Dk. Pallangyo awakaribisha wazawa kwenye uzalishaji wa umeme

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati Dk. Juliana Pallangyo (pichani) akifungua mkutano unaoshirikisha wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme.
 Sehemu ya watendaji na wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, wakifuatilia hotuba iliyokuwa inatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (hayupo pichani).
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (kulia) na  Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la  Umeme Nchini (TANESCO) Mhandisi Decklan Mhaiki (kushoto) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na mwenyekiti wa kamati ya nchi za kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya  umeme, Josh Chifamba (hayupo pichani)
 Mwenyekiti wa kamati ya nchi za kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, Josh Chifamba (kulia) akimkabidhi zawadi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (kushoto) aliyekuwa mgeni  rasmi kwenye ufunguzi wa mkutano huo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (aliyekaa mbele katikati) akiwa  katika picha  ya  pamoja na sehemu ya  watendaji na wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, mara baada ya  ufunguzi wa mkutano huo.

Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati, Dk Jualiana  Pallangyo amewataka wawekezaji binafsi nchini kujitokeza kwa wingi na kuwekeza katika uzalishaji na uuzaji wa nishati ya umeme  nchini ili  iweze kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi.
Dk. Pallangyo alisema hayo kwenye mkutano unaokutanisha wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme. Nchi hizo ni pamoja na  Bostwana, Msumbiji, Afrika ya Kusini, Lesotho, Namibia, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Swaziland, Zambia na Zimbabwe. Lengo la mkutano huo wa siku moja lilikuwa ni kujadili changamoto zinazozikumba nchi wanachama katika uzalishaji  na uuzaji  wa umeme ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu.
Aliongeza kuwa  wawekezaji binafsi wanaweza kuzalisha   umeme kupitia  vyanzo mbalimbali vya nishati ikiwa ni pamoja na maporomoko madogo ya maji, upepo, bayomasi na  jua kutokana na uwezo wao.
Akielezea fursa za uwekezaji nchini, Dk. Pallangyo alisema kuwa wawekezaji wanaweza kuwekeza  kupitia ujenzi wa miundombinu ya usambazaji  wa umeme, uendelezaji wa miradi ya umeme unaotokana na maporomoko madogo ya maji na  vyanzo  vingine  ikiwa ni pamoja na jotoardhi, upepo na uanzishwaji wa viwanda vidogo kwa ajili ya utengenezaji wa vifaa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umeme.
Dk. Pallangyo aliongeza kuwa ushiriki wa  sekta binafsi  katika sekta ya umeme umeongezeka kila mwaka na kusisitiza kuwa serikali bado inaendelea na mikakati ya kuwawezesha wawekezaji binafsi  katika  uzalishaji ya umeme nchini.
Aliongeza kuwa serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji nchini  ikiwa ni pamoja na sera na sheria mbalimbali  zinazotumika kama mwongozo na kutaja kuwa ni pamoja na sheria ya umeme ya mwaka  2008, sera ya nishati ya mwaka 2003 ambayo inahamasisha ushiriki wa sekta binafsi katika sekta ya umeme.
Alitaja sheria nyingine kuwa ni pamoja na ile ya Mamlaka ya Udhibiti  wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ya mwaka 2001, sheria ya  Wakala wa Nishaji  Vijijini (REA) ya mwaka 2005.
Akielezea mikakati ya serikali katika upatikanaji wa nishati ya  uhakika, Dk. Pallangyo alisema kuwa serikali imeweka mkakati wa  kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025 asilimia 75 ya wananchi wote hasa waishio  vijijini wanapata nishati ya umeme ambayo ni ya uhakika.
“Tunatarajia kuzalisha hadi   megawati 10,000 za umeme ambao utachochea ukuaji wa uchumi wa nchi kupitia viwanda na hivyo nchi kutoka katika kundi la nchi masikini duniani na kuwa  katika kundi la nchi zenye kipato cha kati  duniani,” alisisitiza Dk. Pallangyo.
Akielezea hali ya upatikanaji wa umeme nchini, Dk. Pallangyo alisema kuwa umeme unaozalishwa ni megawati 1461.69 huku mahitaji halisi yakiwa ni megawati 1026.
Umoja wa  nchi zinazoshirikiana katika sekta ya umeme kusini mwa Afrika (Southern African Power Pool; SAPP) ulianzishwa Agosti mwaka 1995 katika Mkutano wa  Umoja wa Nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la  Sahara (SADC) ambapo walisaini makubaliano kwa ajili ya  kushirikiana katika uzalishaji na biashara ya  umeme wa pamoja.

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA INTANETI, AfPIF 2016

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba akielezea matumizi ya intaneti yalivyo nchini na changamoto zinazowakabili watumiaji wa huduma hiyo. 

Mwaka 2016 unakuwa mwaka wa neema kwa Tanzania kupata fursa ya kuandaa Mkutano unaowakutanisha wadau wa intaneti (African Peering and Interconnection Forum), mkutano unaotaraji kufanyika Agosti 31 – Septemba 1, jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia mkutano huo, Meneja Mwandamizi wa Maendeleo wa Taasisi ya Internet Society, Michuki Mwangi amesema mkutano huo unalengo wa kukutanisha wadau mbalimbali wa intaneti ili kutanua miondombinu ya intaneti katika bara la Afrika.
Amesema taasisi yake inapenda kuona huduma ya intaneti ikipatikana kwa urahisi kwa watumiaji wake Afrika na hivyo kupitia mkutano huo wataweza kutazama jinsi gani wanaweza kushirikiana na kubadilishana takwimu za watumiaji wa mitandao kwa bara zima la Afrika.
“Tunatambua kuwa watumiaji wa intaneti wanazidi kuongezeka na kupitia mkutano huu tutaweza kuangalia jinsi gani tunaboresha huduma ya intaneti iwe bora ili iweze kutumiwa na watu wengi zaidi,” amesema Mwangi.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba amesema mkutano huo una umuhimu kwa Watanzania kwa kupata fursa ya kujifunza na kubadilishana mawazo na watu kutoka mataifa mengine katika huduma ya intaneti.
Amesema kwa sasa Tanzania bado ina changamoto nyingi katika huduma ya intaneti na kupata nafasi hiyo ya kuandaa mkutano kutakuwa na faida kwa mashirika yanayotoa huduma ya intaneti ili kuwawezesha kutambua ni jinsi gani wataboresha huduma kwa wateja.
“Nchi yetu inawatumiaji wengi wa intaneti ila bado kuna changamoto nyingi ikiwepo usalama wa mtandao na serikali inafanya jitihada nyingi kumaliza changamoto hizo na kupitia mkutano huu tunaamini utasaidia zaidi Watanzania kupata kitu kipya katika huduma ya intaneti,” amesema Simba.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary amesema Watanzania wengi bado hawajafahamu umuhimu wa intaneti kutokana na kutokuwa na ujuzi wa kutosha kuhusu intaneti lakini kupitia mkutano huo ulioandaliwa na Internet Society wataweza kuapata elimu mpya kuhusu intaneti.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba (kushoto) akizungumza jambo na Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary.
Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba (kushoto), Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary, Meneja Mradi wa Tanzania Internet Exchange (TIX), Frank Habicht na Meneja Mwandamizi wa Maendeleo wa Taasisi ya Internet Society, Michuki Mwangi wakizungumza jambo kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary akifungua mkutano huo.
Meneja Mwandamizi wa Maendeleo wa Taasisi ya Internet Society, Michuki Mwangi akizungumzia mkutano wa Intaneti, AfPIF utakaofanyika nchini, Agosti, 30 - Septemba, 1
Baadhi ya washiriki waliohudhuria mkutano huo.
Baadhi ya waandishi waliohudhuria mkutano huo.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.

THE BEAT FESTIVAL @ SLIPWAY MSASANI DAR ES SALAAM THIS FRIDAY


FRIDAY 01. April - 21.00 - 02.00 
Venue: Paparazzi Club, Slipway - Msasani Bay, Dar es Salaam
Entrance: 10.000 TSH only
  SIKINDE – Dance orchestra / Tanzanian rumba

Formerly known as DDC Mlimani Park Orchestra, Sikinde is one of the greatest Tanzanian dance bands of all time. Although the group was first formed in 1978 they embody the sound of independence, which took place in Tanzania in 1961, since the founding members came from the pre independence groups Dar es Salaam Jazz Band and the workers union band Ottu Jazz Band. While many of the older orchestras in Tanzania have lost or replaced many of their founding members, Sikinde is perhaps the oldest orchestra who still have most their founding members in their group. Don't miss this opportunity to see one of Tanzanias greatest orchestras performing classic Tanzanian rumba lead by the charismatic lead singer Hassan Bichuka.
MOPOA JAZZ TRIO – Afro Jazz
This trio is lead by Jazz guitarist Emmanual Abraham Mopao who is steadily becoming one of the authorities on the Dar es Salaam Jazz scene. Towards the end of last year he released his first solo album and toured with his trio project as the opening act for the Mzungu Kichaa tour in Germany and Denmark. He is a self taught and hard working musician, inspired by African Jazz stars such as Jimmy Dludlu and Hugh Masekela as well as the American Jazz standard traditions. His performance is based on improvisation and is a rare treat for Dar es Salaam Jazz enthusiasts.
KIFIMBO – Afrofusion / Reggae
Kifimbo is a reggae-afrofusion artist from Dar es Salaam who is respected on the Tanzanian reggae scene for his high energy on stage. His up-tempo songs never seize to put his audience in a good mood. He is based in Bagamoyo where he does different farming activities when he isn’t doing music. He performed his first performance at THE BEAT last year and surprised us all with his high-energy performance. We look forward to welcoming him back to THE BEAT!
BLACK FIT – Reggae / Dancehall
Hussein Badru Hussein, whose artist name is Black Fit, started his musical career in 1995 while he was still a “street boy”. He gained experience through participating in Street festivals and managed to record his first album “Harakati za Mweusi” in 2014. In 2007, he participated in one of the biggest Festivals of that time, held at the “Makumbusho Village Museum, “YA KALE YANAPOKUTANA NA YA SASA FESTIVAL”, and won 3rd prize which boosted his name on the scene. In 2009 he won the first prize during the same festival. Flack Fit has been studying at Music Mayday with an EU scholarship, perfecting his skills in both performance and self management through their 2 year music program. 
ABOUT THE BEAT: The Beat is a monthly festival showcasing the best live music from Tanzania and abroad. The festival is powered by: Caravan Records, Paparazzi Bistro Club, Jameson, and Goethe Institut Tanzania. Info: CRTanzania@gmail.com web:www.facebook.com/TheBeatFestival

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU YAVUTIWA NA UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBONI




Barabara za kuingia na kutoka katika Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam zinavyoonekana, wakati Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu walipotembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo ambalo limekamilika kwa asilimia 99.9 na litaanza kutumika rasmi kuanzia Aprili 16.
Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara (kulia) akibadilishana mawazo na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu na Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka wakati Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipotembelea dalaja hilo.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka wakati Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipotembelea dalaja hilo.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakikagua ujenzi wa daraja la Kigamboni.


Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka akiwaonyesha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu barabara zinazoingia katika daraja hilo, wakati walipofanya ziara ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wake jijini Dar es Salaam.
Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka akifafanua jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara.
Ufafanuzi kwa Wabunge.
Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu jijini Dar es Salaam jana, walipotembelea kuangalia ujenzi wa daraja hilo linalotarajiwa kuzinduliwa Aprili 16. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Prof. Norman Sigala na kulia ni Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi wa NSSF, Yacoub Kidula.
Muonekano wa barabara za kuingia katika daraja la Kigamboni.
Darala la Kigamboni linavyonekana baada ya kukamilika kwa asilimia 99.9.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga akifafanua jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Prof. Norman Sigala.
Wabunge wa Kamati hiyo wakipata ufafanuzi kutoka kwa Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka.

Wakandarasi wasiolipa mishahara, madeni kutopewa kipaumbele REA III.

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika moja ya kikao na wakandarasi wanaosambaza  Umeme Vijijini vilivyoanza tarehe 29 Machi na kumalizika tarehe 31 mwezi huu.Wa Tatu kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Lutengano Mwakahesya na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Ufundi kutoka REA, Mhandisi Bengie Msofe. Wengine ni watendaji kutoka kampuni ya Angelique International inayosambaza umeme mkoani Arusha, Wizara na REA.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika kikao na kampuni  ya Engineering & Construction inayosambaza umeme vijijini mkoani Kagera katika wilaya za Ngara, Biharamulo, Misenyi, Karagwe, Kyerwa, Bukoba vijijini na Muleba kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Lutengano Mwakahesya na anayemfuatia ni Meneja wa Tanesco Kanda ya Ziwa, Mhandisi Amos Maganga.Wengine ni watendaji kutoka kampuni hiyo, Wizara na REA.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (wa kwanza kushoto), Meneja wa Tanesco Kanda ya Ziwa, Mhandisi Amos Maganga (wa pili kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Lutengano Mwakahesya (wa Tatu kushoto) wakiwa katika moja ya vikao vilivyojumuisha wakandarasi wanaosambaza umeme vijijini vilivyoanza tarehe 29  Machi na kumalizika tarehe 31 Machi, mwaka huu.
Na Teresia Mhagama
Imeelezwa kuwa wakandarasi wenye tuhuma za kutolipa mishahara wafanyakazi wao, kuomba rushwa  kwa wateja wanaotaka kuunganishiwa umeme na kutolipa fedha za watoa huduma waliokuwa wakifanya nao kazi katika usambazaji  umeme vijijini Awamu ya Pili, hawatapewa kazi husika katika miradi ya REA Awamu ya Tatu.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na kampuni mbalimbali zinazotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini Awamu ya Pili inayotarajiwa kukamilika mwezi Juni mwaka huu.
“Kampuni zitakazopewa kipaumbele ni zile zilizofanya vizuri katika miradi ya REA Awamu ya Pili na kuonekana kuleta ushindani kwa kampuni nyingine za ndani na nje ya nchi kwa kufanya kazi waliyopewa kwa bidii na kutokuwa na tuhuma mbalimbali ikiwemo rushwa,” alisema Profesa Muhongo.
Awali Meneja Operesheni wa  kampuni ya Engineering & Construction, Julius Kateti  inayosambaza umeme vijijini mkoani Kagera katika wilaya za Ngara, Biharamulo, Misenyi, Karagwe, Kyerwa, Bukoba vijijini na Muleba alimweleza Profesa Muhongo kuwa kazi ya usambazaji umeme katika mkoa huo imehusisha vijiji 451 na wanatarajia kuunganisha wateja 30,000 kabla ya muda wa ukomo uliowekwa na Serikali.
Alisema kuwa katika wilaya za Ngara na Biharamulo jumla ya wateja 4385 wa njia moja ya umeme waliunganishwa kati ya wateja 4554 na wateja 49 wa njia tatu za umeme waliunganishwa ambapo jumla ya transfoma 47 zilifungwa na kwamba kwa wilaya za  Ngara na Biharamulo wanatarajia kukamilisha kazi hiyo ifikapo Aprili 20 mwaka huu na kuukabidhi mradi huo kwa Shirika la Umeme Tanzania  (TANESCO).
Aidha alisema kuwa katika wilaya ya  Karagwe jumla ya transfoma 82 zilifungwa na wateja wa njia moja ya umeme wapatao 3507 waliunganishwa kati ya wateja 5480 na wateja 95 wa njia tatu ya umeme wameunganishwa ambapo wanatarajia kukamilisha kazi mwezi Mei mwaka huu.
“Mheshimiwa Waziri,  kwa upande wa wilaya ya Kyerwa tumeshafunga transfoma 63 ambapo lengo la awali lilikuwa ni kufunga transfoma 53, na kwa wilaya hii wateja 2044 wa njia moja ya umeme wameunganishiwa umeme kati ya wateja 3228 na wateja 30 wa njia tatu za umeme waliunganishwa na tunatarajia kuendelea kuunganisha wateja hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu,” alisema Kateti.
Vilevile alisema kuwa  katika wilaya ya Misenyi jumla ya transfoma 52 zimefungwa ambapo wateja 1345 wa njia moja waliunganishwa  kati ya wateja 4308 na wateja waliounganishwa kwa njia tatu za umeme ni 17 huku wakitarajia kukamilisha kazi mwezi Juni mwaka huu.
Aliongeza kuwa kwa upande wa wilaya za Muleba na Bukoba Vijijini jumla ya transfoma 118 zimefungwa  ambapo wateja 5649 wa njia moja ya umeme waliunganishwa na huduma hiyo kati ya wateja 12,703 huku wateja waliounganishwa katika njia tatu za umeme wakifikia 22 na wanatarajia kukamilisha kazi mwezi Mei mwaka huu.
Kwa upande wa  kampuni ya JV State Grid, Meneja Mradi wa kampuni hiyo Mhandisi  A. Mwaipaja alisema kuwa kampuni hiyo inasambaza umeme vijijini katika wilaya za Rungwe, Kyela na  Ileje mkoani Mbeya ambapo kazi ya  kusambaza umeme katika wilaya hizo  imekamilika kwa asilimi 92 hadi kufikia katikati mwa mwezi Machi mwaka huu na wateja wapya 2,244 wameunganishwa katika vijiji 65 na kufunga transfoma 90 kati ya 133 wanazopaswa kufunga.
Aidha katika wilaya ya Mbarali mkoani humo, JV State imeshakamilisha kazi kwa asilimia 92  hadi kufikia tarehe 15 Machi, 2016 ambapo wateja wapya 1724 kati ya 4505 katika vijiji 27 wameunganishwa na transfoma 35 kati ya 56 zimefungwa.
Alisema kuwa  kampuni hiyo pia inafanya kazi ya kusambaza umeme vijijini katika mkoa wa Kigoma katika wilaya Sita za  Kigoma Vijijini,  Buhigwe, Kasulu, Kibondo, Kakonko na Uvinza ambapo kazi imekamilika kwa asilimia 93 hadi kufikia Machi 2016 na jumla ya vijiji 63 na wateja  2,647 kati ya 8773 wameunganishwa na umeme katika wilaya hizo.  
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Nishati, Wizara ya Nishati na Madini,  Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo aliwataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini kujiepusha na masuala ya rushwa katika utekelezaji wa miradi hiyo hasa katika zoezi la  uunganishaji umeme kwa wateja.

SERIKALI KUSAIDIANA NA TAASISI YA MILLEN MAGESE MAPAMBANO DHIDI YA TATIZO LA ENDOMETRIOSIS

DSC_8548
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akitoa hotuba yake katika semina hiyo. Kushoto ni Mwasisi wa Taasisi ya Millen Magese, Millen Happiness Magese. (Picha na Video na Andrew Chale,Modewjiblog).
DSC_8330
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Mwanadada, Millen Happiness Magese (katikati) pamoja na Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Bw. Rogers Shemwelekwa.
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imesema kuwa ipo tayari kushirikiana na wadau mbalimbali akiwemo Mwanadada Millen Magese na Taasisi yake katika mapambano ya ugonjwa na athari za Endometriosis ambao unawapata wanawake wengi hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa mapema leo Machi 30.2016 na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati wa kufungua rasmi semina maalum kwa vijana wapatao 500 wa shule za Sekondari zikiwemo za Turiani Sekondari,Makurumla na zinginezo za Manispaa ya Kinondoni pamoja na walezi na walimu, ambapo katika mkutano huo, Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, juhudi zinazofanywa na Mwanadada Millen Magese ni za kuungwa mkono hivyo wataendelea kushirikiana naye bega kwa bega.
Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, anatambua wanawake wengi duniani kote wanasumbuliwa na tatizo hilo ambapo gharama zake kwa kawaida ni kubwa huku bado wataalam wanaendelea kushughulikia namna ya upatikanaji wa tiba yake ili kuweza kuwa nafuu.
“Napongeza juhudi za dhati zinazofanywa na taasisi ya Millen Magese, katika kuunga mkono juhudi za serikali ya tano kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto za kuwasogeza wananchi karibu na huduma bora kwa ajili ya Maendeleo na Ustawi wa Jamii yetu.
Tatizo la kutoshika mimba (kitaalamu Endomytiosis) hutokana na sababu mbalimbali, nyingi zikichangiwa na uelewa mdogo wa jamii inayomzunguka msichana au mama anayejianadaa kuanza kubeba mimba, lakini pia upungufu wa vifaa tiba hospitalini na kwenye vituo vya afya sambamba na kukosekana kwa wataalamu katika hospitali zetu, Hivyo tunapenda kuchukua fursa hii kupongeza juhudi kama hizi za kuandaa semina na warsha ikiwa ni hatua madhubuti na ya msingi katika kuikabiliana na changamoto ya uelewa wa tatizo hili katika jamii.
Kwani, tunaamini, limekuwa jambo la faraja sana, tangu Magesse alipojitokeza hadharani na kuihabarisha dunia juu ya tatizo hili linalomkabili yeye binafsi. Naomba kusema wazi kuwa, huo ulikuwa uthubutu wa pekee wa mrembo huyo, kiasi cha kuifanya jamii kubwa ya kimataifa kuanza kulifuatilia tatizo hili ili kusaidia mabinti wadogo ambao walikuwa hawajakumbwa na hali hiyo. “ alieleza Naibu Waziri Dk. Kigwangalla katika hotuba yake hiyo.
Aidha, Dk. Kigwangalla aliongeza kuwa, ni faraja kubwa kwa watanzania tangu Magese Foundation ilipoanzishwa ikifanya kazi kubwa ya kuhamasisha upatikanaji wa vifaa na pia ujenzi wa hospitali maalumu kwa ajili ya kutibu tatizo hilo. Jambo hilo linaendelea kuitia moyo serikali hususani Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kufikia lengo la kumuwezesha mtoto wa kike kufikia malengo tarajiwa.
Kwa upande wake, Mwanadada Millen Magese amewaeleza vijana wa kike katika semina hiyo kuwa, wawe wazi pindi wajisikiapo dalili mbalimbali wakati wanapokuwa katika mzunguko wa siku zao ambapo na kubainisha kuwa, jambo hilo endapo litabainika mapema ni rahisi kulipatia tiba kuliko kuficha na kufika steji mbaya.
Mwanadada, Millen Magese pia alitumia wasaha huo kuishukuru Serikali kwa namna walivyokubaliana kushirikiana naye bega kwa bega katika mapambano dhidi ya tatizo hilo hapa nchini ambapo pia amewashukuru wadau wote kwa kuwa naye dhidi ya mapambano hayo.
Semina hiyo pia imeweza kukusanya watu mbalimbali wakiwemo watu maarufu wasanii, wanamitindo na wabunigu wa mavazi, wafanyabiashara na wanaharakati wanawake katika maendeleo hapa nchini huku wanaume nao wakijumuika pamoja ilikusambaza ujumbe huo kwa wenza wao na marafiki zao.
Tazama MO tv, kuona tukio hilo hapa:

DSC_8338
Mwanadada, Millen Happiness Magese.
DSC_8343
Baadhi ya wanafunzi, wadau wanaosaidiana na mwanadada Millen Magese wakifuatilia semina hiyo.
DSC_8349
Baadhi ya wageni waalikwa, wakiwemo waliowahi kushiriki mashindano ya ulimwende hapa nchini ..wakiwa wamejumuika pamoja kuungana na taasisi ya Millen Magese.
DSC_8353
Wanafunzi wakifuatilia semina hiyo.
DSC_8366
Wanafunzi wakifuatilia semina hiyo.
DSC_8370 DSC_8388
Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Bw. Rogers Shemwelekwa akitoa hotuba fupi katika semina hiyo
DSC_8382
Baadhi ya wadau walioungana kwa pamoja kusaidiana na taasisi ya Millen Magese wakifuatilia semina hiyo. Mustafa Hassanali pamoja na Rio Paul ambao wote ni wabunifu wa mavazi hapa nchini.
DSC_8478
Seven Mosha na Miss Tanzania 2008, Nasreen Kareem.
DSC_8394
Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, akitoa hotuba yake.
DSC_8380 DSC_8401
Mmoja wa madaktari bingwa wa wanawake wa Hospitali ya Muhimbili akitoa maelezo machache.

KIKOSI CHA UFARANSA CHAKAMATA MELI ILIYOJAA SILAHA ZINAZOPELEKWA SOMALIA

Kikosi cha askari cha majini cha Ufaransa kinachofanya dori kaskazini mwa bahari ya India kimeikamata meli iliyojaa sialaha zinazosemekana zilikuwa zinapelekwa nchini Somalia.

Mamia ya bunduki zikiwemo aina ya machine gun pamoja silaha za makombora zimekutwa kwenye meli hiyo.

Silaha zilizokamatwa zipo katika orodha ya zilizopigwa marufuku na Umoja wa Mataifa kuingia mikononi mwa makundi ya wapiganaji wa Somalia.