JAJI WA SHINDANO LA TUZO ZA EJAT 2015, NATHAN MPANGALA ALIPONGEZA BARAZA LA HABARI TANZANIA (MCT)

1Baadhi ya majaji wa Shindano la Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) 2015, wakifuatilia utoaji tuzo wa shindano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam wiki iliyopita. Kutoka kushoto ni Bw. Nathan Mpangala, Bw. Juma Dihule, Bw. Kiondo Mshana, Bi. Valerie Msoka (Mwenyekiti), Bw. Ndimara Tegambwage na Dkt. Joyce Bazira Ntobi.
2Jaji wa Shindano la Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) 2015, Nathan Mpangala (kushoto) akimkabidhi tuzo Bw. Mansour Jumanne wa SAUT FM ya Mwanza katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.
……………………………………………………………………………………
MMOJA wa majaji wa Shindano la Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) 2015, ambaye pia ni mchoraji vibonzo maarufu nchini, Nathan Mpangala amelipongeza Baraza la Habari Tanzania (MCT), kwa kumpa heshima ya kuwa mmoja wa majaji wa tuzo hizo zilizofanyika wiki iliyopita Jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia ushiriki wake katika shindano hilo, alisema toka kinyang’anyiro hiko kianze mwaka 2009 hakijawahi kuwa na jaji mchora vibonzo. Safari hii MCT wameliona hilo. Ni jambo zuri na la kupongezwa.
“Yanapofanyika mashindano ya aina yeyote yale, ni vema yakahusisha watu waliobobea katika eneo husika ili waweze kusaidia kutoa miongozo,” alisema Mpangala.
Jopo hilo la majaji liliongozwa na Bi. Valerie Msoka, wajumbe wengine ni  Bw. Ndimara Tegambwage, Dkt. Joyce Bazira Ntobi, Bw. Ali  Uki, Bw. Jesse  Kwayu, Bw. Kiondo Mshana,  Bw. Juma Dihule, Bw. Godfrey  Nago na  Bi. Pili Mtambalike.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni