MTU ALIYETAKA KUJIUWA KWA KULIWA NA SIMBA AOKOLEWA

Mwanaume aliyevua nguo zote na kisha kujirushwa kwenye chumba cha simba nchini Chile kwa lengo la kujiuwa amenusurika kifo, lakini ni baada ya simba hao kuuwawa.

Mamlaka za Jiji la Santiago zimethibitisha kutokea kwa tuko hilo ambapo simba wawili waliuwawa wakati wakimg'ata mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 20 siku ya jana.

Mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina la Franco Luiss Ferrada Roman alikimbizwa hospitali iliyopo karibu kwa matibabu na hali yaki inasemekana ni mbaya.
                     Simba wakimg'ata mtu huyo aliyetumbukiwa kwenye chumba chao
Mwanaume aliyejitumbukiza kwenye chumba cha simba akiwa amemkumbatia kwa mikono na miguu simba dume aliyekuwa akimng'ata shingoni

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni