Mbunge
 wa jimbo la Mkuranga Mh. Abdallah Ulega akichangia Bajeti ya Serikai 
katika Mpango pili  wa wa miaka mitano ijayo wakati wa vikao vya bunge 
la bajeti linaloendelea mjini Dodoma hivi karibuni.
Mbunge wa jimbo la Mkuranga Mh. Abdallah Ulega akizindua kisima cha maji Mkamba katika jimbo lake  la Mkuranga mkoani Pwani. 
...................................................................................................................
SERIKALI
 ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imedhamiria 
kuwa Serikali ya mageuzi ya Viwanda ukilinganisha na zilizotangulia.
  Rais Dkt.Magufuli hata katika kampeni zake za uchaguzi 2015 
wakati akipita kuomba kura alisisitiza dhamira ya Serikali ya kujenga 
uchumi wa Viwanda.
 
 Wakati Serikali ikisisitiza kujenga uchumi wa Viwanda huku ikipata 
sapoti kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi wabunge nao katika kuunga 
mkono hilo kila mmoja amekuwa na kiu ya Jimbo lake kuwa la mfano katika 
eneo hilo.
 Abdallah Ulega ni Mbunge wa Jimbo la Mkuranga  lililopo Wilaya 
ya Mkuranga mkoani Pwani kwa upande wake tangu achaguliwe na wananchi 
wake ameonesha dhamira na kiu ya kutaka kuwakomboa wananchi wake Kwa 
kutaka jimbo hilo kuwa na viwanda. 
 
Anasema kuwa lazima wao kama wawakilishi wa wananchi Kwa maana 
ya wabunge wanaotokana na Chama cha Mapinduzi CCM wapokee Kwa mikono 
miwili mageuzi haya kwani wameahidi hivyo lazima watende.
  Ulega anasema kuwa Jimbo la Mkuranga ni kubwa na  linarutuba 
ya kutosha hivyo anakaribisha wawekezaji kuingia na kukubali Kuwekeza 
viwanda vidogovidogo na vikubwa katika kilimo hasa cha mazao mbalimbali 
 Kwa ajili ya maendeleo ya watu wake. 
 
Anasema kuwa kuna jitihada kama Mbunge amekuwa akizifanya za 
kuhakikisha kwamba jimbo lake ni miongoni mwa majimbo ambayo yanafaidika
 na mikakati ya Serikali ya kutaka mageuzi ya viwanda.
  "Kimsingi jimbo langu la Mkuranga ni kubwa kama nilivyosema na uzuri zaidi lina ardhi nzuri sana na ndiyo maana naomba wahisani na wawekezaji wa ndani kujitokeza kuja Kuwekeza na zaidi kijenga viwanda."anasema ulega
 Anasema kuwa kutokana na utajili wa Ardhi yenye rutuba wanaweza
 kujenga viwanda vya kusindika mazao lakini pia kwa sababu eneo lao ni 
kubwa basi hata viwanda vya kubangua korosho na kujengwa Kwa viwanda 
hivyo kutasaidia kuleta ajira katika eneo hilo.
  Anasisitiza kuwa  ndio maana wakati akichangia mpango wa wa 
maendeleo wa Serikali Kwa miaka mitano ameomba Serikali na wahisani 
kujitokeza Mkuranga lakini Kwa upande wa Serikali kuiweka Mkuranga kuwa 
sehemu yenye hitaji la ujenzi wa viwanda.
  Anasema amebainisha wazi kiu ya wananchi wa jimbo lake la 
kutaka maendeleo na ajira hivyo bila kuwepo na viwanda hakuna ajira 
inayoweza kuwepo na zaidi vijana watazidi kulaumu serikali yao. 
 
"Nimesema wazi kuwa Mkuranga kuna matatizo ya miundombinu 
mbalimbali ikiwamo barabara.Maji .kilimo na mambo mengine na katika 
baadhi ya maeneo haya nashukuru baadhi ya marafiki wameitikia mwito 
wangu na wameweza kusaidia katika kichimba visima ambapo wananchi wangu 
wameaza kupata Maji safi na salama."anasema Ulega 
 
Anasema kuwa anawashukuru African Foundation Reflection Kwa 
kuonesha moyo wa kusaidia na juhudi  hizo zote zimetokana na jitihada 
zake za kutaka kuona siku moja Mkuranga inakuwa ya kutolea mfano tofauti
 na ilivyo sasa. 
 
Aidha katika mpango huo wa maendeleo Kwa miaka mitano Kwa 
Serikali ameomba kujengewa barabara Kutoka Kisiju hadi Mkuranga Kwa 
kiwango cha lami kwani barabara hiyo ni muhimu Kwa wananchi wa wilaya 
hiyo lakini hata wale wanaotoka Mafia. 
 
Pia anasema katika mpango  mpango wa pili wa maendeleo wa miaka 
mitano Kuhusu maendeleo ya miundombinu nchini na hapo aliangalia  wilaya
 ya Mafia kwa sababu pale kuna bandari na watu wake pia ndiyo 
wazalishaji wakubwa wa korosho na samaki.
  Anasema kuwa  pia kwenye kata yake ya  mbezi kwaniaba ya 
wananchi wake wa Mkuranga wangeishauri Serikali kuwa  eneo la viwanda 
ili wananchi wake wawe sehemu ya uzalishaji wake. 
 
Aidha Ulega anazungumzia suala la kuondoa kero ya uhaba wa 
upatikani wa Maji katika jimbo hilo ambapo Serikali ingefanya bidii ya 
kutoa maji hayo kutoka katika mto rufiji kupitia kibiti hadi kufika 
Mkuranga na hatimaye Dar es Salaam.
  Anasema haiwezekani Kwa miaka nenda rudi tatizo la Maji 
halipatiwi ufumbuzi wakati Mkuranga inapitiwa kwa karibu  na Mto Rufiji 
ambapo mikakati madhubuti ya kuleta Maji ikifanyika tatizo hilo litabaki
 kuwa historia katika eneo hilo. 
 
Anasema tatizo la ajira Kwa vijana ni kubwa mno hivyo 
wanashukuru Serikali Kwa kutambua umuhimu wa kutilia mkazo uazishwaji na
 ufufuaji wa viwanda kwani eneo hilo ndilo linaweza kuwa.msaada Kwa 
vijana kuweza kupata ajira. 
 
"Mimi kama Mbunge wao kama nilivyosema awali nitaendelea 
kupambana na kufanya kila linalowezekana Kwa kuhakikisha Mkuranga 
inakuwa sehemu ya viwanda na naendelea kitoa rai Kwa wawekezaji 
kuchangamkia Ardhi yetu Kwa kujenga viwanda vingi ili vijana wangu 
wapate ajira."anasema 
 
Anaongeza kuwa mkuranga ilisahaulika mno pamoja kwamba ni 
miongoni mwa wilaya za siku nyingi lakini imekuwa nyuma kimaendeleo 
hivyo niwakati mwafaka wa kushirikiana Kwa pamoja Kwa ajili ya 
maendeleo.
  Anasema kuwa wananchi wake waendelee kumuombea Kwa Mungu na 
wazidi kudumisha Umoja na mshikamano ili Kwa pamoja wapambane Kwa lengo 
la kuona jimbo la mkuranga linakuwa la mfano.
 Akizungumzia kilimo cha korosho anasema kuwa pamoja na zao hilo
 kuwa ndio zao linalotegemewa kuendesha maisha ya wananchi wake lakini 
bado kwasababu ya ukosefu wa kuwepo Kwa viwanda hususani vya ubanguaji 
kunafanya pasiwepo na tija sana wanayoipata wananchi wake katika kilimo 
hicho.
  Anasema kuwa kutokana na hali hiyo ana kazi kubwa ya kuendelea
 kuzungumza na watu mbalimbali ili kuleta ushawishi wa kukubali Kuwekeza
 kwenye ujenzi wa viwanda hivyo. 
 
Pia akizungumzia Elimu anasema  anatambua changamoto zilizopo 
katika eneo hilo hivyo amedhamiria Kwa dhati Kwa kushirikiana na 
Halmashauri wanaongeza hamasa Kwa wanafunzi ili waweze kufanya vema 
katika masomo yao na hatimaye kuweza kupata wataalamu wa baadae. 
 
"Najua kuna Changamoto ya madawati na hili tunalishugulikia Kwa 
kushirikiana na kamati mbalimbali za Shule,wazazi,pamoja na walimu ili 
kuona namna ya kukabiliana na tatizo hilo na hata uchakavu wa majengo 
."anasema Ulega.
  Anahitimisha Kwa kuwataka wananchi wa Mkuranga kila mmoja 
kujielekeza katika kuzalisha Mali huku wakienda na Kauli mbiu ya Rais 
Dkt.Magufuli ya Hapa Kazi Tu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni