Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati Dk. Juliana Pallangyo
(pichani) akifungua mkutano unaoshirikisha wakurugenzi wa mashirika ya umeme
katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya
umeme. 
 Sehemu
ya watendaji na wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini
mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, wakifuatilia hotuba
iliyokuwa inatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk.
Juliana Pallangyo (hayupo pichani). 
 Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo
(kulia) na  Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la  Umeme Nchini (TANESCO) Mhandisi Decklan
Mhaiki (kushoto) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na mwenyekiti wa
kamati ya nchi za kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya  umeme, Josh Chifamba (hayupo pichani)
 Mwenyekiti
wa kamati ya nchi za kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya
umeme, Josh Chifamba (kulia) akimkabidhi zawadi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini anayeshughulikia 
masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (kushoto) aliyekuwa mgeni  rasmi kwenye ufunguzi wa mkutano huo.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo
(aliyekaa mbele katikati) akiwa  katika
picha  ya 
pamoja na sehemu ya  watendaji na
wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika
zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, mara baada ya  ufunguzi wa mkutano huo.
Na
Greyson Mwase, Dar es Salaam
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati,
Dk Jualiana  Pallangyo amewataka
wawekezaji binafsi nchini kujitokeza kwa wingi na kuwekeza katika uzalishaji na
uuzaji wa nishati ya umeme  nchini
ili  iweze kuchangia katika ukuaji wa
uchumi wa nchi.
Dk.
Pallangyo alisema hayo kwenye mkutano unaokutanisha wakurugenzi wa mashirika ya
umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara
ya umeme. Nchi hizo ni pamoja na 
Bostwana, Msumbiji, Afrika ya Kusini, Lesotho, Namibia, Jamhuri ya
Demokrasia ya Kongo, Swaziland, Zambia na Zimbabwe. Lengo la mkutano huo wa
siku moja lilikuwa ni kujadili changamoto zinazozikumba nchi wanachama katika
uzalishaji  na uuzaji  wa umeme ikiwa ni pamoja na kubadilishana
uzoefu.
Aliongeza
kuwa  wawekezaji binafsi wanaweza
kuzalisha   umeme kupitia  vyanzo mbalimbali vya nishati ikiwa ni pamoja
na maporomoko madogo ya maji, upepo, bayomasi na  jua kutokana na uwezo wao.
Akielezea
fursa za uwekezaji nchini, Dk. Pallangyo alisema kuwa wawekezaji wanaweza
kuwekeza  kupitia ujenzi wa miundombinu
ya usambazaji  wa umeme, uendelezaji wa
miradi ya umeme unaotokana na maporomoko madogo ya maji na  vyanzo 
vingine  ikiwa ni pamoja na
jotoardhi, upepo na uanzishwaji wa viwanda vidogo kwa ajili ya utengenezaji wa
vifaa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umeme.
Dk.
Pallangyo aliongeza kuwa ushiriki wa 
sekta binafsi  katika sekta ya
umeme umeongezeka kila mwaka na kusisitiza kuwa serikali bado inaendelea na
mikakati ya kuwawezesha wawekezaji binafsi 
katika  uzalishaji ya umeme
nchini.
Aliongeza
kuwa serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji nchini  ikiwa ni pamoja na sera na sheria
mbalimbali  zinazotumika kama mwongozo na
kutaja kuwa ni pamoja na sheria ya umeme ya mwaka  2008, sera ya nishati ya mwaka 2003 ambayo
inahamasisha ushiriki wa sekta binafsi katika sekta ya umeme.
Alitaja
sheria nyingine kuwa ni pamoja na ile ya Mamlaka ya Udhibiti  wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ya mwaka
2001, sheria ya  Wakala wa Nishaji  Vijijini (REA) ya mwaka 2005.
Akielezea
mikakati ya serikali katika upatikanaji wa nishati ya  uhakika, Dk. Pallangyo alisema kuwa serikali
imeweka mkakati wa  kuhakikisha kuwa
ifikapo mwaka 2025 asilimia 75 ya wananchi wote hasa waishio  vijijini wanapata nishati ya umeme ambayo ni
ya uhakika.
“Tunatarajia
kuzalisha hadi   megawati 10,000 za umeme
ambao utachochea ukuaji wa uchumi wa nchi kupitia viwanda na hivyo nchi kutoka
katika kundi la nchi masikini duniani na kuwa 
katika kundi la nchi zenye kipato cha kati  duniani,” alisisitiza Dk. Pallangyo.
Akielezea
hali ya upatikanaji wa umeme nchini, Dk. Pallangyo alisema kuwa umeme
unaozalishwa ni megawati 1461.69 huku mahitaji halisi yakiwa ni megawati 1026.
Umoja
wa  nchi zinazoshirikiana katika sekta ya
umeme kusini mwa Afrika (Southern African Power Pool; SAPP) ulianzishwa Agosti
mwaka 1995 katika Mkutano wa  Umoja wa
Nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la  Sahara
(SADC) ambapo walisaini makubaliano kwa ajili ya  kushirikiana katika uzalishaji na biashara
ya  umeme wa pamoja.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni