HALI KATIKA HOSPITALI ZA VENEZUELA INATISHA

Kudorora kwa uchumi wa Venezuela kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta, kumeiathiri sekta ya afya ambapo hospitali sasa hazina umeme, dawa, vitanda na hata sabuni ambapo hali ni mbaya mno.

Hospitali za Venezuela pia zinamazingira machafu, wagonjwa wenye kutokwa damu wakiwa wametelekezwa na damu zao kuchuruzika kwenye sakafu za hospitali, madaktari nao wanalazimika kufanya upasuaji bila vifaa.

Hali hiyo imebainika huku rais wa Venezuela, Nicolas Maduro, akidai kuwa nchi yake hiyo inahuduma bora za tiba duniani ikiwa nyuma baada ya taifa la Cuba, jambo ambalo ni tofauti na uhalisia.
Wagonjwa waliovunjika miguu wakipatiwa matibabu kwa kutumia madumu ya maji badala ya vyuma vizito
Mama akiwa na mtoto wake mwenye tatizo la pumu akimpatia msaada wa kumshikilia kifaa cha oxygen
Mgonjwa aliyeumia vibaya sehemu ya kichwa akiwa hospitali akingojea kwa mwaka mzima kufanyiwa upasuaji

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni