Mhadhiri
 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. James Jesse akitoa mada mbele ya 
waandishi wa habari kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya 
Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa warsha ya siku moja 29 
Aprili 2016 Mkoani Morogoro.
 
  
Afisa
 Utetezi na Haki za Binadamu wa Shirika la Under The Same Sun (UTSS) Bi.
 Perpetua Senkoro akitoa mada kuhusu masuala ya watu wenye ulemavu 
kupewa haki zao wakati warsha ya siku moja kuhusu Mpango
 wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) 
wakati wa warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.
 
 
 
   Wadau
 wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakiwa katika picha ya 
pamoja na Waaandishi wa Habari waliohudhuria mafunzo ya siku moja ya 
warsha kuhusu Mpango wa Kimataifa 
wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa 
warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.
  (Picha zote na Benedict Liwenga)
 
  Na Benedict Liwenga.
 
 
Asasi
 za Kiraia pamoja na Taasisi za kutetea haki za binadamu nchini 
zimewaasa Waandishi wa Habari nchini kujikita katika kuhabarisha umma 
kuhusiana na masuala ya haki za binadamu ikiwemo mauaji ya watu wenye 
ualbino, mauaji ya vikongwe, ukatili dhidi ya watoto, pamoja na adhabu 
ya vifo. 
  
Rai
 hiyo imetolewa leo na Kamishna wa Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bi.
 Salma Ally Hassan wakati wa Warsha ya siku moja iliyofanyika mkoani 
Morogoro yenye lengo la kuwajengea uelewa Wanahabri kuhusu Mpango wa 
Kimataifa wa kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR). 
  
Bi.
 Salma ameeleza kuwa kutokana na tathmini ya masuala ya haki za binadamu
 nchini, vyombo vya habari havinabudi kuwa na uelewa mkubwa kuhusu 
umuhimu wa kuziongelea haki za binadamu kwani jamii imekuwa haizitambui 
baadhi ya haki hizo na kumekuwepo na kukithiri kwa vitendo vya uvunjifu 
wa amani yakiwemo matukio ya mauaji ya watu wenye ualbino, vikongwe 
pamoja na ukatili kwa watoto. 
  
Ameongeza
 kuwa, baadhi ya watu nchini wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi kwa 
kuua watu ambapo watu wenye kuyasemea hayo ni Vyombo vya Habari lengo 
likiwa ni kukemea kuendelea kwa vitendo hivyo. 
  
“Uvunjaji
 wa haki za binadamu unafanywa na watu katika jamii, kwa mfano, mauaji 
ya Watu wenye Ualbino, mauaji ya vikongwe, pale sio Serikali inakua 
imevunja haki za binadamu, bali ni watu katika jamii”, alisema Bi. 
Salma. 
  
Kwa
 upande wake Mshauri wa masuala ya haki za binadamu kutoka Ofisi ya 
Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Bi. Chitralekha Massey ameeleza kuwa, 
ni vema Tanzania ikakubalina na mapendekezo yanayohusiana na masuala ya 
haki za binadamu yanayoendana na Dunia kwa ajili ya ulinzi wa haki hizo. 
  
“Sisi
 kama Umoja wa Mataifa tunapenda kuona Tanzania inafanya uamuzi 
utakaosaidia kuboreshwa kwa haki za binadamu nchini kwani ni wakati sasa
 wa jamii kusema kwa uwazi kuwa mapendekezo hayo yatakuwa yenye manufaa 
kwao”, alisema Massey. 
  
Aidha,
 katika warsha hiyo, vyombo vya habari, jamii pamoja na Serikali 
wanajukumu la kulinda haki za binadamu na kuendelea kukemea matukio 
yanayovunja amani katika jamii. 
  
Tarehe
 9 Mei, 2016 Tanzania inatarajiwa kufanyiwa tathmini ya pili juu ya hali
 ya haki za binadamu nchini na Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa ambapo
 tayari Asasi za Kiraia na Watetezi wa haki za binadamu wamekwisha 
wasilisha mapendekezo yao kwa Wawakilishi wa nchi wanachama wa umoja 
huo. 
 | 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni