Walemavu
 wakishangilia kwa pamoja na viongozi wa kampuni ya GAPCO ambao walikuwa
 ndiyo wadhamini mbio za kilomita 10, za Kilimanjaro Marathon 2016 
zilizofanyika mjini Kilimanjaro mwishoni mwa wiki iliyopita. 
 Walemavu
 wakianza kutimua mbio za kilomita 10, za Kilimanjaro Marathon 2016 
zilizokuwa zimedhaminiwa na kampuni ya GAPCO na kufanyika mjini 
Kilimanjaro mwishoni mwa wiki iliyopita.
Viongozi
 wa kampuni ya GAPCO wakiwa na Mgeni Rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (wa pili toka kushoto) akiwaangalia 
walemavu wakitimua mbio za Kilometa 10 za Kilimanjaro Marathon 2016 
zilizokuwa zimedhaminiwa na kampuni ya GAPCO na kufanyika mjini 
Kilimanjaro mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mmoja
 ya walemavu Vosta Peter (30) kutokea Dar es Salam akiongoza katika mbio
 za Kilometa 10 za Kilimanjaro Marathoni 2016 zilizokuwa zimedhaminiwa 
na kampuni ya GAPCO na kufanyika mjini Kilimanjaro mwishoni mwa wiki 
iliyopita.
Kila mmoja akionyesha ustadi wa kuendesha baskeli.
Mwanadada
 Linda Macha (32) ambaye aliweza kuwashinda wenzake katika mbio za 
Kilometa 10 za Kilimanjaro Marathoni 2016 zilizokuwa zimedhaminiwa na 
kampuni ya GAPCO na kufanyika mjini Kilimanjaro mwishoni mwa wiki 
iliyopita. 
Mshindi
 wa mbio za Kilometa 10 za Kilimanjaro Marathon 2016, Vosta Peter (30) 
akishangilia mara baada ya kumaliza. Mbio hizo za Kilometa 10 
zilidhaminiwa na kampuni ya GAPCO na kufanyika mjini Kilimanjaro 
mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mshindi
 wa kwanza kwa mbio za walemavu kilomita 10, Vosta Peter (30) akipokea 
cheki ya Shilingi Milioni Moja kutoka kwa kampuni ya GAPCO, 
wanaomkabidhi ni Meya wa Manispaa ya Moshi Raymond Mboya (kushoto), 
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Gapco Afrika Mashariki, Macharia Irungu 
(anayepiga makofi toka kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa GAPCO 
Tanzania, Vijay Nair. 
Picha zote na Cathbert wa Kajunason Blog.
Na Cathbert Kajuna - Kilimanjaro. 
Mkurugenzi
 Mkuu wa Kampuni ya GAPCO Afrika Mashariki, Macharia Irungu amewataka 
wanamichezo kujibidishe kwa kufanya mazoezi mara kwa mara ili waweze 
kufanya vizuri katika mashindano wanayoshiriki. 
Akizungumza
 mwishoni mwa wiki mjini Kilimanjaro wakati wa Mashindano ya Kilimanjaro
 Marathoni 2016, ambapo GAPCO ndiyo waliodhamini upande wa Walemavu, 
alisema kuwa wanamichezo wengi walemavu na hata wasiowalemavu hujisahau 
sana kufanya mazoezi ya kutosha jambo linalowafanya wengi wao kutoweza 
kufanikiwa kushinda kwenye mashindano. 
Aliongeza
 kuwa wao kampuni ya GAPCO waliweza kujitolea kuwasaidia walemavu ili 
waweze kuonyesha vipaji vyao japo mwanzo waliweza kuwasisitiza wafanye 
mazoezi na ndiyo maana wameweza kufanya vyema. "Napenda kuwaasa 
wanamichezo wale walemavu na wasio walemavu, wapende kujitoa kufanya 
mazoezi ya kutosha maana siri ya ushindi ni mazoezi wala hakuna muujiza 
unaoweza kukupa ushindi kama haujajitoa kufanya mazoezi ya kutosha," 
alisema Irungu. 
Kwa 
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya GAPCO Tanzania, Vijay Nair
 alisema wamefurahishwa na mahudhurio ya watu wenye ulemavu waliojitoa 
kushiriki mashindano hayo, na wao hawatawatupa wataendelea kuwa nao bega
 kwa bega. Bw. Nair aliwaasa walemavu wawe na moyo wa upendo na 
mshikamano ili waonyeshe mfano bora hata wanapojitokeza kusaidiwa 
wafaidike kwa pamoja. 
Mashindano
 ya mbio za Kilimanjaro marathon za 10KM kwa walemavu zilidhaminiwa na 
GAPCO ambapo shindano lilijumuisha baiskeli za walemavu zenye matairi 
matatu zenye viwango vya kimataifa wapatao 60 kutoka Dar es Salaam, 
Arusha, Moshi na Zanzibar.









Hakuna maoni:
Chapisha Maoni