MLIPUKO WAUWA AFISA POLISI MMOJA NA KUJERUHI WENGINE 19 NCHINI UTURUKI

Afisa polisi mmoja ameuwawa kwa mlipuko uliokuwa ndani ya gari karibu na Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kusini mashariki mwa mji wa Gaziantep nchini Uturuki.

Maafisa polisi 19 na raia wanne wameripotiwa kujeruhiwa na mlipuko huo uliotokea leo asubuhi.

Uturuki imekuwa ikikumbwa na matukio ya mfululizo ya milipuko tangu mwaka uliopita, inayofanywa na wapiganaji wa Kikurdi na Dola ya Kiislam (IS).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni