Spika
 wa Bunge Mhe. Job Ndugai akilihutubia Bunge la Afrika (Pan African 
Parliament) kuwasilisha Ujumbe wa Mshikamano kwa wabunge wa Bunge hilo  
wakati wa Ufunguzi wa rasmi wa Mkutano wa Pili wa Bunge hilo uliofanyika
 Mjini Midrand Afrika Kusini. Mhe. Ndugai alikuwa miongoni mwa viongozi 
mashuhuri 12 kutoka Barani Afrika walioalikwa kutoa ujumbe  huo kwa 
wabunge wa Afrika. 
Spika
 wa Bunge Mhe. Job Ndugai akilihutubia Bunge la Afrika (Pan African 
Parliament) kuwasilisha Ujumbe wa Mshikamano kwa wabunge wa Bunge hilo  
wakati wa Ufunguzi wa rasmi wa Mkutano wa Pili wa Bunge hilo uliofanyika
 Mjini Midrand Afrika Kusini. Mhe. Ndugai alikuwa miongoni mwa viongozi 
mashuhuri 12 kutoka Barani Afrika walioalikwa kutoa ujumbe  huo kwa 
wabunge wa Afrika. 
Spika
 wa Mhe. Job Ndugai akiwa na baadhi ya Maspika wenzie kutoka mabunge ya 
Nchi za Bara la Afrika  kwenye Mkutano wa Bunge la Afrika (Pan African 
Parliament) alikoalikwa kuwasilisha Ujumbe wa Mshikamano kwa wabunge wa 
Bunge hilo  wakati wa Ufunguzi wa rasmi wa Mkutano wa Pili wa Bunge hilo
 uliofanyika Mjini Midrand Afrika Kusini. Mhe. Ndugai alikuwa miongoni 
mwa viongozi mashuhuri 12 kutoka Barani Afrika walioalikwa kutoa ujumbe 
 huo kwa wabunge wa Afrika. Kulia kwake ni Spika wa Bunge la Seneta la 
Lesotho Mhe Seeiso Berenge Seeiso na kushoto ni senate kutoka Bunge la 
Afrika Mhe. Bennette hayatoe 
Wabunge
 wa Bunge la Afrika wanaowakilisha Tanzania wakila kiapa cha uaminifu. 
Kutoka kushoto ni Mhe. Asha Abdalah Juma, Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile, 
Mhe. David Silinde na Mhe. Mboni Mhita. 
                                                        Na Owen Mwandumbya, Midrand Afrika Kusini. 
 Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Job Ndugai amesema ili Bara la afrika 
liweze kuwa Bara lenye nguvu kiuchumi na sauti ya maamuzi duniani halina
 budi kujikita katika umoja na mshikamono. 
 Mhe. Ndugai 
aliyasema hayo alipokuwa akilihutubia Bunge la Afrika (Pan African 
Parliament) leo kuwasilisha Ujumbe wa Mshikamano kwa wabunge wa Bunge 
hilo  wakati wa Ufunguzi wa rasmi wa Mkutano wa Pili wa Bunge hilo 
uliofanyika Mjini Midrand Afrika Kusini. 
 Akizungumzia 
changamoto zinazolikabli bara la Afrika Mhe. Nduagi alisema nchi nyingi 
barani Afrika zinakabiliwa na matatizo yanayolingana ambayo ni Vita vya 
wenyewe kwa wenyewe, ugaidi, umasikini na mengineyo ambayo yanahitaji 
suluhisho la Pamoja kuyakabili.. 
 “ katika duniani ya sasa ni 
vyema tukakabiliana na changamoto zinazotukabili kwa pamoja. Matajiri 
hawawezi kuepuka athari za umasikini na ukosefu wa amani. Kinachotokea 
eneo moja kinaathiri maeneno mengi mathalani vita vya wenyewe kwa 
wenyewe Somalia imesababisha wakimbizi katika maeneo mengi duniani” 
alisema Ndugai 
 Akizungumzia nafasi ya wabunge katika kupiga 
vita changamoto zinazolikabili bara la Afrika, Mhe. Ndugai amesema 
wabunge wa Bunge la Afrika kama wawakilishi wa Manbunge ya Nchi 
wanachama wa Umoja wa Afrika wanawajibu wa kutetea maslahi ya Bara la 
Afrika bila kujali itikadi za kisiasa, maeneo wanayotoka na mambo 
mengine yanayoweza kuligawa bara la Afrika. 
 “ Mkiwa Wabunge 
mnaowakilisha nchi zenu katika Bunge hili, nilazima mhakikishe Umoja wa 
Afrika unasimamia ipasavyo masalahi ya bara la Afrika ili kutimiza ndoto
 waliokuwa nayo waasisi wa umoja huu wa Afrika. Kwa mfano baba wa Taifa 
la Tanzania Mwalimu Julius kambarage Nyerere alisema lazima tukimbie 
wakati wengine wakitembea” aliongeza Ndugai 
 Mapema akitoa 
salamu za Bunge la Lesotho, Spika wa Bunge la Nchi hiyo Mhe.  Nthloi 
Motsamai alisifu juhudi za Mwalimu Julius Nyerere pamoja na waasisi 
wengine wa bara hili katika kuimarisha umoja wa Afrika na kuwataka 
wabunge wa Bunge la afrika kuhakikisha mawazo ya viongozi hawa ya 
kulifanya bara la afrika kuwa moja yanatimia. 
 Katika hatua 
nyingine, wabunge wa Tanzania wanaowakilisha Tanzania katika Bunge la 
Afrika walikula kiapo cha uaminifu kuwa wabunge wa Bunge hilo baada ya 
Bunge la Tanzania kuwachagua mapema mwezi Januari. 
 Wabunge hao 
ni pamoja na Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile, Mhe. Mboni Mhita, Mhe. David 
Silinde na Mhe. Asha Abdalah Juma. Mhe. Ndugai anatarajia kurejea nchini
 kesho jumatano ambapo Bunge la Afrika linaendelea na Vikao vyake hadi 
tarehe 13 Mei, 2016. 
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni