Na Benedict Liwenga, Maelezo.
Kiongozi
 wa Chama cha Kisoshalisti kilichojulikana kama “NAZI” Adolf Hitler 
(1889-1945) alikuwa mmoja kati ya Madikteta dhalimu na mwenye nguvu 
kuwahi kutokea katika karne ya 20. 
Baada
 ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mbabe huyo aliamka kwa nguvu kupitia 
Chama hiko cha Wafanyakazi wa Ujerumani na kuchukua udhibiti wa Serikali
 ya Ujerumani mnamo mwaka 1933.
Hitler
 aliamuru uanzishwaji wa kambi za mateso dhidi ya Wayahudi na makundi ya
 watu wengine huku akiamini kuwa kufanya hivyo ilikuwa chachu na tishio 
tosha dhidi ya ukuu wa himaya ya Aryani na hatimaye kusababisha vifo vya
 zaidi ya Wayahudi wapatao milioni Sita.
Mashambulizi
 ya Ujerumani dhidi ya nchi ya Poland mwaka 1939 ndiyo yaliyoanzisha 
Vita Kuu ya Pili ya Dunia ambapo mpaka kufikia mwaka 1941Ujerumani 
iliteka sehemu kubwa ya ardhi ya Ulaya na Afrika Kaskazini. 
Ili 
kuepuka kukamatwa kwa kukwepa utumishi katika jeshi la Austria-Hungary, 
Adolf Hitler aliondoka toka Vienna na kuelekea Munich mnamo Mei 1913 
lakinibaadaye alilazimika kurudi tena.
Taarifa
 za kihistoria zinasema kuwa Kiongozi huyo wa Nazi alijiunga na jeshi la
 Bavaria na kuanza kufanya kazi za kujitolea ambapo mwaka uliofuata 
alishiriki kikamilifu katika vita ya Kwanza ya Dunia akiwa mstari wa 
mbele upande wa Magharibi ambapo uzoefu wake katika vita na mapambano 
uliathiri mawazo, fikra na mitazamo yake yote baada ya hapo.
Baada
 ya Vita Kuu ya kwanza ya Dunia, Hitler alichukua udhibiti wa chama hiko
 cha wafanyakazi wa Ujerumani kama kiongozi hivyo alitumaini 
kingemwezesha kushika dola ya Ujerumani punde si punde.
Aliposhindwa
 kwenye jaribio la Mapinduzi la mwaka 1923 yeye na wenzake walikamatwa 
na kufungwa jela na baada ya kutoka jela alijitahidi kukijenga chama 
hiko na kuanza mikakati ya kukamata dola kwa njia zilizo halali.
Hitler
 alikusudia kufanya mageuzi na kuendesha sera za kibaguzi ambazo 
zingetoa nafasi ya kutosha kwa Wajerumani kuweza kuishi katika himaya 
kubwa duniani.
Kwanza
 alitabiri ingekuwa rahisi kuiteka Czechoslovakia, na kufuatiwa na 
Ufaransa ambayo ilikuwa kizingiti kigumu kwa wakati huo hatimaye 
kumalizia na nchi ya Uingereza.
Kwa 
mujibu wa mikakati ya Adolf Hitler, vita ya Tatu ingefuata juu ya 
uvamizi dhidi ya Jumuiya ya Kisovieti ambayo kwake ulikuwa ni mtihani 
ambao alipanga afaulu kwa kufikiri vita ingepiganwa kwa haraka na kwa 
urahisi.
Kwa 
mujibu wa fikra zake za kuipiga Urusi, hii ingempa utajiri wa malighafi 
za kutosha hususan mafuta ambayo yangemwezesha kuandaa mkakati wa 
maandalizi ya vita ya Nne dhidi ya Marekani.
Vita
 hiyo ingekuwa rahisi tu kwake endapo Ujerumani ingeweza kuwa na ndege 
ziwezazo kusafiri masafa marefu pamoja na meli za kivita na kwa upande 
mwingine ndege za kutosha na jeshi la maji kubwa na imara lingemwezesha 
kumkabili adui kokote aliko bila umbali kuwa kikwazo.
Mara
 baada ya Hitler kuingia madarakani mwaka 1933, maandalizi ya Ujerumani 
kijeshi yalianza kufanyika, hivyo mkazo na mkakati wa muda mfupi ulikuwa
 kutengeneza silaha kwa ajili ya vita dhidi ya mataifa ya Magharibi na 
mkakati wa muda mrefu ulikuwa juu ya uzalishaji wa silaha nzito kwa 
ajili ya vita dhidi ya Marekani.
 Mnamo
 mwaka 1938 Hitler aliachana na mpango wa uvamizi wa kijeshi dhidi ya 
Czechoslovakia na kuangalia zaidi makubaliano ya amani na kiongozi wa 
nchi hiyo ambayo yalifanyika mjini Munich na hilo lilikuwa kosa lake 
baya na kubwa kuwahi kulifanya.
Alipoamua
 kuigeukia Ufaransa na Uingereza Hitler hakuweza kuishawishi Serikali ya
 Poland kujiunga na kuwa sehemu ya himaya ya Ujerumani kwa njia za amani
 ili kuhakikisha hali ya utulivu inakuwepo katika Mashariki ya Ulaya, 
hivyo alichukua maamuzi ya kuivamia na kuiharibu Poland kabla ya kuanza 
kuzikabili nchi za Magharibi.
Uvamizi
 wa nchi ya Poland ulikususudiwa kufanyika ifikapo Septemba 1, 1939 
lakini, ili kufanikisha adhma yake hiyo na ushindi wa haraka juu ya 
Poland kwa kuvunja kila aina ya kikwazo mbele yake, alikusudia kuiingiza
 Ujerumani katika makubaliano na Urusi ili mwisho wa siku iwe rahisi 
kwake kuzivamia nchi za Magharibi bila pingamizi lolote baada ya Poland.
Hali
 kadhalika, Hitler alikusudia kufanya uvamizi dhidi ya Mataifa ya 
Magharibi katika msimu wa baridi mwishoni mwa mwaka 1939, lakini hali 
mbaya ya hewa ilikuwa ni kikwazo kikubwa ambacho kingeathiri jeshi lake 
la anga, kwahiyo  aliamua kuhairisha mpango huo na kuhamishia uvamizi 
huo ifikapo mwanzoni mwa mwaka 1940 katika majira yajoto.
Kutokana
 na ushauri alioupata toka kwa Admiral Erich Raeder juu ya kuivamia na 
kuiteka Norway ili kuwezesha upatikanaji wa njia rahisi kwa jeshi lake 
la maji katika bahari ya Atlantiki kuelekea Kaskazini, aliivamia Norway 
mwaka Aprili 1940.
Baada
 ya kupokea ushauri tena toka kwa Kamanda Mkuu Erich Von Manstein lengo 
la uvamizi kuanzia Kaskazini lilibadilishwa na kuamua kupanga 
mashambulizi kuelekea nchi zilizoko Kusini mwa Ulaya kwa lengo la kuzuia
 misaada ya kijeshi toka jeshi la Washirika (Allied force) kuelekea nchi
 za Ubelgiji na Uholanzi.
Mkakati
 mpya wa Hitler kwa mara ya kwanza ulionekana kufanya kazi wakati jeshi 
la Ujerumani lilipofanikiwa kuvunja mstari wa ulinzi wa jeshi la 
Kifaransa na kufanikiwa ndani ya siku kumi kufika kwenye mkondo wa pwani
 nyuma ya vikosi vya majeshi ya Muungano.
Baada
 ya kuonekana wazi kuwa majeshi ya Washirika yaliyokwama yanaweza 
kutotoroka kipigo cha jeshi la Ujerumani, mwelekeo wa silaha na jeshi la
 Ujerumani ulibadilika tena, lakini jeshi hilo lilikwisha chelewa kuweza
 kuzuia na kufanya mashambulizi dhidi ya askari wa jeshi la Muungano 
kwasababu kikosi maalumu cha jeshi la Uingereza na wanajeshi wa Ufaransa
 walifanikiwa kuokolewa na kutoroka.
Pigo
 lililotokea mapema mwa mwezi Juni 1940 lililopelekea anguko kwa mstari 
wa mwisho wa ulinzi wa jeshi la Ufaransa ulikuwa ni ushindi kamili 
uliompa Hitler furaha na shangwe huku akijua anapata msaada wa kutosha 
toka kwa Makamanda na Majemedali wake wa kivita, ambao kila mara alikuwa
 akiwapandisha vyeo na kuwapa namna nyingine za rushwa kama sehemu ya 
kuwapa motisha ya kuendelea na mapambano.
Taarifa
 zinasema kuwa, kwasababu ilionekana kama vita hii ilikuwa imeisha baada
 ya Ujerumani kuiteka Ufaransa, Hitler alianza kupanga mipango mingine 
kwa ajili ya vita dhidi ya Marekani na Umoja wa Kisovieti.
Mnamo
 Julai 11, 1940 Hitler alitoa amri kuanza kwa ujenzi wa jeshi la maji 
ikiwemo ujenzi wa meli za kivita na ilipofika Julai 31, 1940 baada ya 
mkakati wa kutaka kuvamia Umoja wa Kisovieti katika msimu wa baridi wa 
1940, Hitler kutokana na ushauri wa wafanyakazi wake wa kijeshi aliamua 
kuishambulia Urusi katika majira ya joto mwishoni mwa mwaka1941.
Wakati
 Uingereza ikikataa kukubali kushindwa na kusalimu amri, Hitler alipanga
 kuchanganya hatua tatu ambazo zingehakikisha Uingereza inasalimu amri;-
 Kwanza kabisa, jeshi la anga la Ujerumani lingefanya uvamizi na 
kuharibu uwezo wa Uingereza kujitetea; Pili Uingereza ingevamiwa ardhini
 iwapo kama isingejisalimisha, na tatu ushindi ambao ungepatikana dhidi 
ya Urusi ungeondoa uwezekano wa Uingereza kupata msaada wowote ule toka 
Urusi, hivyo kuangamia zaidi na kumaliza hatari yoyote dhidi ya Japan, 
ambayo ingehamasika kusafiri katika bahari ya Pasifiki na kuivamia 
Marekani upande wa Magharibi.
Kwa 
upande mwingine Hitler alitaka Japan kujiunga katika vita na Uingereza 
na kuahidi kujiunga na Japan katika vita dhidi ya Marekani kama Tokyo 
ingeona umuhimu juu ya hilo, na hii ingekuwa njia nyingine kwa Ujerumani
 kupata kuimarisha jeshi la maji dhidi ya Marekani.
Kampeni
 dhidi ya eneo la Balkan, kiongozi huyo mbabe wa enzi hizo (Hitler) 
alikusudia kupata alicho amini kuwa ngome ya upande wa Kusini iliyokuwa 
katika hali tete lakini hata hivyo aliona operesheni kubwa ya jeshi la 
anga katika eneo la Balkani ingekuwa ya gharama ya juu sana kutokana na 
ugumu wa eneo lenyewe na hivyo kutokusudia kufanya operesheni kama hiyo 
tena.
Ikumbukwe
 kuwa, uvamizi wa Ujerumani dhidi ya Umoja wa Kisovieti, ulianza tarehe 
22 Juni, 1941 ambapo hapo mwanzo uvamizi huo ulionekana kwenda kama 
ilivyo pangwa, lakini gafla kila kitu kilianza kwenda vibaya  vipigo vya
 kwanza ambavyo vilikusudia kuangusha Umoja wa Kisovieti ndani ya wiki 
chache havikuleta matokeo yaliyokusudiwa na hayakuweza kuwa na athari 
katika nchi hiyo, hivyo baada ya hapo, swali daima lilikuwa kwa 
Ujerumani ni sekta ipi nyeti na muhimu ishambuliwe ili kuidhoofisha 
Urusi na sekta gani iachwe.
Katika
 hali hiyo, Hitler alijikuta  mara kwa mara akitofautiana na Majenerali 
wake walioko mstari wa mbele katika kuamua mustakabali wa vita na baada 
ya vita kuonekana ikiielemea na kuigeukia Ujerumani hali ya kutofautiana
 kati ya Makamanda wa Hitler ilizidi kuongezeka.
Wakati
 jeshi la Ujerumani likiendelea kurudi nyuma, Hitler alikuwa daima na 
wasiwasi kuhusu hasara waliyokuwa wakiendelea kuipata ya watu hali 
kadhalika ya uharibifu wa vifaa vyake vya kijeshi kwahiyo baadhi ya 
Majemadari kama Erwin Rommel na Walther Model, mara kwa mara walikuwa 
wanapingana na amri ya Hitler kwa kurudi nyuma wakati Majenerali wengine
 walikuwa wakirudishwa  nyumbani kukusanya kiinua mgongo chao cha kila 
mwezi na kustaafu kwa kutofautiana na amri za kiongozi wao ingawa 
wengine walikuwa wakiendelea na kazi zao.
Hitler
 alifikiri kwamba kushindwa kwa Ujerumani katika Vita Kuu ya Kwanza ya 
Dunia kulitokana na anguko lililotokea katika ardhi ya nyumbani mbele na
 kwa hivyo kudhani kuwa uanzishwaji wa sera za kidikteta na mauaji ya 
kukusudiwa ya Wayahudi ulikuwa uhakika wa ushindi wa vita dhidi ya 
majeshi washirika na safari hii Hitler alipoona hana jinsi na majeshi 
washirika yameshaingia mjini Berlin huku yakiongozwa na Jeshi Jekundu la
 Urusi, Hitler alijawa na hofu ya kisasi ambacho Warusi wangetoa dhidi 
ya Wajerumani, hivyo aliamua kumuoa mke wake na wote kwa pamoja kuamua 
kujiua muda mfupi kabla ya jeshi la Urusi kuwasili.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni