Kamishna
 Jenerali wa Magereza John C. Minja( wa pili kushoto) akikagua maeneo 
mbalimbali ya Gereza Bukoba alipofanya ziara ya kikazi leo Machi 11, 
2016 (wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera, SACP. Omari
 Mtiga (wa pili kulia) ni Mkuu wa Gereza Bukoba, ACP. Benizeth Bisibe.
Mkuu
 wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella akiongea ofisini kwake na Kamishna
 Jenerali wa Magereza John C. Minja na ujumbe wake (hawapo pichani)
Mkuu
 wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella akiongea ofisini kwake na Kamishna
 Jenerali wa Magereza John C. Minja na ujumbe wake kama inavyoonekana 
katika picha.
Jaji
 Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba Mhe. Sivangilwa Mwangesi 
Akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza John C. Minja 
alipomtembelea ofisini kwake.
Kamishna
 Jenerali wa Magereza John C. Minja (wa nne kushoto) akiwa katika picha 
ya pamoja na Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Mkoani Kagera mara 
baada ya kutembelea Gereza la Wilaya ya Bukoba (Picha na Lucas Mboje wa 
Jeshi la Magereza). 
Kamishina Jenerali wa 
Mageraza nchini John Carmir Minja afanya ziara ya kikazi  Mkoani Kagera 
yenye lengo la kutembelea na kukagua Magereza ya Mkoa wa Kagera pamoja 
na kujionea miradi ya uzalishaji inayosimamiwa na Jeshi hilo. 
Akiwa
 Mkoani hapa Kamishna Jenerali Minja alifika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa
 Kagera Mhe. John Mongella na kufanya naye mazungumzo kuhusu utendaji 
kazi na ufanisi wa Jeshi la Magereza Mkoani hapa katika kuimarisha 
ulinzi na usalama. 
Aidha katika mazungumzo hayo walizungumzia  
changamoto ya  msongamano wa Mahabusu katika Gereza la Wilaya ya Muleba 
ambalo hivi sasa linatumika kuhifadhi Mahabusu wa Wilaya ya Muleba na 
Wilaya ya Chato Mkoani Geita ambayo haina Gereza la Wilaya. 
Kamishna
 Jenerali wa Mageraza nchini John Carmir Minja pia alitembelea Mahakama 
Kuu Kanda ya Bukoba na kufanya mazungumzo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama 
hiyo Mhe. Sivangilwa Mwangesi juu ya namna ya kuongeza kasi ya 
usikilizwaji wa kesi mbalimbali za watuhumiwa ili kuondoa msongamano 
Magerezani. 
Vilevile Kamishna Jenerali Minja alitembelea Gereza 
la Wilaya la Bukoba na kuongea na wafungwa na Mahabusu wa Gereza  hilo 
pia na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la zahanati ambalo lipo katika 
hatua za mwisho kukamilishwa ili liweze kutoa huduma za afya kwa 
wafungwa na watumishi wa Jeshi hilo pamoja na wananchi wanaoishi jirani 
na zahanati hiyo. 
Kamishna Jenerali Minja yupo Mkoani Kagera kwa
 siku 7 kuanzia tarehe 10 hadi 16 Machi, 2016 ambapo lengo la ziara hiyo
 ni kutembelea na kukagua Magereza ya Mkoa wa Kagera pamoja na kujionea 
miradi ya uzalishaji inayosimamiwa na jeshi hilo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni