Wataka EU na AU kutoshiriki katika mazungumzo ya amani ya Burundi

buj1
Jiji la Bujumbura linavyoonekana katika picha.
………………………………………………………………………………………………
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Vyama tisa vya upinzani vilivyoshiriki  uchaguzi wa Burundi  wa mwaka 2015 na ambavyo vinashiriki mazungumzo ya kutafuta amani ya Burundi vimetaka wawakilishi wa  umoja wa Ulaya  na Umoja wa Afrika kutoshiriki katika mazungumzo ya amani ya Burundi.
Viongozi wa vyama hivyo kwa pamoja wanasema kuwa  wawakilishi wa taasisi hizo wameonyesha kuegemea upande katika mgogoro wa Burundi kufuatia msimo wao wa kutaka chama cha CNARED ambayo wanadai imeshiriki katika vurugu na mauaji nchini Burundi kushiriki katika mazungumzo hayo.
Katika taarifa yao ilitiwa sahihi  na viongozi wote tisa  wa vyama hivyo ,wamesema kutokana na lugha  na misimamo ya wawakilishi hao wa taasisi za juu  ni wazi wataharibu mchakato huo unaoendelea wa n kutafuta amani ya Burundi.
Taaarifa iliyotolewa na viongozi wa vyama hivyo baada ya kumalizika mazungumzo  ya awali ,viongozi hao wamemtaka msuluhishi wa mgogoro huo Rais  mstaafu wa Tanzania  kutokukubalina  na wawakilishi hao na kushirikisha pande zote zenye masilahi na mgogoro wa Burundi. 
“Tunamtaka msuluhishi alione hili  na kuonya taasisi hizo kuacha propaganda za kuwagawa Warundi katika mgogoro huo “taaarifa hiyo ilisema .
Taarifa hiyo ilisisitiza kuwa Burundi itizamwe kama serikali halali iliyochaguliwa na wananchi na haipaswi kuingiliwa uhuru wake na watu ama taasisi za nje.
Aidha taarifa hiyo ilivitaja vyama hivyo kuwa ni UPRONA ,FNL,FNL IRYAGIRAGAHUTU,RADEBU,zingine ni RADEBU,FLORINA,MSPINKINZO Y’IJAMBO ,PMP,PRP na PIEBU.
Na katika hatua nyingine akifunga mazungumzo hayo ya awali msuluhishi wa mgogoro huo Rais Benjamen Mkapa ameeleza kuridhishwa na jinsi wajumbe wa mazungumzo hayo walivyoshiriki mazungumzo hayo ya awali kwa dhati na kuonyesha nia kutaka amani katika taifa lao.
“Nimeguswa na namna mlivyoonyesha katika fikra na mawazo yenu ,mmeonyesha uzalendo mkubwa kwa kuonyesha madhara ya mgogoro katika nchi yenu kiuchumi na maisha ya watu  yanayoharibiwa na mgogoro huo”Alisema Mkapa .
Mkapa ambaye anafanya usuluhishi huo chini ya rais Yoweri Mseveni aliyeteuliwa na marais wa Afrika mashariki kutatua mgogoro alishukuru uwepo uwepo wa taasisi za kimataifa na za kikanda katika mazungumzo hayo.
Aidha rais Mkapa aliwaambia wajumbe  wa mkutano  huo kwa muda wa wiki tatu zijazo atahakikisha kuwa anafanya mazungumzo na makundi mengine ambayo yalialikwa lakini hayakuweza kufika Arusha kutoa maoni yao kuhusu utatuzi wa mgogoro wa nchi yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni