MKE WA ALIYEKUWA RAIS WA KENYA, MAMA LUCY KIBAKI ALAZWA HOSPITALI

Mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki, Mama Lucy Kibaki amelazwa hospitali Jijini Nairobi hapo jana.

Kumekuwa na taarifa za kuchanganya kuhusiana na hali yake, huku msemaji wa familia akisema hali yake ni njema anafanyiwa vipimo tu.

Hata hivyo vyanzo vingine vya habari nchini Kenya vimedai kuwa Lucy Kibaki ambaye hajaonekana hadharani kwa muda sasa amelazwa kwenye chumba maalum cha uangalizi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni