Kaimu
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo Alex Nkenyenge akimuelezea jambo Mkuu wa Mkoa wa Dar es
 Salaam Paul Makonda wakati wa hafla ya uzinduzi wa mashindano ya mbio 
za magari za Alliance Auto MMSC Rally Mzunguko wa Pili jana jijini Dar 
es Salaam. Ambapo zaidi ya  magari 15 yanashiriki katika viwanja vya 
vilivyopo wilayani Bagamoyo.
Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akisikililiza kwa makini maelezo 
kuhusu mbio za magari za Alliance Auto MMSC Rally kutoka kwa Mratibu wa 
mashindano hayo ambaye pi ni Mwenyekiti wa Mzizima Motors Sports Club 
Bi. Hidaya Kamaga (katikati) jana jijini Dar es Salaam. Aliyesimamani ni
 mshiriki wa mashindano hayo kutoka Timu ya Puma Energy Bw. Dharam 
Pandya.
Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akiangalia moja ya magari 
yanayotumika katika mbio za magari za Alliance Auto MMSC Rally jana 
jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya 
Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Alex 
Nkenyenge.
Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akiruhusu gari ambalo 
linawakilisha timu ya wasanii wa Bongo Movie kuanza safari ya kuelekea 
Bagamoyo mkoani Pwani tayari kwa mashindano ya Alliance Auto MMSC Rally 
jana jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo 
ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Alex 
Nkenyenge na Katibu wa Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo.Timu hiyo ya 
Bongo movie imeshiriki katika mbio hizo kwa lengo la kuhamasisha 
uanzishwaji wa Mfuko wa Filamu Tanzania.
Mmoja
 wa washiriki wa mbashindano ya mbio za magari za Alliance Auto MMSC 
Rally kutoka Timu ya Hari Singh ya Moshi Kilimanjaro Bw.Gujrit Dhani 
akielezea jambo mara baada ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ya 
mashindano hayo jana wilayani Bagamoyo.
 
 
Baadhi ya magari yakiwa katika mashindano ya Alliance Auto MMSC Rally yanayofikia tamati leo mjini Bagamoyo.
Baadhi ya magari yakiwa katika mashindano ya Alliance Auto MMSC Rally yanayofikia tamati leo mjini Bagamoyo.
Baadhi
 ya mashabiki wa mchezo wa mbio za magari wakifuatilia mbio za Alliance 
Auto MMSC Rally mzungoko wa Pili jana wilayani Bagamoyo.
Baadhi
 ya watazamaji wa mbio za magari wakirejea makwao mara baada ya 
kumalizika kwa awamu ya kwanza ya mbio za magari za Alliance Auto MMSC 
Rally jana wilayani Bagamoyo. Picha na Frank Shija, WHUSM.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni