MTEKAJI NDEGE YA MISRI AWAACHIA HURU ABIRIA NA KUJISALIMISHA

Tukio la kutekwa ndege ya abiria ya Misri na kupelekwa kisiwa cha Cyprus limemalizika huku abiria wote waliotekwa wakiachiwa huru na mtekaji kujisalimisha.

Ndege hiyo ya shirika la EgyptAir Flight MS181 ilitekwa na abiria mmoja mwanaume ambaye alidaiwa kuvaa kiunoni mkanda uliokuwa na milipuko.

Maafisa wa shirika la ndege la Misri wamesema wameambiwa na mamlaka za Cyprus kuwa mkanda huo wa mabomu ulikuwa ni feki.
                                           Abiria wakishuka kwenye ndege ya Misri iliyotekwa
Abiria walioshuka wakiwa kwenye uwanja wa ndege wa nchini Cyprus baada ya kuachiwa huru na mtekaji

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni