Jiji la Bujumbura linavyoonekana katika picha. 
………………………………………………………………………………………………
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Vyama tisa vya upinzani 
vilivyoshiriki  uchaguzi wa Burundi  wa mwaka 2015 na ambavyo 
vinashiriki mazungumzo ya kutafuta amani ya Burundi vimetaka wawakilishi
 wa  umoja wa Ulaya  na Umoja wa Afrika kutoshiriki katika mazungumzo ya
 amani ya Burundi.
Viongozi wa vyama hivyo kwa 
pamoja wanasema kuwa  wawakilishi wa taasisi hizo wameonyesha kuegemea 
upande katika mgogoro wa Burundi kufuatia msimo wao wa kutaka chama cha 
CNARED ambayo wanadai imeshiriki katika vurugu na mauaji nchini Burundi 
kushiriki katika mazungumzo hayo.
Katika taarifa yao ilitiwa 
sahihi  na viongozi wote tisa  wa vyama hivyo ,wamesema kutokana na 
lugha  na misimamo ya wawakilishi hao wa taasisi za juu  ni wazi 
wataharibu mchakato huo unaoendelea wa n kutafuta amani ya Burundi.
Taaarifa iliyotolewa na viongozi 
wa vyama hivyo baada ya kumalizika mazungumzo  ya awali ,viongozi hao 
wamemtaka msuluhishi wa mgogoro huo Rais  mstaafu wa Tanzania  
kutokukubalina  na wawakilishi hao na kushirikisha pande zote zenye 
masilahi na mgogoro wa Burundi. 
“Tunamtaka msuluhishi alione 
hili  na kuonya taasisi hizo kuacha propaganda za kuwagawa Warundi 
katika mgogoro huo “taaarifa hiyo ilisema .
Taarifa hiyo ilisisitiza kuwa 
Burundi itizamwe kama serikali halali iliyochaguliwa na wananchi na 
haipaswi kuingiliwa uhuru wake na watu ama taasisi za nje.
Aidha taarifa hiyo ilivitaja 
vyama hivyo kuwa ni UPRONA ,FNL,FNL IRYAGIRAGAHUTU,RADEBU,zingine ni 
RADEBU,FLORINA,MSPINKINZO Y’IJAMBO ,PMP,PRP na PIEBU.
Na katika hatua nyingine akifunga
 mazungumzo hayo ya awali msuluhishi wa mgogoro huo Rais Benjamen Mkapa 
ameeleza kuridhishwa na jinsi wajumbe wa mazungumzo hayo walivyoshiriki 
mazungumzo hayo ya awali kwa dhati na kuonyesha nia kutaka amani katika 
taifa lao.
“Nimeguswa na namna mlivyoonyesha
 katika fikra na mawazo yenu ,mmeonyesha uzalendo mkubwa kwa kuonyesha 
madhara ya mgogoro katika nchi yenu kiuchumi na maisha ya watu  
yanayoharibiwa na mgogoro huo”Alisema Mkapa .
Mkapa ambaye anafanya usuluhishi 
huo chini ya rais Yoweri Mseveni aliyeteuliwa na marais wa Afrika 
mashariki kutatua mgogoro alishukuru uwepo uwepo wa taasisi za kimataifa
 na za kikanda katika mazungumzo hayo.
Aidha rais Mkapa aliwaambia 
wajumbe  wa mkutano  huo kwa muda wa wiki tatu zijazo atahakikisha kuwa 
anafanya mazungumzo na makundi mengine ambayo yalialikwa lakini 
hayakuweza kufika Arusha kutoa maoni yao kuhusu utatuzi wa mgogoro wa 
nchi yao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni