WATOTO MAPACHA WALIOUNGANA MWILI WAFARIKI DUNIA MJINI MOMBASA

Watoto mapacha walioungana mwili waliozaliwa hospitali ya rufaa ya Pwani mjini Mombasa nchini Kenya wamefariki dunia leo alfajiri.

Watoto hao walizaliwa Alhamisi na walikuwa wasafirishwe kwa ndege kwenda Hospitali ya Taifa ya Kenyatta kwa matibabu maalum wamefariki wakiwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi.

Akithibitisha vifo vya mapacha hao Mtendaji Mkuu CPGH Dk. Iqbal Khandwalla ameviambia vyombo vya habari vya Kenya kwamba jitihada za madaktari za kuokoa maisha ya watoto hao zimeshindikana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni