WAZIRI
 MKUU Kassim Majaliwa amekagua hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kagera na 
kumpa siku tano Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw. Adam Swai amletee 
taarifa juu matumizi ya sh. Milioni 80 ambazo ni fedha za UKIMWI.
Pia
 amemtaka ifikapo Machi 20, nwaka huu awasilishe taarifa nyingine ya 
matumizi ya sh. Milioni 40 za ukarabati wa jengo la wagonjwa maalum  
(Grade A)
Ametoa
 agizo hilo leo asubuhi (Jumanne,  Machi 15, 2016) wakati akizungumza na
 watumishi wa hospitali hiyo baada ya kutembelea maeneo kadhaa yakiwemo 
wodi ya watoto, wodi ya wazazi, chumba cha wagonjwa mahututi (ICU ) na 
chumba cha kuhifadhia maiti.
"Kulikuwa
 na frsha za ukimwi sh. Milioni 80 ambapo kila mtumishi alipaswa kupata 
sh. 200,000/- lakini ninyi mmewapa sh. 80,000 /-. RAS fedha hizi 
zimeenda wapi?  Nataka uniletee taarifa ofisini kwangu Dar es Salaam 
ifikapo tarehe 20 mwezi huu," alisema huku akishangiliwa.
"Kwa
 mujibu wa taarifa ya CAG pale grade A kuna mgogoro wa sh. milioni 40. 
Wewe taarifa unayo lakini hujaifanyia kazi yoyote.  Nataka tarehe 20 
nayo hii pia niipate na nione umetoa mapendekezo gani."
Kuhusu
 tatizo la madaktari katika hospitali hiyo, Waziri Mkuu alisema 
atawasiliana na Waziri wa Afya ili madaktari watano ambao wanasubiri 
ajira rasmi lakini wameanza kazi kwa mkataba hospitali hapo wapewe ajira
 rasmi. Pia alisema amebaini upungufu wa madaktari bingwa uliopo katika 
hospitali hiyo.
Pia
 aliahidi kufuatilia maombi yao ya gari la wagonjwa hasa ikizingatiwa 
kuwa anayo maombi kama hayo kutoka hospitali za Mawenzi (Kilimanjaro), 
na Ligula (Mtwara).
Katika hatua nyingine, 
 Waziri Mkuu aliwapongeza watumishi wa hospitali hiyo kwa huduma zao 
nzuri wanazotoa kwa wagonjwa.  "Nineridhishwa na kauli walizotoa 
wagonjwa juu yenu. Tofauti na hospitali nyingine nilizopita, wao 
wamesema hawajatozwa fedha ili wapatiwe dawa. Nimefarijika sana."
"Endeleeni
 kuwa na huruma kwa wagonjwa. Endeleeni kuwa na lugha nzuri kwa 
wagonjwa. Hawa wagonjwa hawakuogopa kuelezea hisia zao. Wamesema kwa 
uwazi kabisa kwamba mnawajali," alisema.
Mapema, 
 akisoma taarifa mbele ya Waziri Mkuu,  Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dk.  
Thomas Rutachunzibwa alisema hospitali hiyo inakabiliwa na upungufu 
mkubwa wa madaktari bingwa pamoja na madaktari wa kawaida.
"Tunao
 madaktari 10 lakini wanaohitajika ni 30. Tunao madaktari wasaidizi 
wanane lakini wanaohitajika ni 23 na madaktari bingwa waliopo ni watatu 
tu lakini wanaohitajika ni 24. Tunaomba tupatiwe watumishi hawa ili 
tuweze kutoa huduma kulingana na matarajio ya wananchi wetu," alisema.
Akifafanua
 kuhusu mahitaji ya hospitali hiyo, Dk. Rutachunzibwa alisema wanahitaji
 sh. bilioni 1.8 kwa mwaka bila ya kuweka mishahara ili waweze kufanya 
kazi yao kwa umakini. "Tunahitaji sh. milioni 802 kwa ajili ya matumizi 
ya kawaida lakini tunachopokea hivi sasa ni sh. milioni 299 ambayo ni 
sawa na asilimia 30 ya mahitaji yetu."
"Bajeti
 ya dawa tuliyotenga ni sh. milioni 960 lakini tunapokea sh. milioni 143
 ambazo kiuhalisia zinatosha kwa matumizi ya miezi miwili tu. 
Tumelazimika kufanya marekebisho ya bei za dawa kwa ridhaa ya Bodi ya 
hospitali ili tuweze kumudu kutoa huduma kwa wananchi," alisema.
Alisema
 ili kubana mianya ya upotevu wa mapato, wanahitaji kuwa na kompyuta 15 
lakini hadi sasa wamefanikiwa kununua kompyuta mbili tu ambazo ziko 
Grade A na idara ya wagonjwa wa nje (OPD) ili kuimarisha utaratibu wa 
ukusanyaji mapato.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMANNE, MACHI 15, 2016.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni