……………………………………………………………………………………
MMOJA
wa majaji wa Shindano la Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT)
2015, ambaye pia ni mchoraji vibonzo maarufu nchini, Nathan Mpangala
amelipongeza Baraza la Habari Tanzania (MCT), kwa kumpa heshima ya kuwa
mmoja wa majaji wa tuzo hizo zilizofanyika wiki iliyopita Jijini Dar es
Salaam.
Akizungumzia
ushiriki wake katika shindano hilo, alisema toka kinyang’anyiro hiko
kianze mwaka 2009 hakijawahi kuwa na jaji mchora vibonzo. Safari hii MCT
wameliona hilo. Ni jambo zuri na la kupongezwa.
“Yanapofanyika
mashindano ya aina yeyote yale, ni vema yakahusisha watu waliobobea
katika eneo husika ili waweze kusaidia kutoa miongozo,” alisema
Mpangala.
Jopo
hilo la majaji liliongozwa na Bi. Valerie Msoka, wajumbe wengine
ni Bw. Ndimara Tegambwage, Dkt. Joyce Bazira Ntobi, Bw. Ali Uki, Bw.
Jesse Kwayu, Bw. Kiondo Mshana, Bw. Juma Dihule, Bw. Godfrey Nago
na Bi. Pili Mtambalike.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni