SERENA WILLIAMS AONDOLEWA MICHUANO YA MIAMI OPEN NA SVETLANA KUZNETSOVA

Mchezaji tenesi namba moja na bingwa mtetezi, Serena Williams ameondolewa katika raundi ya nne ya michuano ya Wazi ya Miami.

Katika mchezo huo Mmarekani Serena alipoteza mchezo kwa seti 6-7 (3-7) 6-1 6-2 dhidi ya Mrusi Svetlana Kuznetsova, na kuondolewa mapema mno katika michuano hiyo.

Serena Williams, 34, aliyetwaa mataji 21 ya Grand Slam alikuwa akijaribu kushinda taji lake la tisa la michuano hiyo ya wazi ya Miami.
           Serena Williams akishindwa kujizuia kuonyesha huzuni kwa kuondolewa
      Svetlana Kuznetsova akizuia mpira uliopigwa na Serena Williams katika mchezo huo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni