Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na 
Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiombewa na  Askofu Mkuu wa Dayosisi ya 
Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex 
Malasusa na Mchungaji Charles Mzinga wakati wa Ibada ya Pasaka katika 
Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na 
Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Mama Rebecca Malasusa na Askofu 
Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri 
Tanzania Dkt. Alex Malasusa baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la 
KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016 
 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 
akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya 
Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex 
Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika 
Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016 
 
Kwaya wakati wa  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016 
 
 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na 
Mkewe Mama Magufuli wakishiriki na waumini wengine Ibada ya Pasaka 
katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27,
 2016 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na 
Mkewe Mama Janeth Magufuli wakisalimiana na waumini baada ya Ibada ya 
Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo 
Machi 27, 2016 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 
akisalimiana na kikundi cha Matarumbeta na Kwaya baada ya Ibada ya 
Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo 
Machi 27, 2016 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 
akisalimiama na Mama Rebecca Malasusa, mke wa  Askofu Mkuu wa Dayosisi 
ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex
 Malasusa baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front
 jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na 
Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiagana -na  Askofu Mkuu wa Dayosisi ya 
Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex 
Malasusa na Mchungaji Charles Mzinga wakati wa Ibada ya Pasaka katika 
Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016 
 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 
akisalimiana na Mchungaji Charles Mzinga alipowasili kwa Ibada ya Pasaka
 katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 
27, 2016 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 
 akiwapungia waumini baada ya  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la 
Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016 
PICHA NA IKULU
…………………………………………………………………………..
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi watanzania kuendelea kuwa 
wamoja na kushirikiana kuijenga nchi yao, badala ya kubaguana.
Rais Magufuli ametoa wito huo leo 
katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa 
Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya Pasaka pamoja
 na waumini wa kanisa hilo.
Amesema Mwenyezi Mungu alimtoa 
mwanae wa pekee Yesu Kristo kuja kuikomboa dunia bila kuwabagua 
wanadamu, vivyo hivyo nasi binadamu tunapaswa kutobaguana, iwe kwa dini 
zetu, makabila yetu, mitazamo ya kisiasa na hata rangi zetu.
Aidha, Rais Magufuli amewakumbusha
 watanzania kufanya kazi kama ambavyo vitabu vitakatifu vinasisitiza 
umuhimu wa kufanya kazi, na amebainisha kuwa Tanzania yenye neema 
inawezekana endapo kila mtu atazingatia kufanya kazi.
“Tukifanya kazi hatuhitaji hata 
misaada kutoka nje, nchi hii ina neema nyingi. Kwa kweli tukifanya kazi 
kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi nyingine na sio
 kuomba misaada kutoka nchi nyingine” Amesisitiza Dkt. Magufuli.
Rais Magufuli ambaye amesali 
kwenye kanisa hilo kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini ikiwa ni mara yake ya nne kusali
 katika kanisa hilo hata kabla ya kuwa Rais, amewaomba watanzania 
kuendelea kuliombea Taifa lao na pia kumuombea yeye ili afanikiwe 
kutekeleza jukumu kubwa na zito la kuiongoza nchi.
Pamoja na kuongoza maombi ya 
kumuombea Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli waliohudhuria 
ibada hiyo, Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. 
Alex Malasusa amempongeza Rais Magufuli kwa tabia yake ya kupenda 
kuhudhuria ibada na kuwasihi viongozi wengine kupenda ibada.
Askofu Malasusa ameuelezea ufufuo 
wa Yesu Kristo kuwa jambo la kuleta  matumaini, na hivyo amepongeza 
mwelekeo wa nchi kwa sasa, huku akisema Kanisa linaona matumaini kwa 
Taifa.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
27 Machi, 2016
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni