MARCO ROBIO AMSHAMBULIA VIKALI MROPOKAJI DONALD TRUMP

Muwania urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Marco Rubio amemshambulia mwenzake Donald Trump kwa kusema kuwa Uislam unaichukia Marekani, katika mdahalo uliorushwa kwenye televisheni huko Miami.

Bw. Rubio, ambaye anakazi kubwa ya kupambana hadi kufa kushinda kura za maoni za wanachama huko Florida jumanne, amesema kuna tatizo la itikadi kali katika Uislam, lakini waislamu wengi wanajivunia Marekani.

Mgombea huyo amemkubusha Bw. Trump kwamba marais hawapaswi kusema kila wanachotaka kusema, kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha madhara, kauli ambayo ilishangiliwa mno na watu waliohudhuria mdahalo huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni