliyeambatana na Wabunge toka Sweden walipotembelea Ofisini kwake hivi karibuni.



ARUSHA

MKOA wa Arusha umeanza kujipanga katika utaratibu wa kulinda
mji kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya CCTV – Camera ili kuimarisha usalama
wa mji “Safe City”, Mfumo huu utawezeshya Mji kulindwa masaa 24 dhidi ya
uhalifu kwa raia, wawekezaji na watalii.

Kauli hiyo ilitolewa leo mjini hapa na Mkuu wa Mkoa huo Mrisho Gambo ofisini
kwake mara baada ya kutembelewa na Balozi wa Sweden nchini, Bi. Katarina
Rangnite aliyeambatana na Ujumbe wake wa Wabunge kutoka Nchini Sweden.
Akizungumza na ujumbe huo RC Gambo alisema, mkoa huo tayari umekwisha
kuonyesha nia ya kuwekeza katika mfumo huo ili kuwaongezea wananchi na
mali zao usalama zaidi.

“Nia yetu ni kuona hali ya usalama katika mkoa wa Arusha ikiwa ya juu sana ili
kuendelea kuwavutia watalii zaidi kutoka nchi mbalimbali Duniani. Malengo yetu
ni kuwa na mifumo itakayoulinda mkoa wetu kwa Saa 24 na mwaka mzima,”
alisema RC Gambo na kuongeza:
“Hatua hii itaongeza ulinzi kwa raia na mali zao, pia kwa wawekezaji waliopo
mkoani kwetu na watalii wanaokuja kutembelea hifadhi na vivutio mbalimbali
kwani Arusha ndio kitovu cha utalii hapa nchini,” alisema.

Kwa upande wake Balozi Rangnite ambaye kiongozi wa msafara huo
uliojumuisha pia wabunge kutoka Bunge la Sweden wanaowakilisha Kamati ya
Kilimo na Mazingira, alikubaliana na nia ya kuwekeza kwenye mfumo wa
usalama wa mkoa wa Arusha.

Balozi Rangnite alimueleza Mkuu wa Mkoa Gambo kwamba, nchi ya Sweden
inayo wataalamu waliobobea katika mifumo hiyo ya usalama wa miji hivyo
alimuomba Gambo kuwasilisha kwake maandiko ya vitu vinavyohitajika ili
kuwezesha mradi huo kutekelezwa.

“Tukipata maandiko mbalimbali ya mradi tunaweza kuangalia ni wapi Serikali
ya Sweden inaweza kuwekeza ikiwamo kusaidia kwa manufaa ya wananchi wa
nchi zote mbili,” alisema Balozi Rangnite.

Aidha Gambo alitoa ombi kwa Balozi wa Sweeden kushirikiana na Mkoa wa
Arusha kwenye Kampeni ya Kulinda vyanzo vya Maji ili kuwezesha mradi
mkubwa wa maji unaosimamiwa na mamlaka ya maji safi na maji taka
(AUWSA) kutekelezwa kwa mafaniko makubwa. Itakumbukwa kwamba
imepatiwa Bil 476 ili kumaliza tatizo la maji Jiji hapa.

Katika ziara ya ujumbe huo pamoja na mambo mengine ulikuwa na lengo la
kuangalia fursa mbalimbali za uwekezaji katika Kilimo, Mazingira na maeneo
muhimu kutoka mkoani Arusha.

Ujumbe huo kutoka Sweden ukiongozwa na Balozi Rangnite uliridhishwa na
kuvutiwa na maeneo ya utalii yaliyopo katika mkoa huo yakiwamo pia mazingira
rafiki yanayoruhusu uwekezaji kwa jamii yao.
Kiongozi wa ujumbe toka Sweden Bi. Matilda Irnkarns (kushoto) akikabidhi
zawadi yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo


Kutoka kushoto ni Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnite
akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mashaka Gambo pamoja na
Kiongozi wa msafara wa wabunge toka Sweden Bi. Matilda Irnkarns kwenye
picha ya pamoja baada ya Kikao
Katika picha ya pamoja ni kutoka kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa Ndg.
Kwitega, Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnite , Mkuu wa Mkoa
wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo, kiongozi wa msafara wa wabunge toka Sweden
Bi. Matilda Irnkarns, ujumbe toka Sweden pamoja na viongozi wa Ofisi ya Mkuu
wa Mkoa wa Arusha.

MRISHO GAMBO ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UTUME – KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO - ARUSHA


Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo(Katikati) akikata utepe kama ishara ya maadhimisho ya maiaka 50 ya
Utume Burka,kushoto ni Mch. Mchungaji Eliasi Ijiko na kulia ni Askofu Godwin
Godwin Lekundayo.


ARUSHA.

Viongozi wa dini nchini wameombwa kuhamasisha waumini wao kufanya kazi
kwa bidii na kulipa kodi ili kuongeza kasi ya kuleta maendeleo katika Taifa la
Tanzania na pia wametakiwa kuhamasisha waumini wao kuhakikisha wanadai
risiti kila wanapoenda kununua bidhaa au kupata huduma mbalimbali.

Kauli hiyo ilitolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho
Mashaka Gambo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Dr John Joseph Pombe Magufuli aliyekuwa mgeni rasmi katika
Maadhimisho ya miaka 50 ya Utume wa Kanisa la Waadventista wa Sabato.

Akizungumza na waumini na viongozi wa Kanisa hilo lililopo Burka mjini hapa,
Mkuu wa Mkoa Arusha Gambo alisema, Watanzania wanalojukumu la kufanya
kazi kwani hata Vitabu vya Dini vimeelekeza kuwa mtu asiyefanya kazi na asile
na mafundisho hayo ya dini yanaendana na falsafa ya hapa kazi tu.

Mhe. Gambo aliendelea kusisitiza kwamba kutokana na maelekezo hayo ya
vitabu vya dini ni wazi kwamba kila mtu anatakiwa kufanya kazi kwa kadiri ya
uwezo aliopewa na Muumba ili apate riziki hatua itakayowezesha pia
kupunguza wategemezi katika Taifa letu.

Akizungumza katika maadhimisho hayo RC Gambo kwa niaba ya Rais Magufuli
alisisitiza kuwa ni vyema kwa kila mmoja wetu kufanya kazi na kulipa Kodi.

"Kwa yule ambaye hatalipa Kodi ajue kwamba anaikosesha nchi yake mapato
ambayo yangeweza kutumika kuendesha shughuli mbalimbali za maendeleo, pia
tutambue kwamba huduma zote ni gharama na zinatokana na kodi tunazolipa.

Hivyo katika Serikali ya Awamu ya Tano asiyefanya kazi na asile na zaidi ya
hapo asiyelipa kodi ni vyema akafahamau kwamba analirudisha taifa lake
nyuma. Niwaombeni sana viongozi wa Dini muhamasishe waumini walipe kodi
kwa mustakabali wa Taifa letu"

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista wa Sabato
Ulimwenguni Mch. Geofrey Mbwana akitoa somo fupi wakati wa maadhimisho
hayo alisema amefurahishwa sana na uteuzi wa Mhe. Gambo na ana imani na
vijana kwa sababu vijana wakati wao ni sasa na pia ni Taifa la leo hivyo
wakipewa nafasi kama hii hudhihirisha vipawa vilivyomo ndani yao na bila
shaka Mkoa wa Arusha utakua Mkoa kielelezo kwa Taifa hili.

Kanisa hili la Sabato katika Tanzania lilianzishwa Katika kijiji cha Giti kilichopo
Mamba Miamba huko Same mnamo mwaka 1903 na kuendelea kukua katika Mji
wa Shirati Mara na kisha kufika Arusha na kuanzisha Kanisa la Burka mwaka
1966 likiwa na Jengo moja dogo na waumini nane tu.

Hivi sasa Kanisa hili lina majimbo mawili na waumini zaidi ya 500,000
Tanzania. Kanisa hili pia wanamiliko Chuo Kikuu kimoja, Shule za Sekondari 17,
Msingi 11 na shule za awali 11. Pia Kanisa hili lina Hospital moja, Kituo cha
Afya kimoja na Zahanati 28.

RC Gambo aliendelea kuwaomba viongozi mbalimbali wa dini wazidi
kumuombea na kumtia Moyo Mhe. Rais katika kazi yake ngumu na kubwa
anayoifanya kwa maslahi ya Taifa haswa kusaidia wanyonge ambao kwa muda
mrefu hawakuwa sehemu ya Agenda kubwa ya Serikali. Pia waendelee
kuwasisitiza wanasiasa watambue kuwa wakati wa Siasa umekwisha ni vyema
Mhe. Rais akapewa nafasi ya kuwatumikia watanzania kwa yale aliyoyaahidi
kupitia utekelezaji wa ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI na watakutana tena
kwenye siasa mwaka 2019 - 2020.Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho
hotuba ya Mgeni Rasmi kwa viongozi wa kanisa na waumini wa Kanisa la
Waadventista wa Sabato.
Katika picha ya pamoja ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo
(katikati) na viongozi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato.


Mchungaji Eliasi Ijiko akimuonyesha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho
Gambo vitabu na majarida mbalimbali yanayochapishwa na Taasisi za kanisa la
wasabato Tanzania
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(Kushoto) akiendelea
kutembelea mabanda ya maonyesho katika maadhimsho ya miaka 50 ya Kanisa
la Wasabato, Burka.

UNDP YAZINDUA RIPOTI YA KAZI NA MAENDELEO YA BINADAMU, MAVUNDE AAGIZA KAZI ZENYE STAHA

 

IMG_6050
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde (katikati) akiwasili kwenye uzinduzi wa ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) huku akiwa ameambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida (kulia) uliofanyika Machi 11, 2016 jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
 
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu) Antony Mavunde ametaka kuondolewa kwa changamoto maeneo ya kazi ili kazi isaidie maendeleo ya binadamu badala ya kujikimu.
 
Naibu Waziri huyo alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzindua ripoti ya maendeleo ya binadamu ya mwaka 2015 inayoelezea kazi kwa maendeleo ya binadamu.
 
Alisema kwa sasa kuna figisu kubwa katika kazi nchini hasa kutokana na waajiri wengi kugeuza kazi kama sehemu ya kujikimu kwa wafanyakazi wao kwa kutowapa stahiki husika ikiwamo mikataba ya ajira.
 
Alisema kazi inapokuwa ni ya kujikimu kunakuwa na migogoro mingi na kuvurugika kwa uzalishaji na kutishia maendeleo ya taasisi husika na maendeleo ya mtu binafsi.
 
Alisema Tanzania imefurahishwa na yaliyomo katika ripoti hiyo ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kutokana na kuzungumzia jinsi kazi zinavyoweza kusaidia upatikanaji wa maendeleo.
 
Alisema wakati Tanzania inaelekea kujipanga kwa uchumi wa kati, Ripoti inaonyesha ni jinsi gani kazi inaweza kuboresha maisha ya Mtanzanzania kwa kuondoa kazi na kuwapatia wananchi kazi zenye staha na zinazoweza kuwasaidia wao binafsi na hivyo kukuza uchumi na ustawi wa jamii.
 
Alisema amekuwa akizungumza katika maeneo mengi ya kazi na kukutana na changamoto nyingi zikiwemo za kukosekana kwa mikataba, mazingira mabaya ya kufanyakazi, ujira usiokidhi na kutaka waajiri kufuata sheria za kazi kwa kuwapatia mikataba ya kazi na pia kuhakikisha kazi zinakuwa na staha.
 
Awali akizungumza na wageni waalikwa katika hafla hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dar es Salaam, alisema kwamba uzinduzi wa kitaifa ambao unafuatia uzinduzi wa kimataifa uliofanyika mwaka jana mjini Addis Ababa, Ethiopia ni faraja kubwa kwa wadau wa maendeleo nchini.
 
Alisema uzinduzi huo unaweka ripoti hiyo karibu zaidi na wananchi na kuahidi serikali kuifanyia kazi kutokana na umuhimu wake hasa wa kuhakikisha kazi inasaidia maendeleo ya watu.
Anthony Mavunde
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde (kushoto) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (katikati) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida (kulia) kabla ya kuelekea kwenye uzinduzi rasmi wa ripoti ya maendeleo ya watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) uliofanyika Machi 11, 2016 jijini Dar es Salaam na kuratibiwa na ESRF.
Anasema ripoti hiyo inaonesha namna ambavyo kazi inaweza kuchangia maendeleo na ustawi wa jamii.
Alisema wakati Tanzania inaelekea kuwa taifa ambalo limejengeka katika msingi wa maendeleo ya watu kama ilivyokusudiwa tangu kupatikana kwa Uhuru wake 1961, Ripoti hiyo ni chanzo kizuri cha maarifa katika kufanikisha mabadiliko yanayotakiwa kufanikisha maendeleo ya watu.
Alisema kazi ni msingi wa maendeleo kwa hiyo ni vyema kuboresha mazingira ya kazi na wafanyakazi ili kuleta maendeleo kusudiwa kwa kuwa na kazi zenye staha.
Alipongeza UNDP na wadau wengine kwa kufanikisha uzinduzi huo ambao alisema umeenda sanjari na dhima ya serikali ya kutumia maarifa yote yaliyopo kusaidia maendeleo ya watu.
Ripoti hiyo ya UNDP imetazama kwa undani kuhusu kazi, mahusiano ya kazi na maendeleo ya binadamu.
George Mulamula
Mshehereshaji wa uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) akisherehesha uzinduzi huo uliofanyika Machi 11, 2016 jijini Dar es Salaam na kuratibiwa na ESRF.
Aidha imeangalia masuala ya usalama wa kazi na mahitaji ya utaalamu; masuala ya kulipwa na kutolipwa kazini, uangalizi, kujitolea ubunifu na kazi endelevu.
Pia ripoti hiyo inatoa majumuisha yanayostahili kufanywa bali mapendekezo ya utengenezaji wa sera unaotanua uzalishaji kwa kutoa fursa na kulinda wafanyakazi, ubora wa kazi, ujira stahiki, kazi yenye staha na kazi endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Kimsingi Ripoti hiyo inapendekeza kuongeza faida za maendeleo ya binadamu, kupitia utendaji kazi, kwa kupendekeza mikakati ya kujenga fursa za ajira, ili kuhakikisha ustawi wa wafanyakazi, na kuendeleza maeneo yaliyolengwa, ambayo yatabadilisha hali halisi ya sasa.
Aidha ainaangalia Sera zilizopendekezwa, kuhakikisha utendaji kazi bora, utendaji kazi endelevu, ambayo inachangia usawa, badala ya kujenga ukosefu wa usawa, na kazi ambayo inaheshimu haki za wafanyakazi, na kuhakikisha usalama wao.
Human Development Report 2015, Tanzania
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisoma taarifa kwenye uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) uliofanyika jijini Dar es Salaam Machi 11, 2016 na kuratibiwa na ESRF.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo kuna hatua njema kwenye maendeleo ya watu katika ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara, Tanzania ikiwamo lakini ipo haja ya kuangalia pengo kubwa lililopo katika fursa mbalilmbali zikiwamo za kazi.
Imeelezwa ndani ya ripoti hiyo kwamba toka mwaka 2000 nchi ziloizo kusini mwa Jangwa la Sahara zimekuwa na ukuaji wa maendeleo ya binadamu( Human Development Index -HDI) wa kazi wa kiwango cha asilimia 1.7 kati ya mwaka 2000 na 2010 : asilimia 0.9 kwa mwaka 2010 na 2014.
HDI ni kipimo kinachotathmini maendeleo ya muda mrefu ya afya na maisha marefu, elimu na maisha yenye staha.
Kwa Tanzania kumekuwepo na ongezeko la HDI la asilimia 1.18% kati ya mwaka 1985 na 2014, ikiongezeka kutoka 0.371 hadi 0.521, ikiwa ni ongezeko la asilimia 40.5 juu ya ongezeko la nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara la 0.518.
Human Development Report 2015, Tanzania
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde (hayupo pichani) kuhutubia wageni waalikwa kwenye hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) uliofanyika jijini Dar es Salaam Machi 11, 2016 na kuratibiwa na ESRF.
Mratibu wa Umoja wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizungumza katika uzinduzi huo alisema kwamba ongezeko hilo si haba.
Hata hivyo aliwaambia wadau waliokuwepo kushuhudia uzinduzi huo kwamba Taifa bado linakabiliwa na changamoto nyingi zikkiwemo umaskini uliokithiri, kutanuka kwa pengo la usawa na kushindwa kuhimili matukio ya mabadiliko ya tabianchi na uchumi.
Aidha alisema kwamba :”Ripoti ya maendeleo ya binadamu ya mwaka 2015, inaonyesha kuwa, kuimarisha maendeleo ya binadamu, kupitia utendaji kazi, inahitaji sera na mikakati katika maeneo makuu matatu: kujenga fursa za ajira, kuhakikisha ustawi wa wafanyakazi na kuendeleza maeneo yaliyolengwa. Hii inaongeza kasi ya kutengeneza ajira nchini Tanzania.”
Tanzania ikiwa na zaidi ya watu milioni 12 wakiishi katika umaskini na wengi wao uliokithiri changamoto kubwa kwa Tanzania, ni kutafsiri uwezo huu katika miundombinu inayoonekana, kwa kujenga mazingira mazuri, na kuongeza ujuzi wa watu wake kama ilivoainishwa katika Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu mwaka elfu mbili na kumi na tano.
Human Development Report 2015, Tanzania
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde akisoma hotuba ya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) kwa niaba ya Waziri Jenista Mhagama, uliofanyika jijini Dar es Salaam Machi 11, 2016 na kuratibiwa na ESRF.
Alisema changamoto zote hizo ni za kweli na zenye uhusiano na maendeleo ya binadamu na ni vyema ilivyowekwa katika Muono wa maendeleo ya Tanzania kufikia 2025 na utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
Katika hotuba yake ya shukurani Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini, Awa Dabo, alisema kwamba taasisi yake ipo tayari kusaidia Tanzania na nchi nyingine kuwezesha kutambua uhusiano kati ya kazi na maendeleo ya binadamu katika utekelezaji wa Maendeleo endelevu (SDGs).
Human Development Report 2015, Tanzania
Mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde (katikati) na meza kuu wakijiandaa kuzindua ripoti hiyo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Ofisi ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, Bi. Mary Kawar, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Awa Dabo.
UNDP HUMAN DEVELOPMENT REPORT 2015 LAUNCH
Mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde (katikati) akizindua rasmi Ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015) kwenye hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Machi 11, 2016.
Anthony Mavunde
Mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde akionyesha ripoti hiyo kwa wageni waalikwa na waandishi wa habari (hawapo pichani).
IMG_6200
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Ofisi ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, Bi. Mary Kawar, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Mh. Anthony Mavunde, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Awa Dabo kwa pamoja wakiwa wameshikilia ripoti hiyo.
Human Development Report 2015
Muonekano wa Ripoti ya Maendeleo ya Watu ya mwaka 2015 (Human Development Report 2015).

EALA CALLS FOR FULL IMPLEMENTATION OF THE COMMON MARKET PROTOCOL, CITES SENSITISATION AS KEY IN THE PROCESS

The Regional Assembly is urging Partner States to “up their game” in sensitization activities particularly when it comes to the Common Market Protocol in order to raise awareness and showcase benefits to the citizens of the region.
At the same time, the EALA wants Partner States to adopt a phased implementation of the EAC Common Market by prioritizing aspects that carry quick wins or deliver immediate multiplier effects.  This move shall endear citizens to take advantage of the benefits that shall accrue from the Common Market protocol.
The Assembly today debated and adopted the Report of an Oversight activity on the Security related challenges of implementing the Common Market Protocol along the Central Corridor.
The Report presented to the House by the Chair of the Regional Affairs and Conflict Resolution Committee, Hon Abdullah Mwinyi follows the oversight activity undertaken by the Committee in the United Republic of Tanzania in November 2015.
The activity aimed at appreciating first-hand, the existing security related operational challenges of implementing the Common Market Protocol along the Central Corridor; Non-Tariff Barriers (NTBs) constraints including numerous police road blocks and check points; and the ongoing reforms and projects on course to ease cargo transportation in landlocked Partner States of Burundi, Rwanda and Uganda. 
The objective of the Committee was to comprehend and appreciate the implementation of the Common Market Protocol along the Central Corridor and to ascertain the challenges faced in the implementation. 
The Committee held a field trip visiting Dar es Salaam, all through to Vigwaza weighbridge and roadblocks.  It further interacted with various stakeholders including officials of the Ministry of EAC, Ministry of Labour and Employment and the Tanzania Bureau of Standards (TBS). Others included the Business Community, Members of the Tanzania Police Force and the Tanzania Roads Agency (TANROADS) Officials. 
The Committee observed that United Republic of Tanzania had developed a national Common Market Protocol implementation strategy and a national Committee to realize the same.   It further strengthened the National Monitoring Committee for Elimination of Non-Tariff barriers and had commenced on the issuance of the machine readable identifications.

The Committee was nonetheless informed that implementation of the Common Market Protocol continued to lag behind owing to a number of factors including; Inadequate awareness among Private Sector, implementing agencies and the general public on the provisions and implementation of EAC CMP as well as delays by the sectoral Ministries, Departments and Agencies (MDA’s) to amend national laws relevant to the said Protocol. In addition, the Committee took cognisance of the funding requirements for smooth implementation of the EAC Protocol.
During debate, Members noted that Partner States should emulate the United Republic of Tanzania to modernize the weighbridge technology and scales to ensure enhanced speed and accuracy in weighing process targeting reduction of bribery incidences, fines for overloading and time taken in the weighing process.   
At the same time, United Republic of Tanzania should work with other Partner States to re-look on the validity through research the issue of yellow fever cards within the EAC region as an impediment to free movement of persons
Hon Bernard Mulengani remarked that it was necessary to also look at security related matters such as Illegal roadblocks, arrests and the ever worrying trend of terrorism gaining entry through the free movement of persons.  He further requested the Council of Ministers to clarify on the term foreigner in advent of the Common Market Protocol.
Hon Valerie Nyirahabineza decried the constant delays by Partner States to amend the national laws to conform to the Common Market Protocol.  “Article 47 requires Partner States to align their legislation to CMP.  This is vital, she said.  What happens if the laws in the Partner States are not aligned with that of the EAC? Are we going to continue to benefit from the Protocol? She asked.
“In the case of the Customs Union, we have a legal framework in the name of the Customs Union Management Act. It is a high time we have a coordinating structure to handle this aspect,” she added.
Hon Shyrose Bhanji said Tanzania had done well with regards to removal of NTBs. One of the major challenges however is that of lack of sensitization to the public, she said. 
This is not only a recurring problem but looks more like a chronic problem,” she said.  We need more sensitization to the publics to create awareness here in the country.  Even EALA Members need to be more involved in-country   This shall enable us also to brief Tanzanians and other East Africans,” she said.
Hon Makongoro Nyerere however said the various weighbridges on the central corridor continued to delay the speed of movement of goods.  “They need to be reduced so that we also spur free movement of people from one point to another”, he added.
“Hon Mumbi Ngaru said the Government of Kenya had continued to prioritise sensitization of its citizens on the EAC.  “The Council needs to formulate a policy around sensitization.  This is very key., she said.
Others who supported the report were Hon Shyrose Bhanji, Hon Makongoro Nyerere, Hon Martin Ngoga and Hon Ussi Maryam.  Hon Odette Nyiamilimo, Hon Isabelle Ndahayo, Hon Christophe Bazivamo and Hon Taslima Twaha also gave a nod to the report.

NEC: HAKUNA WIZI NA UDANGANYIFU WA KURA UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA 25

 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC), Jaji Damian Lubuva akisalimiana na Mwakilishi wa Chama cha Kitaifa cha Watu Wasioona Zanzibar (ZANAB), Adili Mohamed wakati wa mkutano baina ya taasisi za watu wenye ulemavu nchini na NEC iliyofanyika leo Jumanne Septemba 29, 2015 Jijini Dar es Salaam.
  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC), Jaji Damian Lubuva akisalimiana na Mwakilishi wa Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Mkoa wa Dar es Salamm Mohamed Chazi  wakati wa mkutano baina ya taasisi za watu wenye ulemavu nchini na NEC iliyofanyika leo Jumanne Septemba 29, 2015 Jijini Dar es Salaam.
  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva akiteta jambo na Kamishna wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Vincent Msena wakati wa mkutano baina ya NEC na wawakilishi wa vyama vya watu wenye ulemavu nchini uliofanyika leo Jumanne Septemba 29, 2015 Jijini Dar es Salaam.
  Mwakilishi wa Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Mkoa wa Pwani Hussein Kibindu akisoma taarifa ya mada ya tathimini ya uchaguzi mkuu wa oktoba 25 mwaka huu wakati wa mkutano baina ya taasisi za watu wenye ulemavu nchini na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) uliofanyika leo Jumanne Septemba 29, 2015 Jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Mkoa wa Mwanza, Alfred Kapole akichangia mada wakati wa mkutano mkutano baina ya taasisi za watu wenye ulemavu nchini na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) uliofanyika leo Jumanne Septemba 29, 2015 Jijini Dar es Salaam.
  Mkalimani wa lugha ya alama, Kudra Munishi akitoa ufafanuzi wa mada na hoja kwa watu wenye ulemavu wa kusikia wakati wa mkutano baina ya taasisi za watu wenye ulemavu nchini na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) uliofanyika leo Jumanne Septemba 29, 2015 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA NA ISMAIL NGAYONGA).

Na Ismail Ngayonga MAELEZO
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)  imevitoa wasiwasi  vyama vya siasa  kuwa hakutakuwepo na wizi na udanganyifu wa kura katika matokeo ya uchagauzi wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajia kufanyika nchini tarehe 25 Oktoba, mwaka huu.
AIdha NEC imesema ipo tayari kushirikiana na wataalamu wa vyama hivyo katika kubaini vyanzo vya wizi wa kura iwapo tatizo hilo litajitokeza na hivyo kuhakikisha haki inatendeka kwa vyama vyote vinavyoshiriki uchaguzi huo.

Hayo yamebainishwa leo Jumanne (Septemba 29, 2015) Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Damian Lubuva wakati wa mkutano wake na wawakilishi wa vyama vya watu wenye ulemavu aliokutana nao kwa ajili ya kupata ushauri na maoni ya taasisi hizo kuelekea uchaguzi mkuu mwezi oktoba mwaka huu.

Jaji Lubuva alisema hadi kufikia sasa, vyama vyote vyote vinavyoshiriki uchaguzi huo vimefanyika kampeni za kistaarabu ingawa katika siku za hivi karibuni baadhi ya vyama vimekuwa vikitoa kauli na matamshi yaliyovuka mipaka, ambapo NEC imevionya vyama kuacha mara moja tabia hiyo.

“Vipo baadhi ya vyama vya siasa na wagombea wao  wamekuwa wakitumia muda mwingi kutoa lugha zisizofaa baada ya kunadi sera ya vyama vyao, vyama hivyo tumekutana nao na kuwataka kuacha mara moja kampeni za aina hiyo” alisema Jaji Lubuva.

Jaji Lubuva alisema tarehe 27 Julai mwaka huu, vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mkuu vilisaini maktaba wa maadili ya uchaguzi huo, hivyo ni wajibu wa vyama hivyo kuzingatia viapo walivyotoa katika maktaba huo.

Akifafanua zaidi Jaji Lubuva alisema iwapo chama chochote hakina hoja ya kuzungumza na  wananchi ni vyema kikawa kimya hadi siku ya uchaguzi tarehe 25 Oktoba mwaka huu.
Aidha Jaji Lubuva alivitaka vyama vya siasa kuacha tabia ya kuingilia masuala ya utawala ya tume hiyo, kwani kwa kufanya hivyo vyama hivyo vitakuwa vikifanya kazi za tume hiyo na hivyo kuingilia masuala ya ndani ya kiutendaji ya taasisi hiyo.

Akizungumzia maandalizi ya uchaguzi huo, Jaji Lubuva alisema mahitaji yote ya msingi ya uchaguzi huo tayari yamepokelewa na NEC ikiwa karatasi, wino, na masanduku ya kura ambapo baadhi yake yameanza kusafirishwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Kuhusu Daftari la kudumu la wapiga kura, Jaji Lubuva alisema katika kipindi cha siku 10 zijazo kuanzia sasa Tume hiyo inatarajia kusambaza daftari la kudumu katika mikoa yote nchini na wananchi watatakiwa kuhakiki majina yao katika kipindi cha siku 8.