| Katibu Mkuu wa Chama cha Maofisa Kumbukumbu na Taarifa za Afya Tanzania (THERIA), Rehema Mwaipaja akizungumza na wanachama wa THERIA kabla ya kufungwa kwa Mkutano wao juzi. |
| Katibu Mkuu wa Chama cha Maofisa Kumbukumbu na Taarifa za Afya Tanzania (THERIA), Rehema Mwaipaja akizungumza na wanachama wa THERIA kabla ya kufungwa kwa Mkutano wao juzi. |
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu ameziagiza hospitali mbalimbali nchini kuhakikisha zinachukua tahadhari za kuwalinda wafanyakazi wake kitengo cha kumbukumbu katika mazingira ya kupata maambukizi hasa wanapokuwa kazini wakitimiza majukumu yao.
Waziri, Mwalimu ametoa maagizo hayo kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Uhakiki Ubora wa Huduma za Afya kutoka wizara hiyo, Dk. Mohamed A. Mohamed alipomwakilisha katika hafla ya kufungwa kwa mkutano wa Chama cha Maofisa Kumbukumbu na Taarifa za Afya Tanzania (THERIA) zilizofanyika juzi jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dk. Mohamed alisema wizara hiyo, inatambua mazingira hatarishi ambayo wafanyakazi wa kitengo cha kumbukumbu wamekuwa wakifanyia kazi hasa ukizingatia wao ndio watu wa kwanza kukutana na wagonjwa kabla ya kufika kwa madaktari jambo ambalo linaweza kuzua maambukizi kwa magonjwa yaambukizwao kwa njia ya hewa.
“..Natambua pia mazingira mnayofanyia kazi wengi wenu yanayowafanya kuwa kwenye hatari ya kupata magonjwa ya kuambukiza kwani nyie ndo wa kwanza kabisa kukutana na mgonjwa, kabla ya kuonana na daktari au mtaalamu wa vipimo, hivyo kupata maambukizi ya magonjwa hatarishi hasa yaambukizayo kwa njia ya hewa na mengineyo ni rahisi. Woizara yangu inapenda kuwaagiza Wakuu wote wa hospitali nchini kuhakikisha wanarekebisha mazingira mnayofanyia kazi ili kuondoa hali hii,” alisema Dk. Mohamed akimwakilisha waziri wake.
Aidha wizara hiyo pia iliahidi kushughulikia kero ya uhaba na ukosefu wa wafanyakazi wa taaluma ya utunzaji kumbukumbu za afya kwenye vituo vya afya na hospitali hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuzitaka hospitali na vituo hivyo kuajiri watu wenye taaluma halisi ya utunzaji kumbukumbu na kuhakikisha kada hiyo inapata muundo, stahili zake na kutambulika kama ilivyo kwa makundi ya kada nyingine.
Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Maofisa Kumbukumbu na Taarifa za Afya Tanzania, Rehema Mwaipaja akizungumza katika mkutano huo alisema kuwa THERIA ina umuhimu mkubwa hasa ukizingatia kuwa takwimu sahihi za afya ndio msingi bora kwa huduma kamilifu kwa jamii. Aliongeza kuwa uboreshaji wa hali ya ukusanyaji, uchambuzi na utunzaji wa takwimu sahihi za afya unachangia kuboresha tafiti mbalimbali za afya ambazo ni matunda ya ukuaji na uboreshaji wa huduma kiujumla.
“Nidhahiri kuwa ukuaji wa taaluma ya afya hutegemea sana tafiti mbalimbali zitokanazo na taarifa zilizokusanywa na kutunzwa kikamilifu kazi ambayo ni ya msingi kwa afisa kumbukumbu wa afya mahali popote anapofanya kazi, hayo yote huleta faida kwa wagonjwa, taasisi na kwa wafanyakazi,” alisema Bi. Mwaipaja.
Wanachama wa THERIA kutoka mikoa mbalimbali walikutana kwa siku mbili mfululizo katika wao mkuu uliofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine mkutano huo ulifanya uchaguzi kupata viongozi wapya wa chama hicho.
Mchezaji nyota wa zamani wa
Manchester United, Ryan Giggs ametengana na mkewe Stacey, na
kunamadai kuwa wanatarajia kuivunja rasmi ndoa yao.
Wawili hao walionekana kwenye
sherehe pamoja miezi mitatu iliyopita na kwa sasa bado Giggs na
Stacey wanaishi kwenye nyumba moja.
Winga huyo wa zamani wa Manchester
united, anatuhumiwa kuwa na mahusiano na wahudumu wakike wa hoteli
yake anayoimiliki, Jijini Manchester.
Hii si mara ya kwanza kwa Giggs
kuchepuka kwani aliwahi kuchepuka na mke wa mdogo wake wa kiume
Rhodri aitwae Natasha Lever kwa miaka nane, pia na mwanamitindo
Imogen Thomas.
Watoto mapacha walioungana mwili
waliozaliwa hospitali ya rufaa ya Pwani mjini Mombasa nchini Kenya
wamefariki dunia leo alfajiri.
Watoto hao walizaliwa Alhamisi na
walikuwa wasafirishwe kwa ndege kwenda Hospitali ya Taifa ya Kenyatta
kwa matibabu maalum wamefariki wakiwa kwenye chumba cha wagonjwa
mahututi.
Akithibitisha vifo vya mapacha hao
Mtendaji Mkuu CPGH Dk. Iqbal Khandwalla ameviambia vyombo vya habari
vya Kenya kwamba jitihada za madaktari za kuokoa maisha ya watoto hao
zimeshindikana.
Kaimu
Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akiwa anapokea kadi ya
chadema na kumkabidhi ya CCM alikuwa mgombea wa udiwani kata ya Kisimani
kupitia Tiketi ya chadema Amani John Mgonja Mara baada ya kuhamia Ccm.
Na Mahmoud Ahmad, Kilimanjaro
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM )umesema muda mfupi ujao Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kitaifuata mahali viliko vyama vya NCCR-Mageuzi, TLP na Chama cha Wananchi (CUF ) kwa sababu kimejidhuru kukubali kukumbatia mafisadi .
Aidha umoja huo umevitaja vyama hivyo sasa vinachechemea, vinaishi kwa matimaini na viko mahututi kwani wakati wowote , ugonjwa uliovitafuna vyama hivyo utakishambiulia chadema.
Matamshi hayo yametamkwa leo na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka wakati akizungumza na wanachama wa Uvccm na jumuiya zake katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Maendeleo Kata ya Mabogini wilaya ya Moshi vijijini.
Shaka alisema jeuri na mbwembwe za NCCR 'Mgeuzi, CUF na TLP muda umepita na sasa havina mategemeao tena ya kuibuka na kushindana na chama tawala .
Alisema vyama hivyo hupenda kujiita vyama vya siasa jambo ambalo alisema si kweli kwasababu kujiendesha kwake kunamtegemea mtu badala ya kujijenga na kuwa taasisi kamili.
Alisema vyama hivyo vineajua kutegemea makapi yaloachwa na ccm ili yawasaidie kuendesha masuala ya kisiasa .
Shaka akizungimza katika mkutano huo alimtolea mfano mbunge wa Moshi vijijini Anthony Komu (chadema) akisema hana uwezo wala uaminifu katika dhima ya kuwatumikia wananchi kwasababu historia yake ya kisiasa haionyeshi kama mtu madhubuti na mwenye msimamo.
"Komu alikuwa mwanachama na kiongozi wa NCCR -Mageuzi tokea mwaka 1992 , akahama na kujiunga Chadema akivutiwa na ukabila, wakati fulani akataka aende TLP Mrema akamuwekea ngumu , aina ya kiongozi kama Komu ni ushahidi tosha si kiongozi muaminifu , kesho sivajabu ukasikia amegama chadema kurudi ccm "alisems Shaka
Hata hivyo Kaimu huyo katibu Mkuu aliitaka halmashauri ya wilaya ya Moshi vijijini kufanya kila linalowezekana kupekeka maji katika maeneo ya kata ya Mabogini ili wananchi waondokane na adha ya ukosefu maji.
"Wananchi wa Moshi vijijini nakuhalikishieni kuwa ujenzi wa barabara yenu umbali wa kilomita 14 toka TPC hadi Chekereni itatekelezwa na serekali ya Dk Magufuli kwa kiwango cha lami "alisema shaka.
Katika kijiji cha Chekereni kata ya mabogini wanachama wapya 34 wamejiunga na Uvccm, 27 CCM na UWT wanachama 12.
Afisa polisi mmoja ameuwawa kwa
mlipuko uliokuwa ndani ya gari karibu na Makao Makuu ya Jeshi la
Polisi kusini mashariki mwa mji wa Gaziantep nchini Uturuki.
Maafisa polisi 19 na raia wanne
wameripotiwa kujeruhiwa na mlipuko huo uliotokea leo asubuhi.
Uturuki imekuwa ikikumbwa na matukio
ya mfululizo ya milipuko tangu mwaka uliopita, inayofanywa na
wapiganaji wa Kikurdi na Dola ya Kiislam (IS).
RAIS WA ZANZIBAR, DK. SHEIN ASHIRIKI SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI KATIKA VIWANJA VYA UKUMBI WA SALAMA BWAWANI
posted on
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akipokea maandamano ya Wafanyakazi mbali mbali wa Taasisi za Serikali na
Binafsi, wakipita mbele yake wakati wa sherehe za siku ya Wafanyakazi
Duniani katika viwanja vya Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja leo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akipokea maandamano ya Wafanyakazi mbali mbali wa Taasisi za Serikali na
Binafsi,(pichani) Vijana waliobeba bango kutoka Ofisi ya Makamo wa Pili
ya Rais akipita mbele yake wakati wa sherehe za sikuya Wafanyakazi
Duniani katika viwanja vya Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja leo.
Wafanyakazi
wakipita mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein(hayupo pichani) na bango lao linalotoa
ujumbe"IDARA YA FIDIA NI UTI WA MGONGO WA MAISHA YA WAFANYAKAZI NI
MUHIMU KUANZISHWA" wakati alipokuwa akipokea maandamano ya Wafanyakazi
wa Taasisi mballi mbali za Serikali na Binafsi katika sherehe za siku ya
Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo viwanja vya Ukumbi wa Salama
Bwawani Mjini Unguja
Wafanyakazi
wakimpungia mkono Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein(hayupo pichani) wakati alipokuwa akipokea
maandamano ya Wafanyakazi wa Taasisi mballi mbali za Serikali na Binafsi
katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo viwanja
vya Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja.
Baadhi
ya Viongozi na Wafanyakazi wa Taasisi za Serikali na Binafsi wakiwa
katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika
Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja leo mgeni rasmin akiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
Baadhi
ya Vingozi na Wafanyakazi wa Taasisi mbali mbali za Serikali na Binafsi
wakiwa katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo
katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja, mgeni rasmin akiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
Baadhi
ya Vingozi na Wafanyakazi wa Taasisi mbali mbali za Serikali na Binafsi
wakiwa katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo
katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja,mgeni rasmin akiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
Baadhi
ya Vingozi na Wafanyakazi wa Taasisi za Serikali na Binafsi wakiwa
katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika
Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja leo mgeni rasmin akiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(katikati) pamoja na Viongozi mbali mbali wakinyanyua mikono juu
kuashiria Mshikamano wakati wa sherehe za kilele cha siku ya Wafanyakazi
Duniani,ambazo sherehe zimewajumuisha mbali mbali wa Taasisi za
Serikali na Binafsi katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja leo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akimakabidhi zawadi Musssa Yussuf wa ZSSF Laki Sitafedha taslim akiwa
mfanyakazi Bora Chama cha ZAFICOWV katika sherehe za Siku ya wafanyakazi
Duniani Zilizofanyika leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akimakabidhi zawadi Bi.Asya Rajab Said fedha taslim laki tano,kutoka
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akiwa mfanyakazi Bora
Chama cha ZUPHE katika sherehe za Siku ya wafanyakazi Duniani
Zilizofanyika leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akimakabidhi zawadi Nd,Yunus Sose Hassan fedha taslim laki tano kutoka
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akiwa mfanyakazi Bora
Chama cha ZUPHE katika sherehe za Siku ya wafanyakazi Duniani
Zilizofanyika leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akitoa hutuba yake kwa Wafanyakazi mbali mbali wa Taasisi za Serikali na
Binafsi pamoja na Wananchi wakati wa Kilele cha siku ya Wafayakazi
Duniani sherehe zilizofanyika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja leo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akitoa hutuba yake kwa Wafanyakazi mbali mbali wa Taasisi za Serikali na
Binafsi pamoja na Wananchi wakati wa Kilele cha siku ya Wafayakazi
Duniani sherehe zilizofanyika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja
leo.Picha na Ikulu.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)

















