Golikipa mahili wa Mbeya City Fc, Juma K Juma  amerejea kikosini 
kutoa mapumziko ya majuma mawili aliyopewa na kocha  Kinnah Phiri 
kufuatia  mkwewe Bi Nasra Nassor kujifungua watoto mapacha hivi 
karibuni.
Akizungumza na mbeyacityfc.com  muda mfupi uliopita Kaseja amesema 
kuwa amefurahi kusafiri na hatimaye kurudi salama kwenye timu yake huku 
pia akitoa shukurani zake za dhati wa wale wote ambao wamekuwa karibu 
nae yeye kama mchezaji na pia familia yake tangu alipojiunga na City.
“Nashukuru mungu nimefika hapa salama baada ya safari 
yangu, pia namshukuru kwa kile alichonijaalia, nimerudi kikosini nikiwa 
na ari kubwa zaidi  ili kuituikia timu yangu kwa nguvu zote  katika 
kutafuta mafanikio hasa kwenye kipindi hiki  ambacho ligi inaelekea 
mwishoni, hakika tunapita kwenye kipindi kigumu lakini  umoja wetu 
utatufanya kuvuka hapa” alisema.
Akiendelea zaidi Kaseja  aliyewahi kucheza kwa mafanikio kwenye timu 
za Moro United, Simba, na Yanga aliweka wazi kuwa anaimani kuwa na kocha
 Kinnah Phiri kuwa ataijenga upya City na kuifanya kuwa timu 
itakayotisha zaidi kwenye msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania 
Bara.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni