……………………………………………………………………………………
MMOJA
 wa majaji wa Shindano la Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) 
2015, ambaye pia ni mchoraji vibonzo maarufu nchini, Nathan Mpangala 
amelipongeza Baraza la Habari Tanzania (MCT), kwa kumpa heshima ya kuwa 
mmoja wa majaji wa tuzo hizo zilizofanyika wiki iliyopita Jijini Dar es 
Salaam.
Akizungumzia
 ushiriki wake katika shindano hilo, alisema toka kinyang’anyiro hiko 
kianze mwaka 2009 hakijawahi kuwa na jaji mchora vibonzo. Safari hii MCT
 wameliona hilo. Ni jambo zuri na la kupongezwa.
“Yanapofanyika
 mashindano ya aina yeyote yale, ni vema yakahusisha watu waliobobea 
katika eneo husika ili waweze kusaidia kutoa miongozo,” alisema 
Mpangala.
Jopo
 hilo la majaji liliongozwa na Bi. Valerie Msoka, wajumbe wengine 
ni  Bw. Ndimara Tegambwage, Dkt. Joyce Bazira Ntobi, Bw. Ali  Uki, Bw. 
Jesse  Kwayu, Bw. Kiondo Mshana,  Bw. Juma Dihule, Bw. Godfrey  Nago 
na  Bi. Pili Mtambalike.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni